Msaada jamani wanajf

Vatican

Member
Feb 18, 2013
22
4
Tumsifu Yesu Kristo, nawaomba mniombee jamani nipate kazi wakati wa kusali na kuomba kwenu, nimemaliza shahada ya maendeleo ya jamii mwaka 2010, hadi leo sijapata kazi. ninapigana kwa hali yote lakini namini Bwana Wetu Yesu Kristo atatenda maajabu juu yangu na familia yangu, kupitia maombi yenu jamani. nipo tayari kufanya kazi yeyote.
Neema ya Bwana Wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
 
Hahahaha,Sasa kama muajiri ni muislam kwa maombi hayo shughuli ipo.

Ushauri wa Bure:
Jaribu kufanya ibada sana,na kama unakunywa Pombe acha kabisaa.
Then Funga siku mbili kwa wiki na mungu atakufungulia.(Funga alkhamis na Jumatatu)

Ila uweke imani kwa mungu na wala usimjaribu.Na Pia uwe Tayari kufanya kazi kwa Kipato chochote anglau chenye kukidhi chakula cha familia then mengine yatafuata.

Tatizo ambalo limelojitokeza kwa sasa kwa watu wenye Degree wanajiona kwamba wao VIP na hawawezi kufanya kazi za kipato cha chini.kaa utambue kwamba siku hizi Degree sio kitu kabisa katika ajira zaidi ya kuongeza CV.
Muhim ni uaminifu katika kazi na ujuzi wa kazi.

Then Fikiria kujiajiri mwenyewe
Mifano ipo Hai tu watu waliojijiri kama mamalishe/Babalishe wao wanaingiza pesa kwa mwezi kuliko Aliepo ofisini na AC.
Na ndio maana kwa uchunguzi wangu mie niliejenga huko Chanika,kila mtaa utasikia mwenye kiwanja ni mamalishe na wengine wanasomesha watoto hadi chuo kikuu na wengine wananyumba za maana,Ila walioajiriwa wengie wanaishia kupanga tu
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom