wiseboy
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 2,931
- 3,299
HELLOW G.T...Jamani nilikuwa nimefanikiwa kununua tetea 80 na jogoo 8, lengo langu ilikuwa kununua tetea 150 wa kuku wa kienyeji, na hao kuku nilikuwa nshawapa chanjo ya mdondo (new castle) ila katika khali ya kuendelea kuongeza matetea nilinunua tetea wawili kama wiki mbili nyuma, hawa tetea mmojawapo alipofika tu akaanza kuharisha mharo mweupe nikampa antibiotic, hakupata nafuu na akaanza kukoroma yaani kupumuwa kwa shida ilibidi nimchome pen strep, hakupata nafuu akafa, yule mwenzake naye akakaa kama wiki nae akafa......nikawafukia, sasa ajabu wakafuatia vifaranga wakubwa wakubwa nikaamuka asubuhi na kukuta wamekufa 15 gafla, 20 wakaonyesha dalili zile za kuku mgonjwa na wakafa, sasa kwa kuku wakubwa 15 wako crius wanakoroma, wanaharisha mharo mweupe na wamezubaa, sasa naomba kuuliza nitumie dawa gani hapa? je ni kideri? je ile chanjo haikufanya kazi japo nimechanja mara 2....... nasikitika nitapoteza utitiri wa kuku wangu.