Fahamu kuhusu kuanzisha biashara ya Mobile Money (M-Pesa, Tigopesa)

Mrekebishaji

Senior Member
Mar 19, 2009
168
63
shutterstock_364493930_money-transfer-via-mobile-1600x880.jpg



Wana jukwaa,

Naomba maelezo ya namna ya kuwa wakala wa M-PESA pamoja na uuzaji wa luku.

Ikiwezekana kama kuna mtu anayehusika moja kwa moja naomba kumuona. Nipo Dar es Salaam
Nilipata kuulizia M-pesa wao mtaji wa kufungua duka moja la M-PESA wanahitaji 1,000,000 (one million).

Unatakiwa uwe na TIN number, leseni ya biashara, fremu ya kuanzisha mradi, kitambulisho hata cha mpiga kura nadhani kinafaa.

Kwa biashara inalipa I can tell you, brother japo sijawahi kuifanya. Cha msingi uwe na mtaji imara na wateja wako wawe na uhakika kwamba wakati wowote wakija kwa kibanda chako kutaka kutuma au kutoa kiasi flani cha pesa basi watapata huduma hiyo.

Tatizo kubwa ni wengi wanakuwa na mitaji ya kuzuga ukishataka kutoa zaidi ya laki mbili anakwambia hamna network kumbe fedha hana.

Unaweza pamoja na biashara hiyo ukaunganisha na kusajili, kufanya replacement na kutengeneza special number, kuwa wakala wa EVD (kumbuka pia utakua unalipwa na makampuni ya simu commission)... So ukiwa una mix vibiashara vyote hivyo kwa mitandao yote hasa tigo voda na airtel mwisho wa mwezi unaweza kuwa unapiga faida hata 1,000,000 au zaidi.

Changamoto ya biashara hiyo ni wapita njia wa kutosha na ka mtaji kako kukatuliza, ikiwezekana kuukuza pia, ili kuyaongeza maduka yafikie angalau matatu...

TRY IT MKUU, I'M ENCOURAGING YOU
��
TransactionAgent commission model (ex VAT)
From ToDeposit commissionWithdraw commissionTotal commission
1,000 9,999 200 300 500
10,000 19,999 200 400 600
20,000 49,999 300 400 700
50,000 99,999 400 600 1,000
100,000 199,999 600 800 1,400
200,000 299,999 800 1,300 2,100
300,000 399,999 1,000 1,800 2,800
400,000 500,000 1,000 2,500 3,500
Registration Tshs 500 once off

Hayo ndio mapato ya wakala anaye deposit na anaye withdraw. Hapo vodacom wameshatoa sehemu yao. Hii commission inakusanywa unalipwa kwenye simu yako ya head office kila mwisho wa mwezi. Kama upo chini ya wakala mkuu unakatwa 20% anapewa yeye.

wapalepale post
Heshima kwenu,
1. M PESA
2. Tigo pesa
3. Airtel money
4. CRDB fahari huduma
5. Kifaa cha max malipo kwa ajili ya luku etc

Jamani ndugu yenu nafikiria kuanzisha hii biashara ya u-wakala wa m-pesa. Mwenye details kidogo kuhusu hii biashara anijuza hasa nataka kufahamu kuhusu:

1. Kiwango cha chini cha mtaji unao hitajika
2. Jinsi faida inavyopatikana
3. Jinsi ya kujisajiri (hili nadhani sio issue sana naweza kwenda kwa voda wenyewe) itanirahisishia zaidi

Nawasilisha
================​

Mimi ni wakala wa M-Pesa kitambo sana sijawahi tapeliwa,inalipa sana kama tu goli lako lipo sehemu yenye mchanyiko wa watu wengi na kama unaielewa vizuri biashara hiyo.Unahitaji kuwa na laini,TIN na eneo la kufanyia biashara
kumsajili mteja ni Tsh 500/- kamishen

mteja aliyesajiliwa akiweka pesa kwa mara ya kwanza unapata tsh 2000 kamisheni akituma pesa kwako unapata kamisheni kuanzia tsh 300/- hadi tsh 5000/- inategemeana ametuma kiasi gani
akitoa pesa kwako unapata kamisheni kuanzia tsh500/- hadi tsh 5000/- inategemeana katoa shilingi ngapi

akinunua airtime kwako unapata karibia 10% kamisheni ya airtime aliyonunua
akinunua Luku unapata kamisheni kadhaa
Biashara hii ili ufanikiwe zaidi unaweza kuichanganya na biashara nyingine kama kuuza luku, na vinywaji baridi kama soda na juisi ambavyo havihitaji mtaji mkubwa au kama una biashara yako tayari halafu ukaongezea hii biashara kama ziada

Yaani kwa kijana wa kitanzania wa kawaida akiwa serious inaweza akatolewa na biashara hii kwa ufupi ZAP,M-pesa na Tigo Pesa kama una magoli matatu au maanne kipato cha mwezi ni net 2m, yanini kuajiliwa sasa?

================​

Faida yake inategemea yafuatayo:

Ufanisi wako (via Operator) wa kazi;
Kama service ni nzuri hasa in unavyowasikiliza na kuwashughulikia wateja, hii inahusisha mhudumu wako kua haraka na kujua huduma zote.

Mfano: mteja anaweza asijue jinsi ya kutumia akaunti yaM-pesa, hapo ina maana Mhudumu awe mpole amsaidie.

uwe na mtaji wa kutosha ili kuhakikisha mteja akija kutoa au kutuma pesa anapata
hii itasaidia kuptopoteza miamala kwa kukosa pesa na pia itamfanya mteja awe anaiamini sehemu yako hata siku nyingine kuja kwenye banda lako.
  1. Hakikisha jioni unafunga mahesabu pesa yako mkononi na kwenye laini. Kama jumla ilikuwa milioni mbili asubuhi jioni inatakiwa iwe hio hio milioni mbili
  2. Unapata pesa ya commission mwisho wa mwezi. Kama mtaji wako ni Million 5 kwa siku na inazunguka ipasavo na hio sehemu ina shughuli nyingi, kamisheni inaweza fikia hata milioni moja au zaidi
Changamoto
  1. Kama sehemu haina mzunguko wa pesa wa kutosha unaweza kupoteza muda wako, wateja wapo wa kutosha ni nadra kupata hasara. More inakua out of mistakes kama kutuma pesa mahala ambako sio husika kwa bahati mbaya.
  2. Unaweza ukatuma pesa kwa mtu mwingine ambaye sio mteja kwa bahati mbaya, japo pesa hii unaweza kupiga simu kwa vodacom halafu wakarudisha muhamala huo mara nyingine unaweza usiupate kama uliyemtumia atakuwa haraka kwenda kutoa
  3. Noti feki kama kuna wateja wanaweza wakakuletea mabunda ya pesa huku wakiwa wamechanganya na mabunda ya noti feki, kabalaya kuweka pesa kwenye droo yako hakikisha unaziangalia, kama unafanya hadi usiku nunua tube light ili kuwe na mwanga wa kutosha kugundua noti feki.
  4. Kuna vikwazo pia katika biashara hii, na kubwa likiwa ni suala zima la usalama kuna vibaka au majambazi wanaweza wakakutegea ukiwa unatoka wakakukaba, ni bora kuwa na sefu lako imara, kwenye fremu yako pia kunatakiwa kuwe na grili imara kuzunguka dirisha na mlango
 
Hii ni kutoka chanzo cha kuaminika.

Lazima uwe na leseni ya biashara halali na pia uwe na utambulisho wa mlipa kodi yaani TIN inayotolewa TRA.

Ukiwa navyo utaenda vodacom na utasaini mkataba baada ya kutimiza vigezo vingine vidogo lakini muhimu.
 
Nenda selcom posta ndo utapata full data wale mashine zao zinafanya kazi kibao lakin hii m-pesa sifahamu

Mkuu ukitumia machine za selcom au maximalipo huesabiki kuwa moja ya wakala wa Tanesco. Hao jamaa (selcom na maximalipo) ndio wenye mkataba na Tanesco. walicho fanya ni subcontract kama mkataba wa Tanesco unavyo sema.

Yaani Tanesco aliwakubalia selcom na maximalipo to subcontract under one condition. This condition is that lazima wateja wote watakao wa subcontract wauze Luku kwa bei ya Tanesco. Na mkataba unasema wasipo fanya hivyo then Tanesco kama mwajiri wa selcom na maximalipo will cancel their contract.

Tanesco wanatoa commission ya 3% sasa selcom na maximalipo they decided to share this profit with their customers. Wale wote wenye machine za maximalipo na selcom wanapata 1.5% na wajiri wao wanabakiza 1.5%. There4 ukizingatia hayo utajikuta kwamba unawafanyia kazi selcom au maximalipo.

Nivyema kwenda Tanesco kwa marketing manager Mr Mzava (huyu jamaa nimzuri sana) atakupa maelezo. Na kwa vile uko Dar atakwambia maeneo gani ambayo wanaitaji mawakala. Ukisha pata huo uwakala pia unaweza kufanya kazi kama selcom or maximalipo.

Kuna routers za 3G unaweza kutumia moja kwenye 50 POS kama za maximalipo. ila hii router bei yake iko juu sana lakini inafanya kazi nzuri sana. Hutotakiwa kuingia gharama kama za maximalipo au selcom.
 
You only need to have Tin no and bness licence! for M-PESA
At least 1ml is ok to enjoy the service but depends with location as well
All the best
 
Man ukifanikiwa kupata Luku also weka M-Pesa, Zap, Tigo pesa. Nitakupa mbinu how to get more business by using M-Pesa, Zap, na Tigo pesa and Luku. Hapo Dar sijaona watoa huduma ya Luku wakiitumia hiyo mbinu. It is too profitable if you are based in Dar.

I think kupata M-Pesa, Zap na Tigo Pesa ni rahisi sana ugumu uko kwenye Luku, lazima uwe na muda wakutosha na uvumilivu pia unatakiwa.
 
Man ukifanikiwa kupata Luku also weka M-Pesa, Zap, Tigo pesa. Nitakupa mbinu how to get more business by using M-Pesa, Zap, na Tigo pesa and Luku. Hapo Dar sijaona watoa huduma ya Luku wakiitumia hiyo mbinu. It is too profitable if you are based in Dar.
I think kupata M-Pesa, Zap na Tigo Pesa ni rahisi sana ugumu uko kwenye Luku, lazima uwe na muda wakutosha na uvumilivu pia unatakiwa.

Yep bro!

Hebu weka hadharani hizo mbinu na ss wa mashambani tuzione. Huku kwetu watu wanasafiri umbalimrefu, nauli elf10 kufuatilia umeme wa buk5, na mpesa nayo utata!..IDUMU JF!
 
Yep bro!
Hebu weka hadharani hizo mbinu na ss wa mashambani tuzione. Huku kwetu watu wanasafiri umbalimrefu, nauli elf10 kufuatilia umeme wa buk5, na mpesa nayo utata!..IDUMU JF!

Duh! mkuu it seem hapo mtaani kwako kuna opportunity sana, kutokana na maelezo yako mafupi kuna fedha zimezaga sana hapo. Kwanini usifanye hivi, pata kama Laki 3 or 5. Then weka Tigo pesa elf 50, Zap laki, the rest M-Pesa. Halafu weka bango la huduma ya M-Pesa, Zap, Tigo na LUKU. Kumbuka subject kubwa ni LUKU na M-PESA.

Let the charges for M-Pesa remain constant as per maelezo utakayo pata from wahusika. Kuhusu kuuza LUKU tumia Zap, umeme wa 1000-3000 charge 300, umeme wa 4000-9000 charge mia tano, umeme wa 10000-14000 charge elf, 15000-20000 charge 1500, na 21000 and above 2000

In most cases utakuta kwamba katika laki moja you make a profit of elfu 10 within a few hours. Kama mtaani kwako kuna demand kubwa ya Luku you will make alot of money. Ila you have to make sure that unapata mtu wako wa karibu Airtel so that whenever you need Zap anakurushia halafu unampelekea pesa yake kama mtakavyo elewana. Also make sure you become an agent wa Airtel, watakupa line special.

Normally M-Pesa inasumbua sana wakati wa kununua Luku don't use it kabisa, just use Zap it is the best.
 
@prime mkuu ubarikiwe kwa maelezo yenye tija kabisa nimepata mwanga wa kutosha kabisa
 
Wadau niaje? Pls nisaidieni kunipa info kuhusu biashara ya M-PESA, je inalipa? risk zake ni kama zipi?
kama kuna yeyote mwenye idea anisaidie pls.
 
Wadau niaje? pls nisaidieni kunipa info kuhusu biashara ya M-PESA, je inalipa? risk zake ni kama zipi?
kama kuna yeyote mwenye idea anisaidie pls.

Dada kapate maelezo yanayojitosheleza toka kwa Vodafone wenyewe. Kama uko nje ya nchi watumie email, natumai watakupa maelezo ya kutosha.

All the best.
 
Wandugu naombeni kuuliza manake kuna ndg.yangu anataka kuingia hii business ikoje?commission unapata ngap?kwa kuweka,kutuma nk!kwa yeyote anaeifanya naomba ufafanuzi manake sijui lolote!
 
Wanajamii naombeni kuuliza, Mimi anataka kuingia hii business ikoje? Capital gani inahitajika? Commission unapata ngapi?kwa kuweka,kutuma nk!kwa yeyote anaeifanya naomba ufafanuzi. Asanteni
 
Do research na nadhani hapa should be ur starting point utapata some tips ila uwatembelee wajasiriamali wanaofanya hiyo upate ufahamu zaidi.
 
Hazole, Dr Nashukuru wakuu kwa mawazo. ila nimewaona jamaa watatu wanaofanya hii biashara kila mmoja ananificha undani wake nikaona labda huku Jamvini kuna mtu anaiju zaidi. Wanajamii mko wapi?
 
Nilipata kuulizia M-pesa wao mtaji wa kufungua duka moja la M-PESA wanahitaji 1,000,000 (one million).

Unatakiwa uwe na TIN number, leseni ya biashara, fremu ya kuanzisha mradi, kitambulisho hata cha mpiga kura nadhani kinafaa...

Kwa biashara inalipa I can tell you, brother japo sijawahi kuifanya. Cha msingi uwe na mtaji imara na wateja wako wawe na uhakika kwamba wakati wowote wakija kwa kibanda chako kutaka kutuma au kutoa kiasi flani cha pesa basi watapata huduma hiyo...

Tatizo kubwa ni wengi wanakuwa na mitaji ya kuzuga ukishataka kutoa zaidi ya laki mbili anakwambia hamna network kumbe fedha hana.

Unaweza pamoja na biashara hiyo ukaunganisha na kusajili, kufanya replacement na kutengeneza special number, kuwa wakala wa EVD (kumbuka pia utakua unalipwa na makampuni ya simu commission)... So ukiwa una mix vibiashara vyote hivyo kwa mitandao yote hasa tigo voda na airtel mwisho wa mwezi unaweza kuwa unapiga faida hata 1,000,000 au zaidi.

Changamoto ya biashara hiyo ni wapita njia wa kutosha na ka mtaji kako kukatuliza, ikiwezekana kuukuza pia, ili kuyaongeza maduka yafikie angalau matatu...

TRY IT MKUU, I'M ENCOURAGING YOU
 
Back
Top Bottom