Msaada: Dawa gani nitumie kutibu hili tatizo la maumivu ya upande mmoja wa mshipa wa wa sehemu za uzazi

Shadow7

JF-Expert Member
Sep 28, 2020
12,378
17,041
Habari JF Doctors na wadau mbalimbali,

Nina kijana wa kiume miaka 19 anasumbuliwa na maumivu ya upande mmoja wa mshipa wa sehemu za uzazi, Tatizo hili limemuanza wiki moja nyuma ambapo palianza kuvimba kidogo kidogo lakini saivi pameongezeka na maumivu anasikia makali.

Chanzo cha tatizo alidondoka alipokua mpira wa miguu anacheza na wenzake.

Naomba wenye ufahamu wa hili wanisaidie tafadhali.
 
Kwanini kwanza usimpeleke hospitali wafanye examination ya hilo tatizo vizuri?..najua pia hapa ni Jf doctor lakini kwa cases kama hizi inabidi mtaalamu wa afya aone kwa macho ili matibabu yawe sahihi zaidi.
Nimeshampeleka wakampatia dawa za maumivu kisha wakamwambia atarejea katika hali yake lakini kila siku anazidi kulalamika maumivu yanaongezeka
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom