Msaada: Dada yangu anaangamia kwa ugonjwa Saratani ya Ini, damu na titi

Pole sana Mkuu...

Muendelee kumuomba Mwenyezi Mungu ili mapenzi yake, sio yenu, yatimizwe.

Ninawaombea kwa Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki cha mpito.
 
Saratani ya ini ni moja ya saratani mbaya sana. Kama imefikia hatua ya mwisho kama ulivyosema ni suala la kumuachia Mungu tu. Hayo mengine yatazidi kuwapa mawazo coz mtapoteza muda na pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tangu ulipoleta uzi wako kuna hatua ushachukua, au mgonjwa ameng'ang'aniwa hospitali?
Ndugu zangu,

Nipo/ tupo katika kipindi kigumu sana kama familia, dada yetu aligundulika kuwa saratani ya Ini, damu na titi. Vyote hivyo vipo katika stage ya mwisho na mbaya sana na Madaktari wametupasha kuwa hakuna kitu wataweza kufanya kunusuru uhai wa ndugu yetu.

Mioyo imejawa na simanzi kwani tangu juzi tarehe 17 february hali imezidi kuwa mbaya zaidi na yupo ICU anapumulia Oxygen.

Ombi langu ndugu zanguni, kama kuna anayeweza kutusaidia au kutuelekeza katika tiba au dawa mbadala ambazo pengine zinaweza kumponyesha au kumpa nafuu kidogo basi atusaidie ili tuweze kuokoa uhai wa dada yetu.

Ahsanteni!

Update
Hatimaye Dada yangu ameaga dunia mapema leo ijumaa tarehe 21/02/2020 . Binafsi sina la ziada zaidi ya kumshukuru mungu na nyote ambao mliguswa pale nilipowapatia taarifa za ugonjwa wake na hata kunitia moyo na kunishauri kwa namna ambavyo mliweza. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina lake libarikiwe!!
R.I.P dadaangu kipenzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom