Kuna mtu ameniomba ushauri anataka kurudia mtihani wa form six PCB mwakan 2020 amemaliza mwaka huu je nimshaulije? Naomba msaada wa mawazo alikuwa na 3.14
Anapoteza muda mkuu, usimshauri afanye hivyo .Lengo kuu la kusoma PCB ni aje kufanya MD,pharmacy kwa asilimia kubwa , hivi vitu vinahitaji ufaulu mkubwa sana ambao nina uhakika hawezi kuupata akirudia mtihani.
Mshauri afanye Ku rudia kwa mchepuo wa hge atafauru kama amepata 3.14 kwa PCB.
Kwa pcb simshauri...pcb si kitoto,nina rafikizangu walirudia karibu mara mbili (wote), na kila wakirudia maksi afadhari wasingerudia tuu
Kwanza kabisa ajaribu kuangalia alikua anatamani kusomea nini,kama udaktari asirudia ,simshauri sababu kurudia pepa ukapata B au C ya bio au chem sio mchezo,pia nikama anaweza Akatwanga maji kwenye kinu...harafu hapo Nabado aje kupambana na ushindani, (atapoteza sana Muda)
Ikiwezekana aende diploma au aangalie coz tofauti kwenye awamu hii inayofuata,mfano kwa udom,kuna coz nzuri sana college za informatics,atapata tuu
Kurudia sio inshu anatakiwa kujua anataka nn kama n MD au pharmacy kuna njia nyingi za kufikia huko si lazima arudie mtihani wa six. Njia ya elimu pana siku hzi
Afauate hii
Certificate~diploma~degree
Kuna mtu ameniomba ushauri anataka kurudia mtihani wa form six PCB mwakan 2020 amemaliza mwaka huu je nimshaulije? Naomba msaada wa mawazo alikuwa na 3.14
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.