Miaka mitatu iliyopita kuna mwanamke mmoja mfanya biashara, alifikia nyumbani kwetu akitokea kwenye biashara zake, alikuwa akifikia kwetu mara kwa mara kwani aliwahi kusoma chuo cha tiba na dadangu na walikuwa marafiki, ingawa dadangu huyo kwa muda mrefu sasa anaishi nje ya nchi lakini huyu rafiki yake ilikuwa ni mazowea yake kufikia kwetu toka enzi za chuo na mwenzake.
Kwa kifupi, mara ya mwisho kufikia kwetu aliacha suitcase yake na kusema anaenda Zanzibar atarudi baada ya siku 3. Kwa bahati nzuri au mbaya, huyu dada hajarudi mpaka leo, na wiki mbili zilizopita, tukaamuwa kulifunguwa lile suitcase lake, jamani, tulichokuta humo hakisemeki...
Euro 259,000 taslim, US dollars 56,000 taslim na unga-unga mweupe kilo mbili na nusu, ambao baadae tulijuwa kuwa ni cocaine, imewekwa kwenye vifuko vya plastic vya gram 500 vitano.
Huyu dada kwao ni Mwanza na katika kuulizia kwa dadangu ambae ni rafiki yake, akasema huyo dada kwao ni Mwanza na ana ndugu zake kule, wazee wake walishafariki zamani na alipofika chuo akaanza maisha ya mjini, masomo yakamshinda na hakurudi tena huko Mwanza.
Jamani, Kama kuna mtu anamjua huyu dada yuko wapi, ajitokeze, anaitwa Angelina, ukimuona ni mrefu, ana umbo kubwa la Kinyamwezi, lakini mwenyewe ni chotara wa aina fulani ana damu mchanganyiko na anapenda kutabasamu saa zote, si muongezi sana na hana marafiki niwajuao hapa Dar. Kama alikuwa nao, basi ni siri yake.
Kama kuna nduguye au amjuae yeye au ndugu zake, tuwasiliane. Mpaka sasa nimekopa dollar 6,000 tu katika hiyo suitcase, kumalizia vishida vya hapa na pale.
Kwa kifupi, mara ya mwisho kufikia kwetu aliacha suitcase yake na kusema anaenda Zanzibar atarudi baada ya siku 3. Kwa bahati nzuri au mbaya, huyu dada hajarudi mpaka leo, na wiki mbili zilizopita, tukaamuwa kulifunguwa lile suitcase lake, jamani, tulichokuta humo hakisemeki...
Euro 259,000 taslim, US dollars 56,000 taslim na unga-unga mweupe kilo mbili na nusu, ambao baadae tulijuwa kuwa ni cocaine, imewekwa kwenye vifuko vya plastic vya gram 500 vitano.
Huyu dada kwao ni Mwanza na katika kuulizia kwa dadangu ambae ni rafiki yake, akasema huyo dada kwao ni Mwanza na ana ndugu zake kule, wazee wake walishafariki zamani na alipofika chuo akaanza maisha ya mjini, masomo yakamshinda na hakurudi tena huko Mwanza.
Jamani, Kama kuna mtu anamjua huyu dada yuko wapi, ajitokeze, anaitwa Angelina, ukimuona ni mrefu, ana umbo kubwa la Kinyamwezi, lakini mwenyewe ni chotara wa aina fulani ana damu mchanganyiko na anapenda kutabasamu saa zote, si muongezi sana na hana marafiki niwajuao hapa Dar. Kama alikuwa nao, basi ni siri yake.
Kama kuna nduguye au amjuae yeye au ndugu zake, tuwasiliane. Mpaka sasa nimekopa dollar 6,000 tu katika hiyo suitcase, kumalizia vishida vya hapa na pale.