zumbemkuu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 10,831
- 8,621
Wana JF,
kwanza poleni kwa usumbufu mnaopata kutokana na ujumbe wa simu unaoendelea kusambazwa na hili GENGE LA MAHARAMIA WANAOONGOZWA NA TEJA LAO MIRAJI.
Dhumuni langu kubwa hapa nataka nielezee elimu inayoendelea kutolewa na msanii maarufu hapa nchini Mrisho Mpoto.
Kati ya matangazo yake mengi yanayosambazwa kwenye vituo mbalimbali vya TV, lililonigusa zaidi ni lenye ujumbe ufuatao; nanukuu; ..UKIONA UMEKULA UJUE UMELIWA.
Kutokana na ujumbe huo labda niwaambie marafiki zangu kina MALARIA SUGU, QUIENIN, MAGGID, KUDADEKI na wengineo wengi wanaoendelea kutetea utawala wa kifisadi kutokana labda kulipwa au kufaidika kwa namna moja au nyingine na mfumo wa serikali inayoondoka madarakani hivi karibuni kuwa, KAMA WAMEKULA BASI WAJUE WAMELIWA PIA hasa ukizingatia kauli za rais anayestaafu hivi karibuni kwenye moja ya hotuba zake alipowaambia wananchi kuwa, nanukuu; .UKITAKA KULA NA WEWE LAZIMA ULIWE KIDOGO
Historia itawahukumu hasa pale atakapoinuka mtawala mwingine ambae hamjui mtoto wa MAGGID, SHIMBO, TENDWA, MKUU WA REDET na wengine wenye kutaka kupora haki ya wanyonge kwa kutumia kalamu au vyeo na dhamana walizokabidhiwa.
Ninachowaambia ni kuwa UKIONA UMEKULA UJUE UMELIWA.
kwanza poleni kwa usumbufu mnaopata kutokana na ujumbe wa simu unaoendelea kusambazwa na hili GENGE LA MAHARAMIA WANAOONGOZWA NA TEJA LAO MIRAJI.
Dhumuni langu kubwa hapa nataka nielezee elimu inayoendelea kutolewa na msanii maarufu hapa nchini Mrisho Mpoto.
Kati ya matangazo yake mengi yanayosambazwa kwenye vituo mbalimbali vya TV, lililonigusa zaidi ni lenye ujumbe ufuatao; nanukuu; ..UKIONA UMEKULA UJUE UMELIWA.
Kutokana na ujumbe huo labda niwaambie marafiki zangu kina MALARIA SUGU, QUIENIN, MAGGID, KUDADEKI na wengineo wengi wanaoendelea kutetea utawala wa kifisadi kutokana labda kulipwa au kufaidika kwa namna moja au nyingine na mfumo wa serikali inayoondoka madarakani hivi karibuni kuwa, KAMA WAMEKULA BASI WAJUE WAMELIWA PIA hasa ukizingatia kauli za rais anayestaafu hivi karibuni kwenye moja ya hotuba zake alipowaambia wananchi kuwa, nanukuu; .UKITAKA KULA NA WEWE LAZIMA ULIWE KIDOGO
Historia itawahukumu hasa pale atakapoinuka mtawala mwingine ambae hamjui mtoto wa MAGGID, SHIMBO, TENDWA, MKUU WA REDET na wengine wenye kutaka kupora haki ya wanyonge kwa kutumia kalamu au vyeo na dhamana walizokabidhiwa.
Ninachowaambia ni kuwa UKIONA UMEKULA UJUE UMELIWA.