Mrisho Mpoto balozi rasmi wa Shirika la Posta Tanzania

PendoLyimo

JF-Expert Member
Sep 30, 2014
877
952
Mstanii wa Mashairi Mrisho Mpoto (Mjomba) amesaini Mkataba wa makubaliano ya pamoja na Shirika la Posta Tanzania kuwa Balozi wa Shirika hilo. Shirika la Posta Tanzania limeingia Makubaliano na Msanii huyo ili kulitangaza Shirika pamoja shughuli zote za Shirika hilo ikiwemo Huduma Pamoja, Duka Mtandao, EMS, Post Cargo, Pcum pamoja na Posta kiganjani Ndani na Nje ya Nchi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Postamasta Mkuu Bwa. Macrice Daniel Mbodo amesema kuwa Shirika la Posta kwasasa lipo kwenye mageuzi makubwa ya kiutendaji hivyo Shirika limeona vyema kushirikiana na Mrisho Mpoto kulitangaza Shirika hilo.

"Kwasasa Shirika la Posta lipo kwenye Mageuzi Makubwa ya Kiutendaji pamoja na Maboresho ya Huduma zetu, kama Shirika limemteuwa Bwa Mrisho Mpoto (Mjomba) kuwa Balozi wa Shirika la Posta ili kulitangaza Shirika pamoja na shughuli zote zinazofanywa na Shirika la Posta Tanzania " Macrice Mbodo

Kaimu Postamasta Mkuu aliendelea kwa kusema Wananchi wanafahumu Huduma moja tu inayotolewa na Shirika la hilo,
"Wananchi wanafahamu Huduma moja tu inayotolewa na Shirika la Posta, Huduma ya kutuma na kupokea barua lakini kwasasa kupitia Ofisi zetu za Shirika la Posta unaweza kupata Huduma ya NIDA, RITA, Pasi ya kusafiria pamoja Huduma za Kibenki, Imani yetu kama Shirika kupitia Mrisho Mpoto atazitangaza Huduma hizi kwa Wananchi " Macrice Mbodo

Aidha kwa upande wa Mrisho Mpoto amelishukuru Shirika la Posta Tanzania kwa kumuamini na kumtekuwa kuwa Balozi wa Shirika hilo.

"Nilishukuru sana Shirika la Posta Tanzania kwa kuniamini na kuniteuwa kuwa Balozi hii ni heshima kubwa kwangu nitakwenda kulitangaza Shirika pamoja na Shughuli zote za Shirika la Posta Tanzania kama Balozi wa Shirika hili" Mrisho Mpoto
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Shirika lenyewe liko wapi hapo?

Anaona kitu chenyewe kimekwiisha nayeye anakubali kutwishwa mzigo?
 
Hivi hawa wasani na huo ubaloz wa makampuni

Wanafanyajefanyaj kaz

Ova
 
Jamani tuachee tuache unafiki Posta ya Sasa na Ile zamani utofauti upo Mkubwa sana, huyu Mbodo PostaMasta mkuu anayekaimu Sasa hivi anaupiga mwingi sana
 
Jamani tuachee tuache unafiki Posta ya Sasa na Ile zamani utofauti upo Mkubwa sana, huyu Mbodo PostaMasta mkuu anayekaimu Sasa hivi anaupiga mwingi sana
Andika kwa kutulia basi, Posta imebadilika kwenye nyanja zipi bidada?
 
Shirika la Posta lina kila sababu ya kuwa moja ya makampuni yenye mafanikio kama rasilimali zake zitatumika kwa ufanisi. Nashauri wajikite kwenye usafirishaji wa makasha na mizigo.

Kwa mfano, Ndege ya mizigo inayotarajiwa ingekodishwa kwa shirika hili la Posta badala ya kuwa ATCL, au shirika la Posta liingie ubia na ATCL kwenye biashara ya CARGO.

Masanduku ya barua na vifurushi yanayokodishwa yaunganishwe kwenye huduma za SMS zitolewazo na mashirika ya simu ili barua inapowekwa kwenye boksi mteja apate taarifa ya SMS kama ilivyo kwenye utaratibu wa kibenki.
 
Tatizo la Tanzania ni maneno mengi na porojo kuliko vitendo! Huyo Mpoto ni mtu wa propaganda. Tunahitaji shirika litende zaidi, halihitaji mtu wa kulinadi kama litafanya kazi zake sawa sawa.
 
Back
Top Bottom