Mrisho Gambo: Wafanyabiashara wa maduka ya kubadili fedha za kigeni walioporwa fedha na mali zao warudishiwe

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,986
144,313
Na huyu ndio alikuwa RC wa Arusha wakati huo.

Wapinzani hawako Bungeni, sasa ni lazima wao waseme ukweli mchungu hata kama ukweli huo unawagusa.

Ipo siku watakiri kuwa hata huo ubunge wao ni haramu na wenye busara watakuja kuomba radhi umma wa watanzania.

In short, Magu atakumbukwa kwa uovu mwingi na ni busara WANA-CCM wenzake au wanafamilia wake wakamuombea msamaha kwa watanzania.
 
Wakati yeye ndo alikuwa anasimamia hilo zoezi kwa mbwembwe na kejeli.

Hakyamama mwendazake anachezea za uso mpaka namwonea huruma. Huyu Gambo hajui kawa mbunge kwa juhudi za udhalimu wa mwendazake?

Kitu kimoja kwa hakika, ikatokea mwendazake akafufuka, atadedi tena fasta kwa spidi ya Mombardier, sio kwa unafiki huu wallah.
 
Gambo akapimwe akili kwanza.

Hata ubunge wake kaupata kwa hisani ya Magufuli. Gambo ni miongoni mwa wanafiki wakubwa ambao hawatakiwi kabisa.

Ukimufurahia Gambo ipo siku atakugeuka na wewe. Yeye si mkweli bali ni mfuata maslahi na mjinga mkubwa.
 
Ni kweli pasi na shaka kwamba utawala wa Mwendazake ulikuwa na kasoro nyingi na zimeumiza wengi - Ndani ya CCM yenyewe na nje.

Huyu anayelialia hapa yeye ndiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa - atakuwa anajua namna zoezi hilo lilivyowaumiza watu wengi, kwenye nchi zenye utawala wa sheria kweli kweli huyu anatakiwa muda huu awe anavisaidia vyombo vya dola kuchunguza hili jambo.
 
Amesema ni ma task force, mtu sahihi wa kuulizwa ni Luoga, gavana wa benki kuu.
Wakati yeye ndo alikuwa anasimamia hilo zoezi kwa mbwembwe na kejeli...

Hakyamama mwendazake anachezea za uso mpaka namwonea huruma. Huyu Gambo hajui kawa mbunge kwa juhudi za udhalimu wa mwendazake?

Kitu kimoja kwa hakika, ikatokea mwendazake akafufuka, atadedi tena fasta kwa spidi ya bombardier... sio kwa unafiki huu wallah...
 
Kwasasa

cards zitaisha.. better to keep grading, weka Gold Cards, Platinum Cards, Silver na nyingine.. na Membership Fee iwe tofauti kbs.

Kinachoendelea TFF Hakina Tofauti na CCM.
 
Back
Top Bottom