Mrisho Gambo: Wafanyabiashara wa maduka ya kubadili fedha za kigeni walioporwa fedha na mali zao warudishiwe

Ni kweli ni rahisi kumuita mnafiki lakini kweli hoja anazojenga mjengoni zina mashiko sana na Watanzania wengi tunaziunga mkono kwani Watanzania wengi wamedhulumiwa sana na yule mwendazake na Serikali yake. Ukweli ni lazima ubaki ukweli. Je, atapewa onyo kwamba apunguze maneno makali mjengoni au atakuwa mbunge wa awamu moja? Tusubiri.
Hakika mkuu, huyu jamaa alijijengea taswira mbaya sana machoni pa wengi hasa akiwa RC Arusha. Tangu aingie mjengoni ni kama vile kabatizwa ubatizo wa maji mengi - anajenga hoja zenye mashiko sana. Hata kama atapigwa mawe na wengi kwamba alikuwa sehemu ya udhalimu wa awamu iliypopita lakini ukweli utabakia kuwa ukweli tu kwamba anajenga hoja vizuri. Wahenga walisema: "Ukweli utabakia kuwa ukweli hata kama ungetoka kinywani mwa shetani"!!!
 
Ni kweli ni rahisi kumuita mnafiki lakini kweli hoja anazojenga mjengoni zina mashiko sana na Watanzania wengi tunaziunga mkono kwani Watanzania wengi wamedhulumiwa sana na yule mwendazake na Serikali yake. Ukweli ni lazima ubaki ukweli. Je, atapewa onyo kwamba apunguze maneno makali mjengoni au atakuwa mbunge wa awamu moja? Tusubiri.
BAK umeongea jambo la msingi sana, Gambo alinikosha jinsi alivyotetea watumishi walioonewa kwenye zoezi la uhakiki, na sasa ananifurahisha jinsi anavyotetea walioonewa wengine.

Mimi nasema hivi badala ya kumkatisha tamaa tumwambie keep it up, wakati huohuo tuendelee kummonitor je yuko consistent au ni flipfloper.

Mimi siku hizi najudge kila kitu kwa context ya wakati huo, mtu akifanya zuri namuappreciate ila akizingua nampa za uso palepale
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾👍🏽 Naunga mkono hoja Mkuu. Badala ya kuwazodoa watu kama hawa ndani ya maccm wanaosema ukweli ambao maccm hawaupendi tuwape moyo na kuwaunga mkono ili waendelee kusimamia haki za Watanzania.
BAK umeongea jambo la msingi sana, Gambo alinikosha jinsi alivyotetea watumishi walioonewa kwenye zoezi la uhakiki, na sasa ananifurahisha jinsi anavyotetea walioonewa wengine.

Mimi nasema hivi badala ya kumkatisga tamaa tumwambie keep it up, wajati huohuo tuendelee kummonitor je yuko consistent au ni flipfloper.

Mimi siku hizi najudge kila kitu kwa context ya wakati huo, mtu akifanya zuri namuappreciate ila akizingua nampa za uso palepale
 
Gambo amefanya jambo la kijasiri sana. Tunampongeza kwa hatua hii ya kusimama hadharani kuhesabiwa upande wa kutetea haki.

Wale wanaomshambulia kwa kuwa sehemu ya watekelezaji wa uovu huo watambue yeye alikuwa anatekeleza maagizo ya bosi wake kama mtumishi mtiifu. Kwamba angejiuzuru...bado hatujafika huko...ajiuzuru afe njaa...hapana!

Pamoja na kuwa simpendi Gambo kutokana na matendo yake na kauli zake wakati alipokuwa mkuu wa mkoa,michango yake katika bunge inanishawishi kumuunga mkono. Anatimiza wajibu wake wa kibunge sawasawa.
 
Na huyu ndio alikuwa RC wa Arusha wakati huo.

Wapinzani hawako Bungeni, sasa ni lazima wao waseme ukweli mchungu hata kama ukweli huo unawagusa.

Ipo siku watakiri kuwa hata huo ubunge wao ni haramu na wenye busara watakuja kuomba radhi umma wa watanzania.

In short, Magu atakumbukwa kwa uovu mwingi na ni busara WANA-CCM wenzake au wanafamilia wake wakamuombea msamaha kwa watanzania.
Well Noted
 
Hivi hizo hela zote zilienda wapi kwenye mfuko gani!? Na Gambo unaposema warejeshewe ziko mahali unapafahamu.
Kwani enzi hiyo wewe si ulikuwepo mbona hukumwambia msimamizi wa uporaji azirudishe?? Haiingii akilini kwa haya yanayoendelea! Ina maana note mlikuwa mnaburuzwa na JPM hamkuyaona!!?
Ama kweli !!....
 
Saw

Huyu mnafiki katumwa na Ridhiwan.Yaan haoni kuwa anajimaliza kabisa kisiasa.Huyu jamaa alipokuwa mkuu wa mkoa wa Arusha ,mara kadhaa alikuwa anagombana na mkuu wa wilaya.Ni mpumbavu sana huyu dogo.
We ndio umeandika nini hapa?

Ridhiwan anazingua vipi hapa? Unaonekana unachuki kubwa kwa ridhiwan for nothing. Michango ya Gambo mjengoni imekuwa ya kizalendo sana siku za karibuni.

Gambo anatimiza wajibu wake wa kibunge kikamilifu. Sisi wanaCCM wapenda haki tunamuunga mkono. Hatutaki vitendo vya dhuluma kwa wananchi vifanywe na kiongozi yeyote wa serikali yetu.
 
Gambo akapimwe akili kwanza.

Hata ubunge wake kaupata kwa hisani ya Magufuli. Gambo ni miongoni mwa wanafiki wakubwa ambao hawatakiwi kabisa.

Ukimufurahia Gambo ipo siku atakugeuka na wewe. Yeye si mkweli bali ni mfuata maslahi na mjinga mkubwa.
Mwendazake alishasema Gambo ni mbea.,Akamvua uRC
 
Hivi hizo hela zote zilienda wapi kwenye mfuko gani!? Na Gambo unaposema warejeshewe ziko mahali unapafahamu.
Kwani enzi hiyo wewe si ulikuwepo mbona hukumwambia msimamizi wa uporaji azirudishe?? Haiingii akilini kwa haya yanayoendelea! Ina maana note mlikuwa mnaburuzwa na JPM hamkuyaona!!?
Ama kweli !!....
Waseme zilipo wasije kuchota zingine kwenye nfuko tofautu nakujifanya wana warudishia
 
Dodoma. Mbunge wa Arusha Mjini (CCM), Mrisho Gambo amesema shughuli ya kufunga maduka ya kubadilishia fedha za kigeni iliyofanyika nchini takribani miwili iliyopita, ilikuwa ni uporaji wa kuumiza watu.

Akizungumza jana Jumatatu Juni 14, 2021 bungeni mjini Dodoma katika mjadala wa bajeti kuu ya Serikali, Gambo amedai mchakato huo ulikuwa kama nia ya baadhi ya watumishi wa Serikali kutaka wafanye wao biashara hiyo.

Novemba 20, 2018 maduka zaidi ya 20 yalifungwa jijini Arusha baada ya ukaguzi uliofanywa na maofisa wa Serikali wakishirikiana na vyombo vingine vya dola.

Aprili, 2021 Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga alisema kati ya maduka ya kubadilishia fedha za kigeni 87 yaliyofanyiwa ukaguzi jijini Dar es Salaam, 82 yalikutwa na viashiria vya utakatishaji wa fedha.

Katika maelezo yake, Gambo ambaye amewahi kuwa mkuu wa Mkoa Arusha amedai Serikali ilikuwa ikipandisha viwango vya mitaji kwa lengo la kutaka wafanyabiashara washindwe lakini walipoendelea kufanya biashara zao waliona hakuna namna zaidi ya kuvamia.
"Mlichukua fedha zao, magari, viwanja vyao na mali nyingine watu wakabaki hawana kitu hivi lengo la Serikali ilikuwa nini," amesema Gambo.

Gambo amezungumzia pia sekta ya Utalii akisema imeachwa kabisa bila kuwekewa mkakati katika bajeti jambo ambalo ni hatari kwa uchumi wa nchi.

Amesema Wizara ya Maliasili na Utalii imeshindwa kubuni mbinu ya kuvutia ili kuongeza watalii badala yake imefikiria kuongeza tozo inayoweza kusababisha watalii kupungua nchini.

"Hii bajeti imeacha kabisa kutaja sekta ya utalii, wenzetu wanafikiria kuvutia watalii sisi tunawaza kuongeza tozo, mnawaza nini nyie," amehoji Gambo.

Ametolea mfano wa kupungua kwa watalii kwamba kumesababisha baadhi ya wawekezaji kupunguza gharama kwenye mahoteli yao kutoka Dola 200 za Marekani hadi Dola 100.
 
Gambo aache unafiki na kujipendekeza kwa serikali ya sasa. Kama anayosema ni kweli, mbona yeye ndiye alikuwa mstari wa mbele kutekeleza hayo maagizo. Huu ni umalaya wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom