Mrisho Gambo umehadaa wapiga kura. St. Jude ilivuka vikwazo ikiwa upande wa watesi wao

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,979
Wakati St. Judy inapitia matatizo juu ya madeni Hadi kufikia wanafunzi kugoma na wafanyakazi kurejeshwa nyumbani Mrisho Gambo hakusema lolote Wala akuwatetea kwa chochote. Leo hii baada ya hali kutulia anaibuka Bungeni nakuzungumza huku akijua kabisa muda wa machungu umepita na Sasa shule ile imesimama na inasonga mbele.

Tunaporuhusu Taifa liwe na watu wanoangalia zaidi familia zao nakuacha familia za wengine tunaharibu Taifa. Kama aliyoyasema bungeni yalitoka moyoni alipaswa kukemea wakati watoto wanataabika. Mgogoro umeanza akiwa mkuu wa Mkoa wa Arusha, hakuna siku alisimama kunyanyua mdomo kuwatetea, alisimama na watesi ili apate kuishi.

Tusiwe wepesi kusahau, tuwapinge watu wasio na misimamo. Tuwapinge watu walioamua kuishi kwakufundishwa Cha kusema, tuwapinge watu wanaogeuza matatizo yetu kuwa mtaji wa kisiasa. Tumkatae Mrisho Gambo tukimwelekeza kusimama nasisi kwenye shida na raha bila kujali atapoteza nini.
 
Kipindi akiwa Mkuu wa Mkoa asingeweza kutia neno kwenye lile sakata kwa sababu liliwahusu TRA angethubu kibarua kingeota mbawa
 
Namtetea Gambo
Huu mgogoro ulianza kipindi cha kampeni baada ya shule kugoma kutoa magari ya kubeba wana c cmkwenda kwenye kampeni. Baada tu ya uchaguzi wakaona joto ya jiwe.
Veeeery true.

Walikataa kutoa magari na wanafunzi.

Magofool akafunga akaunti zao bila kujali watoto watakaoteseka.
Unamteteaje mtu ambae alikuwa kimya kwa kuficha ukweli sababu ya kumuogopa mwendazake? anaousema pale bungeni sasa ni unafiki tu kama walivyo CCM wengine.
 
Siyo alitumbuliwa ukuu wa mkoa kabla ya lile sakata? But Kama ana nia asaidie hata sasa Mana bado kuna mahitaji mengi shule inataka toka serikali yeye akiwa kiunganishi muhimu kwa sasa.
 
Wakati St. Judy inapitia matatizo juu ya madeni Hadi kufikia wanafunzi kugoma na wafanyakazi kurejeshwa nyumbani Mrisho Gambo hakusema lolote Wala akuwatetea kwa chochote. Leo hii baada ya hali kutulia anaibuka Bungeni nakuzungumza huku akijua kabisa muda wa machungu umepita na Sasa shule ile imesimama na inasonga mbele.

Tunaporuhusu Taifa liwe na watu wanoangalia zaidi familia zao nakuacha familia za wengine tunaharibu Taifa. Kama aliyoyasema bungeni yalitoka moyoni alipaswa kukemea wakati watoto wanataabika. Mgogoro umeanza akiwa mkuu wa Mkoa wa Arusha, hakuna siku alisimama kunyanyua mdomo kuwatetea, alisimama na watesi ili apate kuishi.

Tusiwe wepesi kusahau, tuwapinge watu wasio na misimamo. Tuwapinge watu walioamua kuishi kwakufundishwa Cha kusema, tuwapinge watu wanaogeuza matatizo yetu kuwa mtaji wa kisiasa. Tumkatae Mrisho Gambo tukimwelekeza kusimama nasisi kwenye shida na raha bila kujali atapoteza Nini.
Gambo ni kielelezo cha unafiki wa UVCCM
 
Alifungua mdomo wake wakati hela zimeporwa?
Kuja kulisemea kipindi hiki ni mazungumzo baada ya habari.
Inawezekana alifanya jambo ila kwa utulivu na uangalifu wa hali ya juu kama anatembea kwenye eneo lenye maji na vipande vya chupa akiwa peku.
 
Sasa angesemaje mbele ya kayafa akiwa hai, kayafa hakutaka kusikia kabisa haya, by the way kayafa ana mkono asilimia nyingi ile ishu ilivyotokea , na maagizo yalikua yake kayafa, fikiria wewe ndio gambo, ungefanyaje?
Ningesimama upande wenye haki. Ndio maana siwezi kuwa mwana siasa kamwe.
 
Namtetea Gambo
Huu mgogoro ulianza kipindi cha kampeni baada ya shule kugoma kutoa magari ya kubeba wana c cmkwenda kwenye kampeni. Baada tu ya uchaguzi wakaona joto ya jiwe.
Sasa Gambo si ndo mwanasisiemu aliyekuwa anafanya hizo kampeni kama anavyosema mtoa mada kwamba huyo Gambo alikuwa upande wa hao watesi?
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom