G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Hapana, labda kama kuna lingine na siyo uongozi mahiri na uwajibikaji uliowafikisha hapo.
Kama Magufuli hakuona umuhimu wa kuwa na Magesa Mulongo ambaye kitabia na kiutendaji amefanana kabisa na hawa vijana wasio kabisa na maadili ya kiuongozi ni kwanini isiwe na hawa?
Mrisho Gambo na Paul Makonda ni mfano wa viongozi wabovu waliojaa umimi, kujiona kusiko na mashiko na kutumia ofisi za umma kiumungu mtu.
Hata kule Iringa DC Kasesera anawakimbiza kwa kuonyesha mfano mzuri pale panapohitaji ushirikiano.
Vijana hawa (ni wakubwa zangu kiumri) wamekalia tu fitina na majungu kwa kuwa tayari wanaujua udhaifu wa "mkubwa" kwa hiyo wao ndiyo kazi waliobaki nayo.
Cha ajabu vijana hawa wamekabidhiwa miji muhimu kiuchumi lakini naona wanafanya mambo ya hovyo na siasa za maji taka kwenye kila jambo! Wanachojua wao ni nguvu ya mapolisi waliyokabidhiwa! Heko Lema na Kubenea kwa kuwafunza vijana hawa wasio na maadili wala weledi wa kazi.
Hata ukiangalia jinsi walivyopata nafasi zao za Ukuu wa mkoa kwa Dar-Paul Makonda na kwa Arusha-Mrisho Gambo utajua ni watu wa aina gani.
Kama Magufuli hakuona umuhimu wa kuwa na Magesa Mulongo ambaye kitabia na kiutendaji amefanana kabisa na hawa vijana wasio kabisa na maadili ya kiuongozi ni kwanini isiwe na hawa?
Mrisho Gambo na Paul Makonda ni mfano wa viongozi wabovu waliojaa umimi, kujiona kusiko na mashiko na kutumia ofisi za umma kiumungu mtu.
Hata kule Iringa DC Kasesera anawakimbiza kwa kuonyesha mfano mzuri pale panapohitaji ushirikiano.
Vijana hawa (ni wakubwa zangu kiumri) wamekalia tu fitina na majungu kwa kuwa tayari wanaujua udhaifu wa "mkubwa" kwa hiyo wao ndiyo kazi waliobaki nayo.
Cha ajabu vijana hawa wamekabidhiwa miji muhimu kiuchumi lakini naona wanafanya mambo ya hovyo na siasa za maji taka kwenye kila jambo! Wanachojua wao ni nguvu ya mapolisi waliyokabidhiwa! Heko Lema na Kubenea kwa kuwafunza vijana hawa wasio na maadili wala weledi wa kazi.
Hata ukiangalia jinsi walivyopata nafasi zao za Ukuu wa mkoa kwa Dar-Paul Makonda na kwa Arusha-Mrisho Gambo utajua ni watu wa aina gani.