Mrisho Gambo na Amos Makala karibuni tena Dar es Salaam

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,865
Ni siku nyingi sana Makamarada wangu Mrisho Gambo na Amos Makala zimepita tokea mliache Jiji letu hili la Maraha na Karaha la Dar es Salaam ila nimefarijika mno kusikia kuwa mnakaribia ama kuja kufanya Ziara kwa pamoja au mmoja wenu akapendezewa kubaki nami hapa Mkoani Dar es Salaam.

Mrisho Gambo najua kama kawaida yetu zile pande za Mwenge na Sea View zitatukoma na kama kawaida yetu Amos Makala najua sasa angalau kila Weekend tutakuwa hatukosekani pale New Msasani Club Kwao FM Academia au Mango Garden Kinondoni kwao Twanga Pepeta.

Nawasubirini kwa hamu sana Makamarada wangu ila sijajua mnakuja lini Dar ili niwapokee tuanze kula Bata zetu zile za 2014 hadi 2015.

Karibuni sana Dar es Salaam Mrisho Gambo na Amos Makala nitawasubirini pale pale Kijiweni kwetu.
 
Back
Top Bottom