Mrisho Gambo: Kuna wizi mkubwa wa fedha za Serikali kwenye jiji la Arusha

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,668
15,066
Kwa mujibu wa mbunge wa jimbo la Arusha mjini bwana Mrisho Gambo, baadhi ya viongozi wa jiji wamechukua fedha za halmashauri na kuziweka katika akaunti zao binafsi, akidai kuna mmoja amewekewa Sh103 milioni, mwingine Sh65 milioni akisema wanaifanya halmashauri kama shamba la bibi.

“Halafu wanataka mbunge acheke cheke tu, sasa utakuwa mbunge wa aina gani? Sipiti njia hapa ndio nimefika na nitaangaika na hawa wapiti njia hadi nijue mwisho wao ni wapi? Amesema Gambo.

Haya hivyo, mkuu wa wilaya ya Arusha, Said Mtanda amesema amesikia kilio cha Gambo kuhusu baadhi ya watumishi wa jiji la Arusha kuwekewa fedha katika akaunti zao binafsi.

Mtanda amesema kwa mujibu wa taratibu mtumishi anaweza kuchukua masurufu na kufanya retirement kwa mwajiri wake, ingawa upo ukomo wa kiasi cha fedha kinachopaswa kuchukuliwa kisheria.

“Suala hili limeshachukuliwa hatua na ofisi ya katibu tawala mkoa, nimesoma nakala ya barua wiki moja iliyopita inayomtaka mkurugenzi wa Jiji na maofisa waliotajwa kutoa maelezo juu ya suala hilo. Ikithibitisha kama kuna matumizi mabaya ya fedha serikali itachukua hatua."

“Naamini mbunge pia anafahamu kuwa uchunguzi wa suala hili unaendelea. Tukiacha haya yanayosemwa bila kuyatolea ufafanuzi wananchi wataamini kuwa serikali yao haichukui hatua dhidi ya tuhuma za ubadhirifu, hivyo kuifanya serikali kuwa dhaifu mbele ya macho ya umma,” amesema Mtanda.
 
IMG-20220508-WA0009.jpg
 
Huu utaratibu kiserikal upo, ambapo watu huwekewa fedha Kwa matumiz Fulani halafu mtumishi husika Huwa anafanya utaratibu wa kuretire. Wataalamu wanaita imprest.
Wanawekewa kwa ajili ya shughuli zipi? Imprest gani ya mamilioni hayo kwa mtumishi?

Nazijua imprest ila kwa matumizi au manunuzi yapi hayo?

Na imprest ni wizi kwa sababu retirement yake huwa ni janja janja.
 
“Naamini mbunge pia anafahamu kuwa uchunguzi wa suala hili unaendelea"

Pumzika kwa amani JPM, enzi zako hakuna mtumishi angesema maneno hayo ya "mchakato" na "uchunguzi" na badala yake pesa zingemtokea mtu kwenye Tundu mojawapo la mwili!
 
Hawa wahuni hawaogopi kuiba mali ya umma, wanajiamini Sana.
 
Hakuna kitu kibaya kama lugha aliyoitoa waziri wa fedha watu wasiwe na wasiwasi waweke fedha zao benki serikali haitafuatilia...rushwa na ufisadi unarahisishwa kwa sababu wamiliki wa akaunti hawana woga kuwa wanaweza siku moja kuulizwa chanzo na uhalali wa fedha zao
 
Walichukua hatua gani

Au ndiyo wanaishi kulalamika tu

Maana nchi sahvi imekuwa ya malalamiko fc

Ova
 
Back
Top Bottom