Mrembo mjasiriamali bongo amshauri Rais Magufuli mambo makuu matatu

Mkuu Kiranga , hivi "with due respect" kiswahili chake ni nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui kama inatafsirika vizuri ukisema "kwa heshima zote". Maana hapo umetafsiri maneno, lakini si dhana.

Ukija kwenye kutafsiri dhana, kitu cha karibu ninachokijua ni "Ashakum si matusi".

Maana yake, unaeleza kwamba, sikusudii kutukana au kuvunja heshima, lakini ninayotaka kusema ni mambo ya lazima katika maisha kama ashakum.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishaona mtu anaanza "with due respect" ujue anataka kuvunja heshima huyo.

"With due respect" ni mazingaombwe ya kupuliza kabla ya kuuma katika lugha ya Kiingereza.

Sent using Jamii Forums mobile app
jipya ni kuwa yeye anajua jinsi ya kuwaleta wawekezaji ila serikali itengeneze mazingira tu yaani kama mpira anaomba serikali impe assist yeye apige goli.yaani kama serikali ingekuwa mfanya biashara ni kwamba unazalisha product ambayo mteja Wa kununua tayari yupo
 
jipya ni kuwa yeye anajua jinsi ya kuwaleta wawekezaji ila serikali itengeneze mazingira tu yaani kama mpira anaomba serikali impe assist yeye apige goli.yaani kama serikali ingekuwa mfanya biashara ni kwamba unazalisha product ambayo mteja Wa kununua tayari yupo
Hapo pia hakuna jipya, kwa maana ya kwamba si kweli kwamba serikali haijui watu kama yeye wapo. Labda yeye ndiye hajui kwamba kuna kitengo tayari cha kushughulika na watu kama yeye, hahitaji barua kwa rais.

Tulikaa kikao na rais Mkapa na Waziri wa Mambo ya Nje Kikwete wakati huo, na balozi wa Tanzania UN Dr. Mahiga siku hizo, mwaka 2004, rais Mkapa alikuja United Nations, tukakaa kikao Watanzania wengi tu hapo 42nd Street New York City kubadilishana mawazo. Joseph Sokoine alikuwapo, watu kutoka ubalozini walikuwapo, January Makamba alikuwapo, vijana wa Kitanzania wengi sana wa New York City na sehemu za karibu walikuwepo.

Maongezi yakaja kuhusu uwekezaji, tukaongea yote hayo, serikali ikasema inaanzisha kitengo maalum cha kuhamasisha uwekezaji, kitengo kikaanzishwa, na kipo, na watu wanafanya kazi kila siku.Na wengine nawajua, kama mtu anataka persoanl introduction anitafute.

Tatizo la serikali ya Tanzania si kuwa na taarifa hizi basic za nini kinatakiwa kifanyike.

Serikali ina taarifa kuliko hizi anazotoa huyu dada.

Tatizo la serikali ya Tanzania ni political will, organization and implementation.

Tulianza wazo la kuhamisha mji mkuu kutoka Dar kwenda Dodoma. Wenzetu wa Nigeria baadaye wakapata wazo kama hilo kuhamisha mji mkuu kutoka Lagos kwenda Abuja.

Watu wa Nigeria kusikia sisi tulikuwa na mpango huo tangu awali yao, wakaja kutafuta ujuzi kwetu.Tukawapa makabrasha ya habari zote.

Wakaenda, wakazifanyia kazi. Wenzetu waliokuja kuchukua makabrasha kwetu wamemaliza shughuli ya kuhamisha mji mkuu zamani sana, sisi bado mpaka leo tunasuasua.

Tatizo si kuwa na habari nini kifanyike, serikali ina studies, ina wajuzi, ina historia, ina habari nyingi sana.

Matatizo ni nia, kujipanga na utekelezaji.

Kuna rafiki yangu mmoja smart sana, jamaa kwao wana hela kasoma mpaka Harvard, halafu ni mtu poa sana anajua kuongea na watoto wa kitaa fresh. Kwa hiyo ana usomi ule wa darasani, halafu na wa kitaa.

Basi, kapata uzoefu sana sekta ya elimu, akawa kama activist wa kuchambua mambo ya elimu, akawa anaikosoa kosoa sana serikali kwenye NGOs huko.

Sasa Kikwete mtoto wa mjini akasema wewe unakosoa sana, nataka kuja kukuonesha ngoma ya ndani. Kikwete akamteua yule rafiki yangu awe mshauri maalum wa rais, apate access yote kuona "how the sausage is made" kutoka ndani.

Basi jamaa akafurahi sana, akajua sasa nimepata sikio la Bwana Mkubwa, nitashauri mambo mazuri yote, tutabadili mengi sana.

Basi akawa anashauri, anasema hapa tufanye hivi. Kikwete anasema "hilo, hilo mbona tunalijua tangu mwaka 1987 kulikuwa na tume imeundwa kulichunguza na ripoti tunayo, kaongee na fulani wizarani, tena atakupa data zaidi ya unazojua wewe".

Dah, jamaa anasema hapa tukate hivi, Kiwete anamwambia "hilo, hilo tunalifahamu na tushaunda ofisi ya kulishughulikia, usiliguse maana itakuwa unaiingilia hiyo ofisi, tunalijua".

Yani yule mchizi wangu kila akisema hivi akifikiri serikali haijui, anakuta watu washafanya studies miaka na miaka, wameandika ripoti, kimbembe utekelezaji.

Mwishowe akawa frustrated, akaondoka Tanzania, sasa hivi anaendesha foundation moja kubwa Marekani yenye bajeti ya kama dola bilioni kadhaa hivi, kasema mambo ya Tanzania magumu sana.

Sasa hapo huyo ni mtu aliyekuwa very smart, in both the Harvard way (he went to Harvard) and the street way.

Sasa ukijua habari kama hizi, halafu ukaangalia hiyo post aliyoandika huyo dada, ndiyo unaona kama nia ya huyo dada ni kujitangaza ajulikane na yeye yupo, na haya ni maoni yake, sawa, anatumia haki yake ya kikatiba kama Mtanzania.

Lakini, kama anataka kuishauri serikali, katika hayo maneno yake, hakuna kipya ambacho ataishauri serikali ambacho serikali haikijui.
 
Kiranga kuna mtu alitaka kuwekeza hapa Tanzania akazuiwa? huyo dada aje na hao wawekezaji tuone kama atazuiwa, diaspora mnaongea tu kulaumu serikali wakati hata mia ya uwekezaji hamna. mnataka serikali ndio iwape pesa za kuwekeza dah
 
Hii tayari ni step forward kwake. Sasa cha kufanya kwake ni kuchukua kadi ya CCM/UVCCM. Kama ana cheti cha darasani kitakachofuata hapo ni kuteuliwa DC wilaya flani!!! Yaani hapa kaji brand!!!
 
Kama
MREMBO mjasiriamali Bongo aitwaye Babra Kalugira ameibuka na kumshauri Rais Dk. John Pombe Magufuli 'JPM' mambo makubwa matatu.

Kalugira ni mjasiriamali lakini pia ni mfanyakazi kwenye taasisi binafsi nchini.
Msikilize mwenyewe.

"MHESHIMIWA rais, mawaziri, wabunge na Watanzania wenzangu, shikamoni. Mimi naitwa Barbra Kalugira, nina miaka 31. Kubwa lililonileta hapa ni kumshauri Rais na serikali yake. Nataka nitoe wazo ambalo ninaamini linaweza likasaidia kujenga uchumi wa Tanzania."

KUHUSU KOROSHO
"Naomba niongelee suala la Korosho. Korosho tumekuwa tukiiangalia kwa kuiuza tu, Korosho kama korosho. Lakini mimi ninaiangalia kwa jicho lingine. Kivipi? Korosho ukiangalia vizuri ina product (bidhaa) nyingi sana ambazo zinaweza kutoka.

"Kuna product inaitwa vegetable oil (mafuta ya mboga). Tukiiangalia kiafya, vegetable oil it is very good. Haina cholesterol.

"Korosho inatoa maziwa. Lakini pia Korosho ukiangalia vizuri, watu ambao wameshatumia ile peanut butter (siagi ya karanga), inatoa ile paste. Korosho inaweza ikatengenezewa cake. Mambo ya bakery (uokaji).

"At the same time, Korosho ukiitumia kama maziwa, ukiitumia kama vegetable oil, yale makapi yake yanatengenezwa chakula cha mifugo. Tukiachana na chakula, Korosho inaweza kutengeneza mafuta ya ngozi mazuri sana ambayo hayaathiri ngozi zetu sisi Waafrika.

"Lakini pia ukiifanya Korosho kama ya kutolea bidhaa nyingi, watu wengi watafaidika, watapata ajira. Hebu tuangalie, hapa pana viwanda saba. Lakini pia kwenye hivyo viwanda saba, kuna wakurugenzi na wasaidizi.

Kuna receptionist (mtu wa mapokezi), kuna wapishi, wahasibu, watu wa masoko. Kuna thinkers (wafikiriaji), jinsi gani product iwe, branding yake. Hawa wote watakuwa wamepata ajira.
"Lakini pia hizo bidhaa zote zikitengenezwa kwa ubora mzuri na branding ikawa nzuri tunaweza kushindana na watu wa nje kwa kupeleka bidhaa zetu.

"Kwa hiyo mheshimiwa rais, kwa kuangalia Korosho kwa upande wa bidhaa, kwanza exportation (usafirishaji bidhaa nje) kwenye nchi itaongeza thamani ya shilingi ya Tanzania. Lakini pia hawa watu wote ambao watakuwa wanafanya kazi kwenye hivi viwanda watakuwa wanatoa kodi.

"Jinsi gani ya kupata investors (wawekezaji) mimi najua. Mheshimiwa rais, najua wewe unaipenda sana Tanzania na unawapenda sana Waafrika ndiyo maana unakuwa mkali. Kwa hiyo napenda niishie hapa kwenye hii ishu ya Korosho na viwanda."

KUHUSU VIPAJI
"Kuwekeza katika vipaji, angalia matajiri wa dunia hii. Ni wale watu ambao wanatumia vipaji vyao. Mimi naamini tunaweza kuchezesha michezo. Tunaweza kutumia talents (vipaji) kuitajirisha Tanzania.
"Angalia ma-bodyguard (walinzi) wa wasanii, watu wanaofanya gym, wama miili mizuri ya mazoezi.

Mheshimiwa rais, mimi najua jinsi ya kuwaleta wawekezaji. WW ikaja hapa. Ukawaambia lengo letu ni kuweka ajira kwa vijana na kuwasaidia Watanzania kuwa na maisha mazuri bila kutegemea mikopo.

"Kwa makabila zaidi ya mia moja tuliyonayo Tanzania, vuta picha umeweka kabila moja watu kama hamsini kwenye stage (jukwaa) wanapiga ngoma kwa zile beats (midundo), unafikiri watalii wangapi wataongezeka hapa nchini?

"Tufanyeje kuhusu hili? Mheshimiwa rais tenga eneo kubwa sana. Kwa mfano, nje ya nchi, kuna sehemu inaitwa Las Vegas. Ni sehemu ya 'kula maisha.' Wewe tenga kijiji, hatutasema ni sehemu ya kula maisha, tenga kijiji ambacho kitakuwa Latest Beautiful Alena in Africa au in the world.

"Mheshimiwa rais, boxing around. Hebu mwangalie Mayweather (Floyd) anavyosumbua. Ni ngozi nyeusi. Maana yake sisi tumebarikiwa mheshimiwa rais. Swimming pool. Ukienda Zanzibar, Mwanza, kuna watoto wanapiga mbizi kupindukia. Hivi vipaji vyote tuviweke katika kutafuta pesa. Watu waje kuangalia pale, wanalipa pesa.

'Kwenye hicho kijiji kuwepo na sehemu za burudani, kama mashindano. Tuwape Watanzania vitu vya kufanya. Tanzania, Afrika zipewe hadhi yake. Wazungu wamechoka na tamaduni zao ndiyo maana wanatamani kwenda kuishi kwenye mwezi. Mheshimiwa rais, mimi naamini tukifanya hivi tutakuwa tumefika."

KUHUSU UTAMADUNI

"Kuhusu utamaduni mheshimiwa rais, ninayo ya kuongea. Nchi ambayo haina utamaduni inadharaulika. Na mtu yeyote ambaye hana utamaduni hahesabiwi kama mtu. Kwa kupitia tamaduni zetu, tunaweza kuajiri vijana wengi.

"Mfano, nizungumzie tiba asili ambayo pia ni sehemu ya utamaduni. Mheshimiwa rais, wewe unaweza kuwa na namna ya kutangaza dawa za asili. Tiba za asili zipo na zinafanya kazi sahihi. Zinaponya kweli. Mimi Babra nimekulia (dawa) Kanyigo, nikiumwa nimekulia Nkaka ambayo ni Alovera. Nimetwangiwa Mshana. Tulikuwa hatujui hospitali.

"Mimi nafanya kazi kwenye tiba za asili. Dawa zetu zilikuwa zinafanya kazi vizuri kabisa. Lakini wenzetu wajanja walipokuja wakaharibu. Sisi tulijua jinsi gani ya kusaidia tiba asili ifike mahali ambapo tulikuwa tunataka kufika. Tulikuwa tunataka tufike hatua badala ya kuletewa dawa za Nutrition Products supplements tufike levo ya kutengeneza supplements zetu na sisi tuwauzie wao.

"Mimi naamini unaipenda Tanzania. Lakini ukweli ni kwamba kuna watu wetu walikwama. Badala ya kusaidia Watanzania ambao wanajihusisha na tiba asili wasonge mbele, wao wakawa wanarudisha nyuma. Wanaweka vikwazo, wanasema msifanye chochote, mara wauza madawa ya kulevya.

"Nyie ni government (serikali), kwa nini msichunguze. Lakini pia ni waganga wangapi ambao wazazi wao walifariki dunia wamewaachia ile mitishamba? Sasa unapowasumbua au huwaelekezi, unawawekea masharti magumu lengo ni nini hasa?

"Mheshimiwa rais, naomba uwe rais wa kufufua vya kwako. Kwenye tiba asili zipo dawa za kutibu malaria ukapona kabisa. Zipo dawa za kutibu fangasi. Hata nguvu za kiume. Wachukuliwe Watanzania kumi, wapewe hizo dawa, muone kama hawatapona. Wakipona tisa maana yake hiyo dawa inafanya kazi.

"Una sera nzuri mheshimiwa rais. Lakini je, huko tunakokwenda wanaelewa? Ambacho tulitakiwa kufanya ni kuweka bajeti kuhakikisha miti ya tiba asili inalimwa kwa wingi. Tungekuwa hatuhitaji hizo dawa zao. Na ndiyo maana wanachukua magogo yetu kwa sababu wanajua kuna dawa. Tulipangiwa matangazo,eti tusiseme tunatibu, lakini kwenye dawa za Kizungu wao wanaandika zinatibu. Mheshimiwa rais, liangalie hili. Nashukuru sana."


Sent using Jamii Forums mobile app
Michele Obama Angalieni huo Nkomo akikukumbatianhazimamuzunguke
 
Hapo pia hakuna jipya, kwa maana ya kwamba si kweli kwamba serikali haijui watu kama yeye wapo. Labda yeye ndiye hajui kwamba kuna kitengo tayari cha kushughulika na watu kama yeye, hahitaji barua kwa rais.

Tulikaa kikao na rais Mkapa na Waziri wa Mambo ya Nje Kikwete wakati huo, na balozi wa Tanzania UN Dr. Mahiga siku hizo, mwaka 2004, rais Mkapa alikuja United Nations, tukakaa kikao Watanzania wengi tu hapo 42nd Street New York City kubadilishana mawazo. Joseph Sokoine alikuwapo, watu kutoka ubalozini walikuwapo, January Makamba alikuwapo, vijana wa Kitanzania wengi sana wa New York City na sehemu za karibu walikuwepo.

Maongezi yakaja kuhusu uwekezaji, tukaongea yote hayo, serikali ikasema inaanzisha kitengo maalum cha kuhamasisha uwekezaji, kitengo kikaanzishwa, na kipo, na watu wanafanya kazi kila siku.Na wengine nawajua, kama mtu anataka persoanl introduction anitafute.

Tatizo la serikali ya Tanzania si kuwa na taarifa hizi basic za nini kinatakiwa kifanyike.

Serikali ina taarifa kuliko hizi anazotoa huyu dada.

Tatizo la serikali ya Tanzania ni political will, organization and implementation.

Tulianza wazo la kuhamisha mji mkuu kutoka Dar kwenda Dodoma. Wenzetu wa Nigeria baadaye wakapata wazo kama hilo kuhamisha mji mkuu kutoka Lagos kwenda Abuja.

Watu wa Nigeria kusikia sisi tulikuwa na mpango huo tangu awali yao, wakaja kutafuta ujuzi kwetu.Tukawapa makabrasha ya habari zote.

Wakaenda, wakazifanyia kazi. Wenzetu waliokuja kuchukua makabrasha kwetu wamemaliza shughuli ya kuhamisha mji mkuu zamani sana, sisi bado mpaka leo tunasuasua.

Tatizo si kuwa na habari nini kifanyike, serikali ina studies, ina wajuzi, ina historia, ina habari nyingi sana.

Matatiizo ni nia, kujipanga nautekelezaji.

Kuna rafiki yangu mmoja smart sana, jamaa kwao wana hela kasoma mpaka Harvard, halafu ni mtu poa sana anajua kuongea na watoto wa kitaa fresh. Kwa hiyo ana usomi ule wa darasani, halafu na wa kitaa.

Basi, kapata uzoefu sana sekta ya elimu, akawa kama activist wa kuchambua mambo ya elimu, akawa anaikosoa kosoa sana serikali kwenye NGO's huko.

Sasa Kikwete mtoto wa mjini akasema wewe unakosoa sana, nataka kuja kukuonesha ngoma ya ndani. Kikwete akamteua yule rafiki yangu awe mshauri maalum wa rais, apate access yote kuona "how the sausage is made" kutoka ndani.

Basi jamaa akafurahi sana, akajua sasa nimepata sikio la Bwana Mkubwa, nitashauri mambo mazuri yote, tutabadili mengi sana.

Basi akawana anashauri, anasema hapa tufanye hivi. Kikwete anasema "hilo, hilo mbona tunalijua tangu mwaka 1987 kulikuwa na tume imeundwa kulichunguza na ripoti tunayo, kaongee na fulani wizarani, tena atakupa data zaidi ya unazojua wewe".

Dah, jamaa anasema hapa tukate hivi, Kkiwete anamwambia "hilo, hilo tunalifahamu na tushaunda ofisi ya kulishughulikia, usiliguse maana itakuwa unaiingilia hiyo ofisi, tunalijua".

Yani yule mchizi wangu kila akisema hivi akifikiri serikali haijui, anakuta watu washafanya studies miaka na miaka, wameandika ripoti, kimbembe utekelezaji.

Mwishowe akawa frustrated, akaondoka Tanzania, sasa hivi anaendesha foundation moja kubwa Marekani yenye bajeti ya kama dola bilioni kadhaa hivi, kasema mambo ya Tanzania magumu sana.

Sasa hapo huyo ni mtu aliyekuwa very smart, in both the Harvard way (he went to Harvard) and the street way.

Sasa ukijua habari kama hizi, halafu ukaangalia hiyo post aliyoandika huyo dada, ndiyo unaona kama nia ya huyo dada ni kujitangaza ajulikane na yeye yupo, na haya ni maoni ayke, sawa, anatumia haki yake ya kikatiba kama Mtanzania.

Lakini, kama anataka kuishauri serikali, katika hayo maneno yake, hakuna kipya ambacho ataishauri serikali ambacho serikali haikijui.

Habari ya huyo rafiki yako ina ufanano kiasi na habari ya yule mbunge wa Nzega, Hussein Bashe.

Alikuwa mkosoaji sana wa serikali ya Magufuli akiwa bungeni.

Sasa Magufuli kamteua kuwa naibu waziri wa kilimo sijui....eneo ambalo alikuwa akiikosoa sana serikali ya Magu.

Siku hizi simsikii kama ilivyokuwa zamani kabla ya kuteuliwa unaibu waziri.

Kukosoa kutoka mbali ni kazi rahisi sana kuliko kutenda ukiwa ndani!
 
Mtoto wa kitusi huyo check alivyopanda juu kwa urefu .Kapendeza mwenyewe.Haya karibuni jamani hiyo ndio sura yake hayo mengine aliyoandika Ni mazungumzo baafa ya habari
Hii inawezekana ndiyo nia ya habari nzima.

Otherwise kama ni kuwakilisha mawazo tu, hayo hayahitaji picha.

Siku hizi mbinu za kujitofautisha ni nyingi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari ya huyo rafiki yako ina ufanano kiasi na habari ya yule mbunge wa Nzega, Hussein Bashe.

Alikuwa mkosoaji sana wa serikali ya Magufuli akiwa bungeni.

Sasa Magufuli kamteua kuwa naibu waziri wa kilimo sijui....eneo ambalo alikuwa akiikosoa sana serikali ya Magu.

Siku hizi simsikii kama ilivyokuwa zamani kabla ya kuteuliwa unaibu waziri.

Kukosoa kutoka mbali ni kazi rahisi sana kuliko kutenda ukiwa ndani!
Bashe amefungwa speed governor na "collective responsibility". Kwa hivyo kumsikia hadharani anakosoa si rahisi.Kwa sababu yeye sasa ni junior cabinet minister, si backbencher.

Ila naona serikali imekubali haitaleta ujinga wa kuingilia biashara ya korosho tena baada ya fiasco.

So labda anawananga kwenye vikao vya ndani huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom