Mrema apinga serikali ya mseto Kigoma

Asha Abdala

JF-Expert Member
Mar 21, 2007
1,130
44
Mrema apinga serikali ya mseto Kigoma

na Jacob Ruvilo

MGOGORO wa serikali ya mseto katika Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma-Ujiji, mkoani Kigoma, umeingia katika sura mpya kutokana na Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema, kupinga Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukabidhi madaraka kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa madai kuwa wananchi wa manispaa hiyo hawakushirikishwa kutoa maoni kuhusu serikali hiyo.

Akihutubia mkutano wa hadhara mkoani hapa mwishoni mwa wiki, Mrema alisema kutokana na hali hiyo seriklali ya mseto katika manispaa hiyo si halali.

Alisema CCM ilikubali mfumo wa serikali ya mseto Kigoma kutokana na kuona kuwa watanufaika.

Aliongeza kuwa kama wangekuwa waungwana, suala la serikali ya mseto Zanzibar lisingesubiri maoni ya wananchi.

Mrema alisema kama suala la serikali ya mseto visiwani Zanzibar linasubiri maoni ya wananchi, basi suala al serikali ya mseto katika Halmashauri ya Manispaa ya Kigoima-Ujiji lingesubiri pia maoni ya wananchi.

Kutokana na utata huo, Mrema ametaka kuvujwa kwa serikali ya mseto katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji, ili kusubiri maoni ya wananchi au kuruhusu serikali ya mseto Zanzibar bila kungoja maoni ya wananchi kama ilivyoundwa serikali ya mseto Kigoma.

Mrema alimtahadharisha Rais Jakaya Kikwete na serikali yake kuwa makini na maamuzi ya ubabaishaji kwa sababu hali hiyo inaweza kusababisha vurugu kama zilizotolea nchini jirani ya Kenya.

Wananchi waliohudhuria mkutano huo, walionekana kuunga mkono kauli hiyo ya Mrema kwa kushangilia mara kwa mara.

Kwa kauli moja wananchi wa Manispaa ya Kigoma-Ujiji wameitaka Chadema kutoachia madaraka hadi maamuzi ya seikali ya mseto yatakapokuwa sawa katika pande zote mbili za Zanzibar na Kigoma
 
Hivi kwani CHADEMA na CCM kila mmoja ana madiwani wangapi Kigoma? Na lile sakata la madiwani wa CHADEMA kutekwa Kigoma na kupewa rushwa kwa kuletwa Dar es salaam na mawaziri limeishia wapi?

Asha
 
Maadamu umeuliza naamini hapa ni jungu kubwa .Majibu yatamwagwa.Lakini mbona kuna kuwa na mabavu sana katika maamuzi ?
 
Hivi kwani CHADEMA na CCM kila mmoja ana madiwani wangapi Kigoma? Na lile sakata la madiwani wa CHADEMA kutekwa Kigoma na kupewa rushwa kwa kuletwa Dar es salaam na mawaziri limeishia wapi?

Asha

Dada Asha imebidi nicheke sana hapa, nishapata mradi mpya, nitakuwa navikusanya hivi vibweka vya ajabu ajabu vya Tanzania ambavyo sie tushavizoea, na kuviuza kwenye vijarida huko, Readers Digest sijui na nini nini, mara Madiwani wametekwa nyara, mara mtu kakutwa na kichwa cha dada yake, these stories are despicable but hey, If the deed is done I might as well find a way to make a few bucks on it.
 
Dada Asha imebidi nicheke sana hapa, nishapata mradi mpya, nitakuwa navikusanya hivi vibweka vya ajabu ajabu vya Tanzania ambavyo sie tushavizoea, na kuviuza kwenye vijarida huko, Readers Digest sijui na nini nini, mara Madiwani wametekwa nyara, mara mtu kakutwa na kichwa cha dada yake, these stories are despicable but hey, If the deed is done I might as well find a way to make a few bucks on it.

They are done indeed, one of the Diwani was caught ready pants at VIP place in Dar es salam International Airport as he/she was being ferried from Kigoma to Dar es salaam by one FISADI Minister. This was written in Tanzanian papers, but I am told there are more. Can some one volunteer to release the details please?

Asha
 
They are done indeed, one of the Diwani was caught ready pants at VIP place in Dar es salam International Airport as he/she was being ferried from Kigoma to Dar es salaam by one FISADI Minister. This was written in Tanzanian papers, but I am told there are more. Can some one volunteer to release the details please?

Asha

Huyo diwani alisafirishwa kwa maswala binafsi/kichama au kiserikali?
 
Huyo diwani alisafirishwa kwa maswala binafsi/kichama au kiserikali?

Iliandikwa magazetini, si ya chama wala si ya kiserikali wala si ya binafsi. Alibebwa na waziri na kuhongwa hela ili asiwepo Kigoma siku ya kupiga kura CCM iwe na simple majority ishinde. Akakamatwa na CHADEMA na kurudishwa Kigoma na kupiga kura. Hivi kwani wabunge wa mkoa hawaruhusiwi kuingia kwenye halmashauri? Kwanini CHADEMA isipeleke wabunge wake wa Kigoma kuongeza idadi wawe na majority?

Asha
 
Msimshangae Mrema kwa hilo, kwani yeye anashangaa ni vipi CCM wakubali mseto hapa kigoma,vipi pale Tarime napo kutakuwepo na mseto? maana twajua nako CHADEMA ndiyo inaingoza hamalshauri ile.
 
Labda kwa kuanza kule Kigoma sio serikali ya mseto moja kwa moja ... walikubaliana (chini ya usimamizi wa Mhe. Pinda) kwamba wagawane zamu ya uenyekiti wa halmashauri ya mji wa Kigoma/Ujiji. Nusu ya kwanza mwenyekiti awe wa Chadema na makamu wake awe wa Sisiem, then nusu ya pili wabalidishane bila uchaguzi. Ni vema Chadema (naamini ni waungwana wa kutosha) wakubali kwa roho safi kubadilshana majukumu ili mambo yaende sawa.
Halmashauri ya miji wa Kigoma/Ujiji ina mdiwani 10 wa Sisiem na 10 wa Chadema. Napenda kumpongeza Mhe. Pinda (wakati huo akiwa Waziri TAMISEMI) kwa busara alioyotumia kutatua mgogoro wa uchaguzi wa mwenyekiti halmashauri ile.
Hali ya Kigoma/Ujiji ni tofauti kabisa na Znzb
 
Roya Roy
Nakuuliza vipi katiba yetu inasema nini kuhusu hili, haya siyo maelewano yao wanasiasa wetu?
 
Wakuu heshima mbele
Ni masiku mengi tuu,tumekuwa tunataka uhuru na mademokrasia za kweli.CCM wamekuja na kuwapa wazanzibar demokrasia za kupiga kura kwa mafaida yao waweze kujichagulia kile wapendacho,cha ajabu waaanza kulalamika.Lamda walimtaka CCM awe dikiteta,asiwape hata hako ka uhuru?
Pigeni kura mjichagulie mpendacho,CUF wakishindwa ni maana ya kwamba huo mseto bado nyakati zake.
 
Iliandikwa magazetini, si ya chama wala si ya kiserikali wala si ya binafsi. Alibebwa na waziri na kuhongwa hela ili asiwepo Kigoma siku ya kupiga kura CCM iwe na simple majority ishinde. Akakamatwa na CHADEMA na kurudishwa Kigoma na kupiga kura. Hivi kwani wabunge wa mkoa hawaruhusiwi kuingia kwenye halmashauri? Kwanini CHADEMA isipeleke wabunge wake wa Kigoma kuongeza idadi wawe na majority?

Asha
kumbe hii michezo imeanza zamani sana
 
Back
Top Bottom