Mrema amvua madaraka mwenyekiti wa Kijiji!

AMARIDONG

JF-Expert Member
Jun 24, 2010
2,502
177
MWENYEKITI wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema (TLP), amemvua madaraka Mwenyekiti wa Kijiji cha Kyala, Kata ya Marangu Magharibi, Agustino Fabiani kwa madai ya unywaji wa pombe haramu ya gongo.

Mrema ametoa uamuzi huo wakati wakiwa katika operesheni maalumu ya Ulinzi Shirikishi kwa lengo la kukabiliana na uhalifu na ujambazi katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.

Mwanasiasa huyo ni Mbunge wa jimbo hilo. Katika operesheni hiyo ambayo ilifanywa kwa ushirikiano na Polisi, timu hiyo ya viongozi ilipita katika baadhi ya vijiji katika jimbo hilo na inadaiwa ilimkuta Mwenyekiti huyo wa Kijiji akiwa amelewa.

Mrema alidai kuwa, pamoja na kwamba Mwenyekiti huyo alikuwa mwanachama wa TLP, lakini yeye hawezi kulea viongozi aliodai hawana maadili kwa kuwa watazorotesha maendeleo ya wananchi.

Mbunge huyo alidai kuwa, taarifa za wanakijiji alizonazo zilieleza kuwa Mwenyekiti huyo alikuwa akisikika akiwahamasisha wananchi wanywe pombe hiyo kwa kuwa haina madhara kwa madai ni sawa na bia zilizopimwa kitaalamu.

“Mimi ni Mbunge wa wananchi wote wakiwemo wasio na vyama..nikimtetea huyu Mwenyekiti, wananchi hawatapata maendeleo, nimemvua madaraka yake ili iwe mfano kwa viongozi wengine wasio na maadili,” alisema.

Wakati wa operesheni hiyo ilibainika kwamba Kijiji cha Nganjoni ni kitovu cha utengenezaji wa pombe hiyo baada ya kukutwa kwa mitambo ya utengenezaji pombe hiyo huku wananchi wa eneo hilo wakihama makazi yao kwa hofu ya kutiwa mbaroni.

Mrema alisema, Jimbo la Vunjo limeathiriwa na vitendo vya uhalifu kutokana na kukithiri kwa uzalishaji wa pombe hiyo pamoja na unywaji wake na uvutaji wa bangi, hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa huku baadhi ya ndoa zikivunjika na wazazi kuacha kupeleka watoto shule.
 
Hahaha, kweli kazi tunayo, hiyo heading na maelezo yaliyo ndani du....Tunamshukuru Mh. hebu na wengine waige, kuna maovu mengi yanayofumbiwa macho.
MWENYEKITI wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema (TLP), amemvua madaraka Mwenyekiti wa Kijiji cha Kyala, Kata ya Marangu Magharibi, Agustino Fabiani kwa madai ya unywaji wa pombe haramu ya gongo.

Mrema ametoa uamuzi huo wakati wakiwa katika operesheni maalumu ya Ulinzi Shirikishi kwa lengo la kukabiliana na uhalifu na ujambazi katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.

Mwanasiasa huyo ni Mbunge wa jimbo hilo. Katika operesheni hiyo ambayo ilifanywa kwa ushirikiano na Polisi, timu hiyo ya viongozi ilipita katika baadhi ya vijiji katika jimbo hilo na inadaiwa ilimkuta Mwenyekiti huyo wa Kijiji akiwa amelewa.

Mrema alidai kuwa, pamoja na kwamba Mwenyekiti huyo alikuwa mwanachama wa TLP, lakini yeye hawezi kulea viongozi aliodai hawana maadili kwa kuwa watazorotesha maendeleo ya wananchi.

Mbunge huyo alidai kuwa, taarifa za wanakijiji alizonazo zilieleza kuwa Mwenyekiti huyo alikuwa akisikika akiwahamasisha wananchi wanywe pombe hiyo kwa kuwa haina madhara kwa madai ni sawa na bia zilizopimwa kitaalamu.

"Mimi ni Mbunge wa wananchi wote wakiwemo wasio na vyama..nikimtetea huyu Mwenyekiti, wananchi hawatapata maendeleo, nimemvua madaraka yake ili iwe mfano kwa viongozi wengine wasio na maadili," alisema.

Wakati wa operesheni hiyo ilibainika kwamba Kijiji cha Nganjoni ni kitovu cha utengenezaji wa pombe hiyo baada ya kukutwa kwa mitambo ya utengenezaji pombe hiyo huku wananchi wa eneo hilo wakihama makazi yao kwa hofu ya kutiwa mbaroni.

Mrema alisema, Jimbo la Vunjo limeathiriwa na vitendo vya uhalifu kutokana na kukithiri kwa uzalishaji wa pombe hiyo pamoja na unywaji wake na uvutaji wa bangi, hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa huku baadhi ya ndoa zikivunjika na wazazi kuacha kupeleka watoto shule.
 
Du kweli tlp hali mbaya lakini nahisi hata mrema anakunywa gongo sura yake now days mmh,nadhani hata hivyo viwanda vya gongo ni vyake polisi waangalie vizuri
 
mwenyekiti wa chama cha tanzania labour (tlp), agustine mrema (tlp), amemvua madaraka mwenyekiti wa kijiji cha kyala, kata ya marangu magharibi, agustino fabiani kwa madai ya unywaji wa pombe haramu ya gongo.

Mrema ametoa uamuzi huo wakati wakiwa katika operesheni maalumu ya ulinzi shirikishi kwa lengo la kukabiliana na uhalifu na ujambazi katika jimbo la vunjo mkoani kilimanjaro.

Mwanasiasa huyo ni mbunge wa jimbo hilo. Katika operesheni hiyo ambayo ilifanywa kwa ushirikiano na polisi, timu hiyo ya viongozi ilipita katika baadhi ya vijiji katika jimbo hilo na inadaiwa ilimkuta mwenyekiti huyo wa kijiji akiwa amelewa.

Mrema alidai kuwa, pamoja na kwamba mwenyekiti huyo alikuwa mwanachama wa tlp, lakini yeye hawezi kulea viongozi aliodai hawana maadili kwa kuwa watazorotesha maendeleo ya wananchi.

Mbunge huyo alidai kuwa, taarifa za wanakijiji alizonazo zilieleza kuwa mwenyekiti huyo alikuwa akisikika akiwahamasisha wananchi wanywe pombe hiyo kwa kuwa haina madhara kwa madai ni sawa na bia zilizopimwa kitaalamu.

"mimi ni mbunge wa wananchi wote wakiwemo wasio na vyama..nikimtetea huyu mwenyekiti, wananchi hawatapata maendeleo, nimemvua madaraka yake ili iwe mfano kwa viongozi wengine wasio na maadili," alisema.

Wakati wa operesheni hiyo ilibainika kwamba kijiji cha nganjoni ni kitovu cha utengenezaji wa pombe hiyo baada ya kukutwa kwa mitambo ya utengenezaji pombe hiyo huku wananchi wa eneo hilo wakihama makazi yao kwa hofu ya kutiwa mbaroni.

Mrema alisema, jimbo la vunjo limeathiriwa na vitendo vya uhalifu kutokana na kukithiri kwa uzalishaji wa pombe hiyo pamoja na unywaji wake na uvutaji wa bangi, hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa huku baadhi ya ndoa zikivunjika na wazazi kuacha kupeleka watoto shule.




naomba maelezo ya ziada kuhusu swala hili, maana kisheria ni wananchi waliomchaguwa ndio wana uwezo wa kumuondoa madarakani mwenyekiti wao. Au ni mwenyekiti wa chama chao hapo kijijini? Na kama ni wa chama basi hiko chama hakina vikao? Yaani maamuzi yanafanyikia vichochoroni? Kazi kweli kweli.
 
naomba maelezo ya ziada kuhusu swala hili, maana kisheria ni wananchi waliomchaguwa ndio wana uwezo wa kumuondoa madarakani mwenyekiti wao. Au ni mwenyekiti wa chama chao hapo kijijini? Na kama ni wa chama basi hiko chama hakina vikao? Yaani maamuzi yanafanyikia vichochoroni? Kazi kweli kweli.

nani kakuambia kyala kuna uchaguzi????
 
MWENYEKITI wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema (TLP), amemvua madaraka Mwenyekiti wa Kijiji cha Kyala, Kata ya Marangu Magharibi, Agustino Fabiani kwa madai ya unywaji wa pombe haramu ya gongo.

Mrema ametoa uamuzi huo wakati wakiwa katika operesheni maalumu ya Ulinzi Shirikishi kwa lengo la kukabiliana na uhalifu na ujambazi katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.

Mwanasiasa huyo ni Mbunge wa jimbo hilo. Katika operesheni hiyo ambayo ilifanywa kwa ushirikiano na Polisi, timu hiyo ya viongozi ilipita katika baadhi ya vijiji katika jimbo hilo na inadaiwa ilimkuta Mwenyekiti huyo wa Kijiji akiwa amelewa.

Mrema alidai kuwa, pamoja na kwamba Mwenyekiti huyo alikuwa mwanachama wa TLP, lakini yeye hawezi kulea viongozi aliodai hawana maadili kwa kuwa watazorotesha maendeleo ya wananchi.

Mbunge huyo alidai kuwa, taarifa za wanakijiji alizonazo zilieleza kuwa Mwenyekiti huyo alikuwa akisikika akiwahamasisha wananchi wanywe pombe hiyo kwa kuwa haina madhara kwa madai ni sawa na bia zilizopimwa kitaalamu.

“Mimi ni Mbunge wa wananchi wote wakiwemo wasio na vyama..nikimtetea huyu Mwenyekiti, wananchi hawatapata maendeleo, nimemvua madaraka yake ili iwe mfano kwa viongozi wengine wasio na maadili,” alisema.

Wakati wa operesheni hiyo ilibainika kwamba Kijiji cha Nganjoni ni kitovu cha utengenezaji wa pombe hiyo baada ya kukutwa kwa mitambo ya utengenezaji pombe hiyo huku wananchi wa eneo hilo wakihama makazi yao kwa hofu ya kutiwa mbaroni.

Mrema alisema, Jimbo la Vunjo limeathiriwa na vitendo vya uhalifu kutokana na kukithiri kwa uzalishaji wa pombe hiyo pamoja na unywaji wake na uvutaji wa bangi, hivyo kupoteza nguvu kazi ya taifa huku baadhi ya ndoa zikivunjika na wazazi kuacha kupeleka watoto shule.

mbona yeye mwenyewe mzee wa kiraracha amebabuka kwa sababu ya kunywa gongo?
 
Du kweli tlp hali mbaya lakini nahisi hata mrema anakunywa gongo sura yake now days mmh,nadhani hata hivyo viwanda vya gongo ni vyake polisi waangalie vizuri


Kaka Mrema ana KISUKARI ndg yangu, ni ugonjwa mbaya sana huu ndg yangu......
 
Naona mrema kaamua kukumushia enzi zake za wizara ya mambo ya ndani!
 
Kijiji cha Nganjoni ni
kitovu cha utengenezaji
wa pombe hiyo.

Hiyo ni kweli.Tulikuwa na shamba pale Masaera na hapo Nganjoni si mbali.
 
Du kweli tlp hali mbaya lakini nahisi hata mrema anakunywa gongo sura yake now days mmh,nadhani hata hivyo viwanda vya gongo ni vyake polisi waangalie vizuri

Hapo kwenye nyekundu ndugu yangu chunga sana! Lugha za wenyewe sisi tunajihamba tu!! Tuwaachie wenyewe kama hatuwezi!!
 
Hapo kwenye nyekundu ndugu yangu chunga sana! Lugha za wenyewe sisi tunajihamba tu!! Tuwaachie wenyewe kama hatuwezi!!

Labda kapitiwa tu si unajua hata unapoandiki kiswagili mtu waweza pitiwa kwa bahati mbaya.
 
hapo nganjoni kuliharibu waseminari wengi sana wakati wangu 1982-1985 wa st james kuna hicho kinywaji kwa maarfu kinajulikana kama chasoo, inueni mioyo, pandisha bega, chang;aa, piwa, nk

mrema amejaribu wengine tumuige, james mbatia yeye alipokuwa anagombea ubunge alienda eneo hili akaenda kuwapa hawa vijana wa nganjoni gongo
 
hapo nganjoni kuliharibu waseminari wengi sana wakati wangu 1982-1985 wa st james kuna hicho kinywaji kwa maarfu kinajulikana kama chasoo, inueni mioyo, pandisha bega, chang;aa, piwa, nk

mrema amejaribu wengine tumuige, james mbatia yeye alipokuwa anagombea ubunge alienda eneo hili akaenda kuwapa hawa vijana wa nganjoni gongo

Chasoo!!!!

Mkuu wakati wenu kulikuwa na venture? Majuu,mbunene,chuma,uarabuni,chimbo,dark room,box room nk?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom