MREJESHO: Wana Jf mlioko Dar nipokeeni nakuja huko kwa matibabu

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,780
14,098
nimatumaini yangu kuwa hamjambo wapendwa katika bwana, bila kupoteza muda naomba niende kwenye hoja yangu

Kama nilivoleta Uzi wangu wa kuwataka wana jf wanisaidie kwa mambo matatu ambayo niliyataja katika Uzi huu>>>>> Wanafamilia wa JF mliopo Dar nipokeeni nakuja huko kwa matibabu<<<< ambapo katika uzi huo nilipata makundi matatu ya watu

Kundi la kwanza ni wale waliojitokeza kunisaidia bila masharti kwani waliguswa na tatizo langu , mungu wabariki sana

Lakini pia kuna kundi jingine nalo lilikuwa tayari kwani nao pia waliguswa na tatizo langu, ila walinipa masharti ya kubadili avatar yangu ndo wanisaidie,nawaombea kwa mungu awabarki kwa moyo wao wa upendo

Kundi la tatu ni wale waliojaa kejeli na dhihaka kisa tu hawajawahi kukutana na changamoto za ugonjwa , lakini pia naamini mungu wa rehema atawasamehe na kuwabariki pia

Mwisho nilifika hapo Muhimbili na kupimwa vipimo viwili vya moyo yaani ECG NA ECHO, Bahati nzuri kipimo cha ECHO, Hakikuonesha tatizo ila ECG ilionesha kuwa nina myocardia infarction(acute) au wanaita shambulio la moyo, ambalo lilipelekea baadhi ya sehemu ya moyo kutopata damu vizuri , kutokana na kuziba kwa mirija{baadhi}, hivo niliandikiwa Dawa aina ya Asparem 75 , ndo natumia kwa sasa

kwa kuhitimisha napenda kuwashukuru madaktari kwa kunusuru uhai wangu, pia wanafamilia ya jf kwa ushauri mzuri, naomba tuzidi kupendana,tofauti za kiitikadi za chama zisitutenge, naomba mniombee nipate ahueni mapema kwa mapenzi ya mungu baba, pia nakaribisha ushauri wa kitabibu ili nipate nafuu mapema na tatizo lisijirudie tena, ikiwezekana hata nielekezwe dawa za kuzibua mirija ya moyo iliyoziba.


Ahsanteni, mungu awabariki

Picha ya kipimo cha ECG>>>>
cd861a15142ddeea4f89bc5d72c0e8db.jpg
<<<<<<
 
Duh, Ati ubadilishe Avatar ndo msaada utoke????


Pole kwa hilo kiongozi wangu kabla ya pole ya ugonjwa.

Jamani napenda nitoe angalizo tuchukiane na kudharauliana katika post za kisiasa tu. Tuendapo kwengineko maisha yaendelee kama Watanzania tulivyo katika mila, desturi na tamaduni zetu.


Pole sana kiongozi wangu
 
nimatumaini yangu kuwa hamjambo wapendwa katika bwana, bila kupoteza muda naomba niende kwenye hoja yangu

Kama nilivoleta Uzi wangu wa kuwataka wana jf wanisaidie kwa mambo matatu ambayo niliyataja katika Uzi huu>>>>> Wanafamilia wa JF mliopo Dar nipokeeni nakuja huko kwa matibabu<<<< ambapo katika uzi huo nilipata makundi matatu ya watu

Kundi la kwanza ni wale waliojitokeza kunisaidia bila masharti kwani waliguswa na tatizo langu , mungu wabariki sana

Lakini pia kuna kundi jingine nalo lilikuwa tayari kwani nao pia waliguswa na tatizo langu, ila walinipa masharti ya kubadili avatar yangu ndo wanisaidie,nawaombea kwa mungu awabarki kwa moyo wao wa upendo

Kundi la tatu ni wale waliojaa kejeli na dhihaka kisa tu hawajawahi kukutana na changamoto za ugonjwa , lakini pia naamini mungu wa rehema atawasamehe na kuwabariki pia

Mwisho nilifika hapo Muhimbili na kupimwa vipimo viwili vya moyo yaani ECG NA ECHO, Bahati nzuri kipimo cha ECHO, Hakikuonesha tatizo ila ECG ilionesha kuwa nina myocardia infarction(acute) au wanaita shambulio la moyo, ambalo lilipelekea baadhi ya sehemu ya moyo kutopata damu vizuri , kutokana na kuziba kwa mirija{baadhi}, hivo niliandikiwa Dawa aina ya Asparem 75 , ndo natumia kwa sasa

kwa kuhitimisha napenda kuwashukuru madaktari kwa kunusuru uhai wangu, pia wanafamilia ya jf kwa ushauri mzuri, naomba tuzidi kupendana,tofauti za kiitikadi za chama zisitutenge, naomba mniombee nipate ahueni mapema kwa mapenzi ya mungu baba, pia nakaribisha ushauri wa kitabibu ili nipate nafuu mapema na tatizo lisijirudie tena, ikiwezekana hata nielekezwe dawa za kuzibua mirija ya moyo iliyoziba.


Ahsanteni, mungu awabariki

Picha ya kipimo cha ECG>>>>
cd861a15142ddeea4f89bc5d72c0e8db.jpg
<<<<<<
Mganga wa wanga na Muumbaji awe nawe na uwe na moyo Mkuu utapona ndgu yangu!
 
Duh, Ati ubadilishe Avatar ndo msaada utoke????


Pole kwa hilo kiongozi wangu kabla ya pole ya ugonjwa.

Jamani napenda nitoe angalizo tuchukiane na kudharauliana katika post za kisiasa tu. Tuendapo kwengineko maisha yaendelee kama Watanzania tulivyo katika mila, desturi na tamaduni zetu.


Pole sana kiongozi wangu
Ahsante sana mpendwa
 
Duh, Ati ubadilishe Avatar ndo msaada utoke????


Pole kwa hilo kiongozi wangu kabla ya pole ya ugonjwa.

Jamani napenda nitoe angalizo tuchukiane na kudharauliana katika post za kisiasa tu. Tuendapo kwengineko maisha yaendelee kama Watanzania tulivyo katika mila, desturi na tamaduni zetu.


Pole sana kiongozi wangu
Nasisitiza abadilishe tuu hata kwa sasa ,hii nchi imeshabadilika si kama zama Za kale watu wamenuna kupita kiasi mm nilitaka kutolewa nyongo siku moja daaah so sad
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom