Mrejesho wa mwezi mmoja baada ya kuacha kazi

Kuacha kazi ili ujiajili unahitaji uwe na akili maalumu, watu wana Mahindi yanaozea ndani hayana soko, nimeshuhudia Songea mwaka Jana mamia ya heka za mbaazi Wakulima wamegoma kuvuna, sababu gharama za kuvuna ni kubwa kuliko bei ya mbaazi.

Kuna Dada yangu aliacha kazi eti anaenda kulima matikiti, kilio alichonacho sasa....

Tuwe tunafuatilia siasa kidogo, wengine alipoingia tu Mtukufu kwa kauli zake za mwanzo tuliona ana mtazamo mbaya na secta binafsi, na ndio kinachotokea.
Zabibu imekosa soko wakulima wanalia! Hizi ni changamoto katika uzalishaji muhimu kuchunguza soko Kabla ya kuwekeza!
Soko limeyumba sana
Soko Soko Soko......
 
Ref my previous post

Namshukuru mwenyezi Mungu muumba wq mbingu na ardhi kwa pumzi na afya njema aliyonijaalia

ilinichukua miaka mitano na nusu kuacha kazi ya serikalini nashukuru Mungu kwa walionisupport juu ya uamuzi wangu huo

nliwakwepa wale wote ambao nlihic watanikatisha tamaa hasa wazazi wangu ilibidi nimtengenezee mazingira ya kutokuniomba hela ya kila mwezi kwa kumwekea pooltable linalomwingizia 150000 kila mwezi

Ninachofanya baada ya kuacha kazi

Ninalima matikiti maji,Zukini na pilipili za kuwasha nimeanza na tikiti maji heka 3 pilipili za kuwasha nusu heka na zukini nusu heka

Zukini na pilipili ndo zao ninalolitegemea kulifanya liwe zao la biashara nimelilima chache kwasababu ckuwahi kulima zukini na pilipili so natafuta experience

tikiti ziko poa ntawaonyesha picha za zilipofikia

Biashara

nimefanya biashara ya mbolea ya mavi ya kuku kwa muda wa week 2 nimeingiza faida ya laki4 though changamoto imekuja kwenye savings kila nkipata hela mahitaji ya shamba yanaongezeka mf dawa mbolea ya dukani kuwalipa posho vibarua nk

Uzuri wa kujiajiri

unaamua ufanye nini muda gani mwenyewe yaani kama nkiamua nisafiri hata nw naweka mipango sawa naenda popote inshort nipo huru

changamoto kuubwa nliyoiona

Savings na mifuko ya jamii

faida inapaswa ihifadhiwe kiac kikubwa kuliko kukitumia mara nyngi tunatumia hela pale tunapokua nazo tusipokua nazo ni ngumu sana kuzitumia natamani nijifunze mbinu ya kisave

natamani nijiunge na ule mfuko binafsi wa penshen tatizo huku Jaribu(kibiti) hakuna hicho kitu

View attachment 848013View attachment 848015View attachment 848016

Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera sana mkuu kwa huo UJASIRI maana kuajiriwa kunazalisha uoga wa hali ya juu

Halafu umechagua mazao exclusive inaonesha ulijipanga.
 
Huu ujasiri nauvutia pumzi sana,time will tell,haiwezekani 5yrs mshahara hata mia hauongezeki,cheo kile kile,matamko kila uchwao,HONGERA MKUU NA MUNGU AKUONGOZE BAADA YA UAMUZI HUO
 
Haya ni maamuzi magumu sana ambayo kwangu si sahihi. Hata kwenye biashara tunafundishwa umuhimu wa portfolio mkuu, unaachaje kazi wakati huna pa kushika? Hukumsikia Dk Lutengwe? Ulitakiwa ukomae na ujasiriamali hivyo hivyo ukiwa umeajiliwa hadi pale utakaposimama ndo uache kazi, ipo siku utajuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ushauri kwa mtu unayetaka kuacha kazi usichukue...hawa ndo wanaowapa uoga wenzao huko maofisini...nilishapitia situation kama hii na bahati mbaya wengi ya watu waliokua wamenizunguka ni kama huyu nilichukua maamuzi magumu na bahati nzuri nimefanikiwa kwa hichi kidogo nipatacho...wale waliokuwa wananipa uoga ndo hao ckuhz wananipigia simu eti niwashauri namna ya kuchomoka kule..za kuambiwa changanya na zako..cha msingi kila mmoja afanye moyo wake unachomtuma
 
Huu ushauri kwa mtu unayetaka kuacha kazi usichukue...hawa ndo wanaowapa uoga wenzao huko maofisini...nilishapitia situation kama hii na bahati mbaya wengi ya watu waliokua wamenizunguka ni kama huyu nilichukua maamuzi magumu na bahati nzuri nimefanikiwa kwa hichi kidogo nipatacho...wale waliokuwa wananipa uoga ndo hao ckuhz wananipigia simu eti niwashauri namna ya kuchomoka kule..za kuambiwa changanya na zako..cha msingi kila mmoja afanye moyo wake unachomtuma
Mkuu ni wangapi waliofanya kama wewe wakafanikiwa?? Akili za kuambiwa hizi.
 
Huu ushauri kwa mtu unayetaka kuacha kazi usichukue...hawa ndo wanaowapa uoga wenzao huko maofisini...nilishapitia situation kama hii na bahati mbaya wengi ya watu waliokua wamenizunguka ni kama huyu nilichukua maamuzi magumu na bahati nzuri nimefanikiwa kwa hichi kidogo nipatacho...wale waliokuwa wananipa uoga ndo hao ckuhz wananipigia simu eti niwashauri namna ya kuchomoka kule..za kuambiwa changanya na zako..cha msingi kila mmoja afanye moyo wake unachomtuma
Pia kusema hivyo haimaanishi kumkatisha mtu tamaa bali kumsaidia the risk around ili azipunguze inapobidi. Mtoa uzi mwenyewe kasema alimnunulia Baba yake pool table kabla ya kuacha kazi.
 
Mkuu ni wangapi waliofanya kama wewe wakafanikiwa?? Akili za kuambiwa hizi.
Kwani wangapi ambao wapo kwenye hizo ajira wamefanikiwa????..mbona hata waliopo kwenye hizo ajira wanalia tu njaa...cha msingi kila mtu afuate moyo wake unachomtuma afanye lakini tusitishianetishiane.
 
Kwani wangapi ambao wapo kwenye hizo ajira wamefanikiwa????..mbona hata waliopo kwenye hizo ajira wanalia tu njaa...cha msingi kila mtu afuate moyo wake unachomtuma afanye lakini tusitishianetishiane.
Kilio cha wenye ajira ni tofauti kabisa na cha wasio na ajira au waliojiajili. Kufata moyo wako bila risk assessment ni hatari. Nadhani kila mtu apime uwezo wake wa kuhimili hiyo risk ikitokea mambo yakagoma. Halafu dhana ya kusema kuajiliwa ni kubaya si nzuri, maana ukijiali nawe utahitaji kuajili watu, sasa kama wote wakichukia kuajiliwa itakuwaje. Mwisho si kwamba kupitia ajira huwezi fanikiwa ni mahesabu tu.
 
Pia kusema hivyo haimaanishi kumkatisha mtu tamaa bali kumsaidia the risk around ili azipunguze inapobidi. Mtoa uzi mwenyewe kasema alimnunulia Baba yake pool table kabla ya kuacha kazi.
Maneno aliyoongea ndo hayohayo wanayoongea huko maofisini wakiona mwenzao anataka kuachana na kuajiriwa ili kukatishana tamaa...kila mtu anapofanya maamuzi lazima kuna vitu anakuwa amejipanga
 
Kilio cha wenye ajira ni tofauti kabisa na cha wasio na ajira au waliojiajili. Kufata moyo wako bila risk assessment ni hatari. Nadhani kila mtu apime uwezo wake wa kuhimili hiyo risk ikitokea mambo yakagoma. Halafu dhana ya kusema kuajiliwa ni kubaya si nzuri, maana ukijiali nawe utahitaji kuajili watu, sasa kama wote wakichukia kuajiliwa itakuwaje. Mwisho si kwamba kupitia ajira huwezi fanikiwa ni mahesabu tu.
Wenye ajira unaowazungumzia wewe ni wapi...hawa ma teacher wanaolipwa laki tatu????
 
Maneno aliyoongea ndo hayohayo wanayoongea huko maofisini wakiona mwenzao anataka kuachana na kuajiriwa ili kukatishana tamaa...kila mtu anapofanya maamuzi lazima kuna vitu anakuwa amejipanga
Anhaaa kumbe hadi ujipange? Si uache tu, sasa kwa nini husisitizi vitu gani mtu ajipange kwanza? Ingekuwa vizuri ukajikita zaidi kwenye kufundisha vitu vya kujipanga kabla ya kuacha.
 
Anhaaa kumbe hadi ujipange? Si uache tu, sasa kwa nini husisitizi vitu gani mtu ajipange kwanza? Ingekuwa vizuri ukajikita zaidi kwenye kufundisha vitu vya kujipanga kabla ya kuacha.
Hamna mtu anayeacha kazi then hajui na hajafanya mipango ya kesho yake...kila mtu anaacha na kichwani mwake anajua anaenda kufanya nini...nachopinga mimi ni mtu yupo kwenye ajira then anampa ushauri mtu anayeacha kazi na anamshauri eti aanzishe mradi wakati yupo kwenye ajira ili mradi ukikua ndo aache kazi wakati huohuo huyo anayetoa ushauri na yupo kwenye ajira hana mradi hata wa kufuga kuku wawili....unanishauri vipi mimi namna ya kupata mafanikio wakati we we hunabhayo mafanikio...or wewe hupendi mafanikio...maswali yangu ndo huwa yapo hapo
 
Ajira rasimi yoyote.
Kama ndo hao tunaishi nao huku mtaani usituambie chochote kuhusu wao...tunawaona kwa macho yetu...alafu wengine tushapitia huko kwa hiyo tunajua kila kitu...na si kwamba huku tulipo kuna maisha mazuri hakuna...but tunaiona tofauti...cha msingi naendelea kusisitiza kila mtu afanye moyo wake unachopenda...
 
Wewe hujaacha kazi mkuu umebadilisha kazi kutoka Kuajiriwa na kujiajiri,kazi yako ili ikukomboe kiuchumi unatakiwa ufikie kiwango cha kuwa na watu uliwaajiri kisha wakuletee pesa zaidi sana ni namna ya kufanya kutengeneza channel ili pesa zikufuate wewe nasio sio viceversa hapo ndio tutasema kuwa ajira binafsi imekukomboa wala haitakiwi iwe ni msuguano mkali wa harakati za kutafuta pesa ili ulipie wage bills za na manpower yako katika phase ya mwanzo ya kujenga uchumi ni ngumu sana lakini ikifanikiwa kuweka mifumo na kuisimamia phase ya pili ni Monitoring na phase ya tatu ndio harvesting kila na kupata returns ambazo zitakufanya hata wakati unarudi kwenye kazi yako ya kilimo basi hata income yako kutoka vyanzo vyako ikusaidie usistruggle sana kuendesha kilimo chako.Ukiona vipi unaweza kubadilisha diversify mtaji wako kutoka kwenye ukulima ukawa mtu kununua na kuuza mazao,hapo itakupunguzia charges nyingi za kulipa watu wengi na faida yako itategemea nguvu ya soko.Wanaokimbia kilimo na gharama zake za uendeshaji wanapata faida mara3 zaidi ya kuwa wakulima na wauzaji wa mazao yao wao wenyewe.
Nikutakie Harakati njema sana za kujikomboa Kiuchumi Direction ndio msingi wa ustawi wako.
 
Back
Top Bottom