Mrejesho: Ugumu wa kupata kibarua hapa Mradi wa Bwawa la Umeme la Nyerere

kasagamba

Member
May 27, 2020
46
51
Wakuu habarini za majukumu! Ni karibu miezi 2 sasa toka nilipotoka Dar na kujielekeza Morogoro eneo la Kisaki kutafuta riziki ya familia kwenye Ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Umeme.

Wakuu huu mradi ni mkubwa sana ila utaratibu wa kuchukua wafanyakazi hasa get la Kisaki ni mbovu sana.

Wajumbe na viongozi wa kijiji hiki ndio wanaoamua nani achukuliwe na nani aachwe. Hivyo kama hauna ile kitu inaitwa Rupia basi utaendelea kuchina huku watu unaona wanaingia tu.

Mimi kwa kuwa ni maskini sina kitu, nimeamua nirudi nyumbani angalau labda nikiwa huko naweza kupata hata kibarua cha kumsaidia Fundi familia ikapata riziki kuliko kukaa huku bila ramani yoyote huku watoto wakifa njaa.

Wakuu Mimi ni Fundi Chuma (steel fixer) ila kama kuna mtu ana kibarua chochote basi anipe nipate riziki ya watoto.

Asanteni

Nitoe tahadhali kama huna mipango ya chini chini usipoteze nauli yako
 
Ulishajaribu kwenye ujenzi wa stendi ya mkoa pale Mbezi Mwisho?​
Jaribu kufika pale asubuhi kwenye saa moja.​
Ukifika kwenye geti asubuhi wewe ingia Kama Kibarua mwenyeji andika jina halafu nenda kwenye mabanda ulizia fundi yeyote mwenye nafasi unaweza pata ndani ya siku hata tatu ila usifike getini useme mm mgeni utazuiliwa kuingia utabaki nje mafundi huwa wanakosa wasaidizi wakati mwingine.​
 
Ulishajaribu kwenye ujenzi wa stendi ya mkoa pale Mbezi Mwisho?​
Jaribu kufika pale asubuhi kwenye saa moja.​
Ukifika kwenye geti asubuhi wewe ingia Kama Kibarua mwenyeji andika jina halafu nenda kwenye mabanda ulizia fundi yeyote mwenye nafasi unaweza pata ndani ya siku hata tatu ila usifike getini useme mm mgeni utazuiliwa kuingia utabaki nje mafundi huwa wanakosa wasaidizi wakati mwingine.​

Mkuu nakushukuru sana Kwa ushauri Maana narudi mjini lakini sina mipango , Najisikia vibaya nimekaa mbali na familia karibu miezi 2 nasubiri kibarua narudi nyumbani na beg tupu bila hata biskuti ya mtoto.
 
Mkuu nakushukuru sana Kwa ushauri Maana narudi mjini lakini sina mipango , Najisikia vibaya nimekaa mbali na familia karibu miezi 2 nasubiri kibarua narudi nyumbani na beg tupu bila hata biskuti ya mtoto.
Pole Mkuuu usikate tamaa, naamini mlango huo kama umefungwa ukifika pengine utapata riziki. Pambana Mkuu kesho yako ipo
 
Pole bro, huwa nakuwaga sana na usikate tamaa, huwa napenda sana vijana wenye kupambana kwelikweli kuliko kukaa kulaumu tu.
Pitia kwenye miradi mbalimbali iliyo karibu na wewe ili kuokoa gharama. Nina imani utapata, kwa kuwa kazi za usaidizi wa fundi ni nyingi sana kwa kuwa mafundi wakuu wengi huwa ni wavivu na wamebweteka
 
Pole bro, huwa nakuwaga sana na usikate tamaa, huwa napenda sana vijana wenye kupambana kwelikweli kuliko kukaa kulaumu tu.
Pitia kwenye miradi mbalimbali iliyo karibu na wewe ili kuokoa gharama. Nina imani utapata, kwa kuwa kazi za usaidizi wa fundi ni nyingi sana kwa kuwa mafundi wakuu wengi huwa ni wavivu na wamebweteka
Pole bro, huwa nakuwaga sana na usikate tamaa, huwa napenda sana vijana wenye kupambana kwelikweli kuliko kukaa kulaumu tu.
Pitia kwenye miradi mbalimbali iliyo karibu na wewe ili kuokoa gharama. Nina imani utapata, kwa kuwa kazi za usaidizi wa fundi ni nyingi sana kwa kuwa mafundi wakuu wengi huwa ni wavivu na wamebweteka
Mkuu Asante kwa ushauri Mungu awe na we
 
Back
Top Bottom