Mrejesho: Tatizo langu la kupata mkojo tena dakika chache kila baada ya kumaliza kukojoa

Pole sana mkuu
nikuulize maswari machache hunijibu

1*je kasi (presha ya mkojo) imepungua
yaan unajikwinya sana kuutoa mkojo
2*je mkojo hutoka ukiwa mwembamba sana(yaan ukubwa wa mkojo vile unatoka upo tafauti na zamani)
3*je wakati mwingne mkojo hutoka km mabomba mawiri au matatu yaan hutawanyika hasa km ukiwa umetoka kuamka
4*je ukimaliza kukojoa ushafunga zipu huwa unajihisi km chembechembe za mkoja zinatoka zinamalizia
5*umeoa au unaishi na mwanake au mpenz ambaye mnakutana(sex) mara kwa mara
6*je huwa unafanya au uliwahi kuwa unafanya punyeto sana
7*je chini ya mbavu au juu ya kitovu pande zote huwa unajihisi maumibu makari hasa mkojo ukiwa umekubana ?
8*kutoka kwenye mbavu kuja kwenye kibovu huwa unahisi km kuna tube(mithiri km bomba) zinawaka moto au maumivu yanafanana na kidonda km kimewekwa ndimu
8*je huwa unahisi maumivu kwenye kibofu yaan kibofu km kinawaka moto mitihili kidonda kilichowekwa ndimu
9*ukimaliza kukojoa huwa unahisi ahueni kubwa kwenye kibofu mpk ureta ambayo udumu kwa muda mchache
10*je kiasi cha mkojo huwa unatoa kwa wingi kutokana ns kukuuma kwa kasi au ni kwa uchache mkojo wa asubuhi huwa unakoa kwa uchache pia
11* je hilo tatizo tangu limekuanza lina muda gani ?
12* swali la mwisho je imefikia hstua unaogopa kunywa maji mengi kuhofia mkojo?

Majibu
1.Kasi yamkojo ni ile ile Kama nimekunywa maji mengi Kama sijanywa inapungua
2.ukubwa wa mkojo nikiwa nimebanwa Kama nimekunywa maji ni ule ule Ila Kama sijanywa ni mwembamba
3. Ndio wakat mwingne Ila Mara chache Sana usiku nikiamka kukojoa unaweza toka Kama uko ktk mabomba mawili au unatoka Kama Bomba moja Ila unakua Kona unapinda pembeni yaan hauwi direct
4.ndio nikimaliza kukojoa nikiwa uume umo ndani au kuupitisha ktk zipu kuingia ndani naskia matone yanamalizikia tone
5.nimeoa Nina mke Ila sikutani nae Mara kwa Mara yaan sishiriki nae tendo la ndoa Mara kwa Mara
6.nilishawahi fanya punyeto Mara 7 tu ktk kipindi choote mpaka nafika umri huu
7.ndio upande wa chini yambavu hasa wakulia huwa nahis maumivu Kama simaumivu Hali flani yakitu kimejaa hivi hasa mkojo unapokua umenibana nanikachelewa kwenda kukojoa nahis hiyo Hali Kama mkojo utakua upanda juu mbavu usawa wakuja ktk kitovu
8.kwenye kibofu huwa sihisi maumivu yoyote Zaid yakuhisi kitu flan kukaa kufura kama mkojo umenibana nikachelewa kidgo kwenda kojoa nahis Hali hiyo yapia mkojo kwenda usawa wa mbavu
9.ndio nikimaliza kukojoa huwa nahis ahueni kubwa kabisa ktk kibofu
10.kiasi Cha mkojo huwa natoa kingi Kama nimekunywa maji mengi namkojo nausukuma kwa Kasi napia asubuh napata kiasi Cha mkojo sio kwa wiingi kwakiasi sio kidogo Wala kingi Ila nakipata usiku wamanane na asubuh pia
11.tatizo tangu limenianza linamuda wamiaka Kama miaka 4 au Zaid sichini yahapo maaana sinakumbukumbu vizur
12.ndio imefika hatua naogopa Kunywa maji mengi kuhofia mkojo hasa nikiwa safarini yamasaa kuanzia mawili au nikiwa katika shuguli zakualikwa au kwenda kwenye maofisi yawatu kwakuogopa kupata mkojo nakwenda chooni Mara kwa Mara.. Ila nikiwa mwenyewe nakunywa mengi tu sihofiii kwenda chooni maana nikinywa maji mengi nikiwa mwenyewe baada dk40 mkojo utaanza kubana nasafar yakwenda chooni Mara kwa Mara unaanza kila baada ya dk30 au Zaid ntaenda Mara Zaid ya7 mpaka nihisi sinamkojo ktk kibofu
Nadhani nimeyajibu maswali yako yoote mkuu
 
Navyoona una Incomplete Bladder Emptying ambayo inaweza kutibiwa kwa dawa za kawaida tuu.

Labda tujue walikupa dawa gani mkuu wangu.
 
Wakuu Leo nimeleta mrejesho wa tatizo langu la kukojoa Mara kwa mwara na kupata mkojo Tena kila napomaliza kukojoa baada ya dakika kadhaa nabanwa Tena na mkojo yaan kiufupi mkojo hausishi.

Wakuu nilifuata ushauri wenu nikafika Muhimbili kitengo cha urology nikamuelezea daktar kila kitu, daktari akaelekeza nikafanyiwe vipimo vya damu,ultrasound na mkojo.

Majibu yaliyotoka ya vipimo ya sina ugonjwa wowote na wakati nafanyiwa kipimo Cha ultrasound nimemaliza wakanambia kakojoe uje tuendelee kufanya kipimo nilipoenda kukojoa nikakojoa kuumaliza mkojo wote Ila baada ya kurud kuendelea na kipimo wakapima Tena ultrasound wakaona kibofu kina mkojo tena, nikawaambia hilo ndio tatizo langu sasa.

Ikabidi waendelea kuangalia ini ktk mbavu chembe ya moyo koote hawakuona kitu wakasema labda huyu afanyiwe kipimo wakataja kipimo sjui kipimo gani skukielewa walitaja kingereza. Kesho yake nilirudi kwa daktar akanisomea majibu akasema majibu yanaonyesha hakuma chochote tezi dume iko sawa ndogo Sana pia kibofu kipo sawa pia figo ziko sawa pia nakipimo Cha damu kipo sawa.

Dokta akanambia inabid Sasa labda ufanyiwe kipimo cha kupitisha kifaa ktk tundu la njia yamkojo mpaka ktk kibofu kuangalia kuna nin shida hapo...kiukweli mimi niliwazaaa hili lakupitisha kifaa ktk njia yamkojo nkaogopa ikabid nimfiche daktari kuwa kwasasa sinapesa yakopimo mpaka baada miezi mitatu ikizingatia naishi mkoani basi daktari akawa kaniandikia nirudi mwezi wanne kwa ajili ya hiko kipimo
Wakuu huu ndio mrejesho wangu je kipimo hicho nilichoandikiwa je ni salama kweli kwa afya ya uume wangu na njia pia ya mkojo.
Nime ku pm. Nina uhakika wa 90% utapona. Pole sana
 
je kipimo hicho nilichoandikiwa je ni salama kweli kwa afya ya uume wangu na njia pia ya mkojo.

Mkuu watu wanapasuliwa kichwa na wengine wanapasuliwa moyo na wanapona sembuse hako kakipimo?

Kwa taarifa yako Daktari ili aitwe daktari anatumia miaka mitano plus mmoja (jumla sita) kuusoma mwili wako kuanzia kwenye nywele mpaka kwenye kuchaya kidole gumba cha mguu acha kuwa na wasi wasi!

Infact hata ulivyosema huna ela alijua kabisa unaogopa kipimo sema hakukuambia tu!!
 

malembeka18 mkuu mimi niliwahi kuumwa na tatizo linalohusiana na mkojo miaka ya nyuma, nilihangaika sana bila ya mafanikio, nilimaliza vipimo vyote hakuna kilichoonekana, nikabakisha hicho kipimo unachokisema, ila Doctor aliekua ananishughulikia alinishauri nisikifanye mpaka hali itakapofika kuwa mbaya, mana ukikifanya kitakutia obovu wa maisha. kwa kweli sikikufanya.

Nilikuja kufanikiwa kupowa tatizo langu kwa njia za asili baada miezi kadhaa mbele.
 

malembeka18 mkuu mimi niliwahi kuumwa na tatizo linalohusiana na mkojo miaka ya nyuma, nilihangaika sana bila ya mafanikio, nilimaliza vipimo vyote hakuna kilichoonekana, nikabakisha hicho kipimo unachokisema, ila Doctor aliekua ananishughulikia alinishauri nisikifanye mpaka hali itakapofika kuwa mbaya, mana ukikifanya kitakutia obovu wa maisha. kwa kweli sikikufanya.

Nilikuja kufanikiwa kupowa tatizo langu kwa njia za asili baada miezi kadhaa mbele.
Njia zipi za asili zilizokusaidia mpaka ukafanikiwa kupona
 

malembeka18 mkuu mimi niliwahi kuumwa na tatizo linalohusiana na mkojo miaka ya nyuma, nilihangaika sana bila ya mafanikio, nilimaliza vipimo vyote hakuna kilichoonekana, nikabakisha hicho kipimo unachokisema, ila Doctor aliekua ananishughulikia alinishauri nisikifanye mpaka hali itakapofika kuwa mbaya, mana ukikifanya kitakutia obovu wa maisha. kwa kweli sikikufanya.

Nilikuja kufanikiwa kupowa tatizo langu kwa njia za asili baada miezi kadhaa mbele.
Dokta alikuambia unaweza kupata ubovu wamaisha upi
 
Mkuu Pole sana kuhsu hicho kipimo cha kutia katika tundu la dushelele lako hakina ubaya. Nikuulize swali unakuw amtu mwenye mawazo sana? na ninahisi utakuwa na maradhi yanayotokana na mambo ya giz aikiwa vipimo vyote umepima na hakuna maradhi yaliyo onekana basi utakuwa unayo maradhi ya kichawi . Ushauri wangu pia jaribu utibiwe na dawa zetu za asili ili uweze kupata kupona ikiw aunaogopa kutiwa kipimo katika dushelele lako.
mzizi upo sahihi kabisa kwenye hili.....nguvu za giza zimefungwa na kizazi chake ndio maana....@mgonjwa wasiliana na mzizi atakusaidia ni ushauri tu ila maamuzi ya mwisho utabaki nayo mwenyewe ila dawa zipo upande wa pili huo ulioshauriwa.
 
Wakuu Leo nimeleta mrejesho wa tatizo langu la kukojoa Mara kwa mwara na kupata mkojo Tena kila napomaliza kukojoa baada ya dakika kadhaa nabanwa Tena na mkojo yaan kiufupi mkojo hausishi.

Wakuu nilifuata ushauri wenu nikafika Muhimbili kitengo cha urology nikamuelezea daktar kila kitu, daktari akaelekeza nikafanyiwe vipimo vya damu,ultrasound na mkojo.

Majibu yaliyotoka ya vipimo ya sina ugonjwa wowote na wakati nafanyiwa kipimo Cha ultrasound nimemaliza wakanambia kakojoe uje tuendelee kufanya kipimo nilipoenda kukojoa nikakojoa kuumaliza mkojo wote Ila baada ya kurud kuendelea na kipimo wakapima Tena ultrasound wakaona kibofu kina mkojo tena, nikawaambia hilo ndio tatizo langu sasa.

Ikabidi waendelea kuangalia ini ktk mbavu chembe ya moyo koote hawakuona kitu wakasema labda huyu afanyiwe kipimo wakataja kipimo sjui kipimo gani skukielewa walitaja kingereza. Kesho yake nilirudi kwa daktar akanisomea majibu akasema majibu yanaonyesha hakuma chochote tezi dume iko sawa ndogo Sana pia kibofu kipo sawa pia figo ziko sawa pia nakipimo Cha damu kipo sawa.

Dokta akanambia inabid Sasa labda ufanyiwe kipimo cha kupitisha kifaa ktk tundu la njia yamkojo mpaka ktk kibofu kuangalia kuna nin shida hapo...kiukweli mimi niliwazaaa hili lakupitisha kifaa ktk njia yamkojo nkaogopa ikabid nimfiche daktari kuwa kwasasa sinapesa yakopimo mpaka baada miezi mitatu ikizingatia naishi mkoani basi daktari akawa kaniandikia nirudi mwezi wanne kwa ajili ya hiko kipimo
Wakuu huu ndio mrejesho wangu je kipimo hicho nilichoandikiwa je ni salama kweli kwa afya ya uume wangu na njia pia ya mkojo.
MKUU UNAYO MARADHI YA KUTOKWA KWA MKOJO KWA WINGI BILA YA KHIARI (POLYURIA):
Haya ni maradhi ya kutokwa na mkojo bila ya khiari .
Kabla mkojo haujakusanyika vizuri kwenye kibofu cha mkojo na mgonjwa kujiandaa kwenda

chooni, hutokwa na mkojo hata kabla ya kufika chooni. SABABU:
(1) Kulegea kwa kibofu cha mkojo.
(2) Maradhi ya kisukari.
(3) Kuwa na minyoo tumboni.
(4 Kutumia madawa ambayo huchochea kutokwa kwa mkojo.
(5) Kuwa katika mazingira au hali ya hewa ya baridi.
(6) Kunywa kwa wingi vinywaji, pombe,n.k.
Tiba yake ninaijuwa nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibia maradhi yako upate kupona uguw apole.
 
Mkuu polee sana. Hicho kipimo kinaitwa urethrogram. Nakushauri ufanye ili iwe rahisi kujua tatizo lako. Usipende sana ramli mkuu. Maumivu ni kidogo sana na pia unakuwa exposed kwenye radiations. Otherwise nadhani ni njia sahihi kujua tatizo lako.

Hicho kipimo wala kisikutishe, kuna vingine ambavyo ni very worse. Mfano barium enema( unapitishiwa kupitia njia ya haja kubwa)
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom