Mrejesho: Mke wangu anapenda maisha ya matawi ya juu

Yaleyale

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
1,789
2,383
Kwanza nianze kuwatakia heri ya Mwaka Mpya.

Mwishoni mwa mwaka jana nilikuja na mada niliyoita Ushauri: Mke wangu anapenda maisha ya matawi ya juu

Nashukuru wadau kwa michango yao mazuri.

Kifupi ni kuwa nilikubaliana naye tukasafiri kwenda mapumziko Zanzibar kwenye hoteli alizokuwa ameona ndo "size" yetu kukaa. Pesa ilinitoka kweli lakini nilivumilia machungu hayo.

Wakati wa mapumziko hayo tulitenga muda wa kutafakari malengo tuliyojiwekea kwa mwaka 2016 na kwa kiwango gani tumeweza kuzifikia. Vilevile kwenye tulizungumzia mipango kwa 2017.

Hivyo pamoja na mambo mengine, tumekubaliana kuwa kuanzia mwaka 2017 Kipato changu na faida inazopatikana kwenye biashara yetu itatumika kuangalia usitawi wa maendeleo ya familia ikiwemo kujenga nyumba za kupangisha kwenye kiwanja chetu kile. Pili, pesa za "kula bata" na kwenda next mapumziko kama itakuwa nje ya Dar zitatoka kwenye akiba yake (mshahara wake).

Tuliongea mengi na kimsingi nimeandaa kabisa muktasari wa kikao na maamuzi. Hivyo akitaka tena kwenda sijui Dubai, Comoro natoa muktasari wa kikao na kumuuliza ameshajiandaa kiasi gani.

Nimalizie kuwashukuru wadau na tuendee kusaidiana kimawazo hapa jukwaani.
 
Haya..! Nadhani ambao wamezoea kutuletea story za Uongo wamekusikia..mkuu!

Anyways, Hongera..mkuu..!
Huu mwaka uwafungulie kila Gumu.. liwe Jepesi
 
Kama utakuwa mtafiti kuna humu hawapendi kusikia mafanikio ya wenzao japo yanakuja katika hali ya changamoto, hivyo mtu akiona katika upande wa mafanikio roho yake yakorosho inapata moto na kulipuka ndio unaanza kuona maneno kama : wewe nimtunzi mzuri, acha uongo na maneno yanayofanana na hayo! Acheni wivu kama katunga atajijua mwenyewe piga kazi weka malengo omba Mungu utatoka tu,
 
Huu mrejeshoo mkuu umekaa poa achana na wanaokukatisha tamaa ukiona mwanamke wako bado anapenda mitoko japo kwa pesa yake jua huyo ndio hulka yake ukiona mitoko haipo weka alama hii? Kwa nn ilikua pesa zangu mitoko y? Pesa zake hakuna mitoko
 
mkuu weka hapa minutes za kikao ili tuzi approve kabla hujazisign!
 
Usisahau mrejesho baada ya miezi sita..... Usijidanganye tatizo limeisha ukaja umbuka.....
 
Tuliongea mengi na kimsingi nimeandaa kabisa muktasari wa kikao na maamuzi. Hivyo akitaka tena kwenda sijui Dubai, Comoro natoa muktasari wa kikao na kumuuliza ameshajiandaa kiasi gani.

Hapo naona kabisa huo muhtsari akiukana siku si nyingi, kwanza anaamini utasahau.
 
Mkuu huyo mkeo ndiyo anafaa Kwa maisha, siyo unakua na mke kwenye bajaji, boda boda anasinzia ataua kipaji.
 
Tuletee na wewe uone kama kutunga za uongo bila tukio halisi ni kazi rahisi!
ungenielewa ingekusaidia mkuu!
sijamaanisha huyu ndio muongo.
What I mean, alileta story ya kweli.. akapewa ushauri, umemsaidia..

sasa what I say.. kwa wale wanaoleta story za Uongo.. wajifunze..

Au na hilo nalo hadi uende chuo kikuu..
 
Back
Top Bottom