supercharger GT
JF-Expert Member
- Sep 25, 2016
- 1,007
- 1,943
Kwanini wanawake wanakuwa desperate na ndoa?
Juzi hapa nilipost kisa changu nikielezea hilo suala. Wengi walishiriki maoni ambayo kweli yalikuwa positive sana na ndo vile vile ambavyo hata mimi nilikuwa nafikiria.
Leo mchana niliamua kuonana na yule binti coz kwanza sina tatizo naye na pia namfahamu vizuri sana hivyo pia mimi suala hili nilikuwa nalichukulia uzito nikijua kuwa lazima litaleta matatizo mbeleni endapo mume wake angejua kuwa huyu binti anataka kulamba cha zamani(maana pia huyu binti huwa hana umakini na simu yake na huwa hana tabia ya kufuta sms au calls) na pia angeona sijachukua hatua yoyote kwa mambo anayotaka mkewe;
twende moja kwa moja kwenye mada
Kuanzia asubuhi tulikuwa tunachat kawaida tu ila wakati mwingine akiweka yale mambo yake, katika majibu yangu nikamwambia atafute muda anaoona unafaa leo tukutane mahali palipotulia nina maongezi naye marefu, kwanza akaogopa akidhani huenda nimewasiliana na mume wake, nikamtoa hofu kwa kumwambia kuwa sina hata namba yake huyo jamaa basi akasema tukutane mchana mahali fulani pametulia.
Mchana nikawahi eneo hilo nikaagiza bia yangu nikawa nashusha mdogo mdogo(huu mji wetu watu wanakunywa tu tangu asubuhi kama vile hakuna ile sheria). Baada ya muda akaja akiwa kavaa vizuri sana kwa style ambazo tukiwa wapenzi nilikuwa napenda avae namna hiyo!! Kufika tu akawa anaona aibu kuongea hata salamu yenyewe katoa kwa kuangalia chini, nikaona nimuagizie nayeye Castle lite ili awake kidogo maana ni kichwa panzi ila anapenda kuonekana shujaa kwenye mambo mengi. Basi tukawa tunaendelea na maongezi ya kawaida kabisaa bila lile suala kuligusia, ikafika muda nikaona aibu zimeanza mtoka akaanza kuongelea mambo ya ndoa yake, na alipokuwa anaongea anaonekana kabisa kama anatua mzigo fulani mzito moyoni mwake, na kumbuka hapo mimi hata sijamuambia kuwa nimemuitia maongezi gani!!! Alianza kwa kunitaja jina langu, halaf akasema " yaani ningejua ningesikiliza hata maneno ya marafiki zangu kuhusu John, sijui alinifumba nini nikawa kipofu kabisa nisione lolote nikatamani tu kuitwa mke wake" baada ya hapo akafunguka sasa!!!!!! Kwa kwel mambo aliyonisimulia nilihisi ananidanganya, nikawa namkatalia kuwa anamsingizia mumewe, akachukua simu yake na kuanza kunionesha sms za mume wake, na evidence zingine kwa kweli nilichoka! Sometimes na sisi wanaume tunachangia 100% wanawake kucheat nje ya ndoa. Mambo hasa aliyonisimulia mpaka yamefikia yeye kuanza kutamani kuwa na mimi upya ni;
1: mwanaume anajali sana pesa kuliko utu au thamani ya mke mwenyewe, anaweza mnunulia hata bangili bahat mbaya ikipotea bas ni kipigo na mwisho wa siku anakuwa anamkemea kwamba anajua kainunua kwa bei gani? ( na anasema mume wake anajua kwel kupiga, kitu kidogo tu basi ni mrahisi kurusha kofi kama sio ngumi)
2: hataki afanye kazi, anataka awe anakaa tu nyumbani(huyu dada ana Diploma ya nursing)
3: jamaa ana wanawake kibao nje ambao inafika mahali had anakuwa anawatambua, ila cha ajabu ni kwamba hata wakati anaolewa naye alikuwa anajua kuwa ana wapenzi nje(hapa sikumuelewa na nilimshangaa sana kwa kwel)
4: Hapa ndo alinichekesha, kwamba mume wake anaweza kaa hata mwez mzma hajamgusa kabisaaa, na bado hana muda hata wa kuongea nae vzur, yeye akiamka ni kazini tu na mambo mengne, ila akiwa na hitaji la pesa anapewa kiasi anachotaka ila ajue jamaa hatasahau hyo pesa alompa!
5: Wivu ulopitiliza, anataka muda wote awe nyumbani, asiwe na marafiki wa kike wa ajabu ajabu, hataki akasuke salon ikitokea bas ni shingo upande.
6: Attention, na affection zile. Mwanaume hayupo romantic hata kidogo, hajui mke anataka nini kwa sasa, zaman anasema alikuwa anajaribu kumuambia ila mume anamjibu kuwa ana mambo ya kitoto
Evidence alizonionesha kwenye cm yake ni pamoja na sms ambazo yeye anamlalamikia kwanini hampi haki yake na jamaa anajibu kwamba mwanamke huyo anapenda sana ngono kuliko kitu chochote, na mambo mengne mengi ambayo siwezi yaandika humu yote!
Baada ya hapo, jambo nililomshauri ni aongee nae hali halisi na amueleze madhara yanayoweza tokea kama hatojirekebisha, pia amuambie wazi kuwa kwa mume wake kufanga hvyo kunahatarisha ndoa yake ikiwemo kuvunjika kabisa.
Akifanya hvyo na kama hakuna mabadiliko basi ahusishe viongozi wa dini au wazazi!
Mrejesho huu nimeona niulete humu kwa ajili yetu wanaume, ingawa na wanawake pia, ila kwa case kama hii tunaona kabisa nani ni Victim hapo!
Juzi hapa nilipost kisa changu nikielezea hilo suala. Wengi walishiriki maoni ambayo kweli yalikuwa positive sana na ndo vile vile ambavyo hata mimi nilikuwa nafikiria.
Leo mchana niliamua kuonana na yule binti coz kwanza sina tatizo naye na pia namfahamu vizuri sana hivyo pia mimi suala hili nilikuwa nalichukulia uzito nikijua kuwa lazima litaleta matatizo mbeleni endapo mume wake angejua kuwa huyu binti anataka kulamba cha zamani(maana pia huyu binti huwa hana umakini na simu yake na huwa hana tabia ya kufuta sms au calls) na pia angeona sijachukua hatua yoyote kwa mambo anayotaka mkewe;
twende moja kwa moja kwenye mada
Kuanzia asubuhi tulikuwa tunachat kawaida tu ila wakati mwingine akiweka yale mambo yake, katika majibu yangu nikamwambia atafute muda anaoona unafaa leo tukutane mahali palipotulia nina maongezi naye marefu, kwanza akaogopa akidhani huenda nimewasiliana na mume wake, nikamtoa hofu kwa kumwambia kuwa sina hata namba yake huyo jamaa basi akasema tukutane mchana mahali fulani pametulia.
Mchana nikawahi eneo hilo nikaagiza bia yangu nikawa nashusha mdogo mdogo(huu mji wetu watu wanakunywa tu tangu asubuhi kama vile hakuna ile sheria). Baada ya muda akaja akiwa kavaa vizuri sana kwa style ambazo tukiwa wapenzi nilikuwa napenda avae namna hiyo!! Kufika tu akawa anaona aibu kuongea hata salamu yenyewe katoa kwa kuangalia chini, nikaona nimuagizie nayeye Castle lite ili awake kidogo maana ni kichwa panzi ila anapenda kuonekana shujaa kwenye mambo mengi. Basi tukawa tunaendelea na maongezi ya kawaida kabisaa bila lile suala kuligusia, ikafika muda nikaona aibu zimeanza mtoka akaanza kuongelea mambo ya ndoa yake, na alipokuwa anaongea anaonekana kabisa kama anatua mzigo fulani mzito moyoni mwake, na kumbuka hapo mimi hata sijamuambia kuwa nimemuitia maongezi gani!!! Alianza kwa kunitaja jina langu, halaf akasema " yaani ningejua ningesikiliza hata maneno ya marafiki zangu kuhusu John, sijui alinifumba nini nikawa kipofu kabisa nisione lolote nikatamani tu kuitwa mke wake" baada ya hapo akafunguka sasa!!!!!! Kwa kwel mambo aliyonisimulia nilihisi ananidanganya, nikawa namkatalia kuwa anamsingizia mumewe, akachukua simu yake na kuanza kunionesha sms za mume wake, na evidence zingine kwa kweli nilichoka! Sometimes na sisi wanaume tunachangia 100% wanawake kucheat nje ya ndoa. Mambo hasa aliyonisimulia mpaka yamefikia yeye kuanza kutamani kuwa na mimi upya ni;
1: mwanaume anajali sana pesa kuliko utu au thamani ya mke mwenyewe, anaweza mnunulia hata bangili bahat mbaya ikipotea bas ni kipigo na mwisho wa siku anakuwa anamkemea kwamba anajua kainunua kwa bei gani? ( na anasema mume wake anajua kwel kupiga, kitu kidogo tu basi ni mrahisi kurusha kofi kama sio ngumi)
2: hataki afanye kazi, anataka awe anakaa tu nyumbani(huyu dada ana Diploma ya nursing)
3: jamaa ana wanawake kibao nje ambao inafika mahali had anakuwa anawatambua, ila cha ajabu ni kwamba hata wakati anaolewa naye alikuwa anajua kuwa ana wapenzi nje(hapa sikumuelewa na nilimshangaa sana kwa kwel)
4: Hapa ndo alinichekesha, kwamba mume wake anaweza kaa hata mwez mzma hajamgusa kabisaaa, na bado hana muda hata wa kuongea nae vzur, yeye akiamka ni kazini tu na mambo mengne, ila akiwa na hitaji la pesa anapewa kiasi anachotaka ila ajue jamaa hatasahau hyo pesa alompa!
5: Wivu ulopitiliza, anataka muda wote awe nyumbani, asiwe na marafiki wa kike wa ajabu ajabu, hataki akasuke salon ikitokea bas ni shingo upande.
6: Attention, na affection zile. Mwanaume hayupo romantic hata kidogo, hajui mke anataka nini kwa sasa, zaman anasema alikuwa anajaribu kumuambia ila mume anamjibu kuwa ana mambo ya kitoto
Evidence alizonionesha kwenye cm yake ni pamoja na sms ambazo yeye anamlalamikia kwanini hampi haki yake na jamaa anajibu kwamba mwanamke huyo anapenda sana ngono kuliko kitu chochote, na mambo mengne mengi ambayo siwezi yaandika humu yote!
Baada ya hapo, jambo nililomshauri ni aongee nae hali halisi na amueleze madhara yanayoweza tokea kama hatojirekebisha, pia amuambie wazi kuwa kwa mume wake kufanga hvyo kunahatarisha ndoa yake ikiwemo kuvunjika kabisa.
Akifanya hvyo na kama hakuna mabadiliko basi ahusishe viongozi wa dini au wazazi!
Mrejesho huu nimeona niulete humu kwa ajili yetu wanaume, ingawa na wanawake pia, ila kwa case kama hii tunaona kabisa nani ni Victim hapo!