Lager
JF-Expert Member
- Mar 4, 2019
- 389
- 1,071
Niliamua kumkataa na kutokutaka asije gheto ili kuomba misamaha yake ya kitandani!, Jambo lililodumu kwa wiki mbili tu wakati nilijua forever.
Mara hii baada ya kuona nimeshikilia msimamo kwa muda mrefu akaamua isiwe tabu akaja gheto kwa lazima lakini hakufanikiwa kuingia maana angeingia tu tayari ningempa msamaha.
Nje na yote jamani dunia hadaa walimwengu shujaa!, Juzi si nikaenda bar kujipongeza kwa kumuacha Grace ile nimekunywa za kutosha nikachukua simu nikampigia ili nimuage nifute na namba yake, kupiga kapokea akiwa na sauti ya huzuni huku mimi nikichekelea kama mshindi wa tatu mzuka tayari na alcohol kadhaa kichwani.
Ktk maongezi nikawa naongea kwa nguvu mpaka mwenye bar akanifukuza nikarudi gheto kusema kweli sikumbuki niliongea nini na Grace isipokuwa naamka asubuhi namuona ubavuni kwangu! Sielewi nani alitupatanisha na nani alimfungulia mlango nachokumbuka neno lake la mwisho kulisema lilikuwa ni neno "TAMU" na sikumbuki alilisema tukiwa kitandani au simuni.
Sasa mara hii najikuta nina vitu viwili vya kupangua ni ama nimuache Grace au pombe maana hivyo vyote viwili nikiacha kimoja, kingine kinamrejesha mwenzake😢
Pia soma>> Grace usije tena gheto
Mara hii baada ya kuona nimeshikilia msimamo kwa muda mrefu akaamua isiwe tabu akaja gheto kwa lazima lakini hakufanikiwa kuingia maana angeingia tu tayari ningempa msamaha.
Nje na yote jamani dunia hadaa walimwengu shujaa!, Juzi si nikaenda bar kujipongeza kwa kumuacha Grace ile nimekunywa za kutosha nikachukua simu nikampigia ili nimuage nifute na namba yake, kupiga kapokea akiwa na sauti ya huzuni huku mimi nikichekelea kama mshindi wa tatu mzuka tayari na alcohol kadhaa kichwani.
Ktk maongezi nikawa naongea kwa nguvu mpaka mwenye bar akanifukuza nikarudi gheto kusema kweli sikumbuki niliongea nini na Grace isipokuwa naamka asubuhi namuona ubavuni kwangu! Sielewi nani alitupatanisha na nani alimfungulia mlango nachokumbuka neno lake la mwisho kulisema lilikuwa ni neno "TAMU" na sikumbuki alilisema tukiwa kitandani au simuni.
Sasa mara hii najikuta nina vitu viwili vya kupangua ni ama nimuache Grace au pombe maana hivyo vyote viwili nikiacha kimoja, kingine kinamrejesha mwenzake😢
Pia soma>> Grace usije tena gheto