Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbona Masanja analima Mpunga UBARUKU MBARALI na anapata magunia ya kutosha mpaka ananunua X6 ya milioni 180 kutokana na kilimo cha mpunga? Nyie mnakwama wapi?
Kilimo ni mtaji, na hicho ndio kinamtofautisha Masanja na wengine. Hata mimi nikipewa 50mil nikalime ni obvious nitatoboa.
Nimeona naye kigwangala analima mpunga.Kilimo ni mtaji, na hicho ndio kinamtofautisha Masanja na wengine. Hata mimi nikipewa 50mil nikalime ni obvious nitatoboa.
Kwa hesabu zako wastani wa kulima kwa heka ni kama TZS 600,000 kwa gunia 10 za debe 7 ambazo kila debe ni kama kg20 so ni sawa ni sawa na tani 1 na nusu.Kwa hivyo wastani wa kulima ni laki 4 kwa tani moja ?(KILIMO CHA KWENYE MAKARATASI) Je naweza tumia hii kama makadirio au muongozo?Asante, inategemeana na aina ya mbegu uliyopanda, Kuna mbegu zinaiva ndani ya siku 90 na 120 lkn pia Hali ya hewa inaweza kusababisha mpunga wako ukachelewa kukomaa, Kama ukilima mbegu moj wanaipenda sana hapa bahi, inaitwa NGANYARO, yenyewe huwa inarefuk tu maji yanapozidi kuwepo, inaweza fikia hata fut 5 kabisa, ila punde maji yanapokauka inabadilika rangi na kukomaa ndani ya siku chcahe tu.
Gharama: kiukweli kilimo Cha mpunga kina gharama lakni mavuno yake yanafidia Mara dufu gharama uliyotumia. Mfano mm nilikodi 150k@heka moj,
Kulima na trekta 60k@heka
Kupandikza mbegu 70@heka
KUVUNA:
Mtu wa kuamia ndge20@mwez (mahitaji yote juu yako)
KUVUNA na kupiga 4000@gania
Usafir toka mbugani mpka mashineni au stoo bahi 3500@gunia moj.
Nadhani hapo umepata picha
Ulitumia gharama kias gan kulimaNimepitia maswali na majibu humu nimeona bora kilimo cha nyanya mara pengine kuliko mpunga. Sijawahi kulima mpunga, ila mwaka jana nilijaribisha kulima nyanya kwa eneo km nusu eka. Nikapata tenga 142. Niliuza kwa bei tatu. Nilianza kwa sh 60000, baadae ikashuka kidogo 55000, bei ya mwisho nikauza 45000. Mwisho nikitoa gharama zote nilibakiwa na mil5+
1200,000 hiviUlitumia gharama kias gan kulima
Nimejiapiza sitalima tena kilimo cha muda mfupi,mimi ntawekeza kwenye kulima miti wajukuu wangu watapiga hela balaa.
Usiniambie hutaki kukaa dukani sasa iviHongera mkuu.
Kilimo cha mpunga kinachukua mda gani hadi kuvuna?
Na gharama zake je?
P ana shamba la maparachichi mbeya ..Usiniambie hutaki kukaa dukani sasa ivi
Daah yaani mkuu kigwangala anatisha.Nimeona naye kigwangala analima mpunga.
Asant sana mkuuKaribu mkuu
Yes mitaji mikubwa pia ana wasiwasi hata akipoteza mil 100 kwasababu baada ya miezi mi5 kashaipata tena ila sie hatuwezi kuwekeza hata mil 5 kwenye kilimo maana ukipoteza kuipata tena ni issue.Daah yaani mkuu kigwangala anatisha.
Niliona na ana ng'ombe pia anapiga mnada.
Wenzetu wanafaulu coz wana mitaji ya kutosha aisee.