Mrejesho: Kilimo cha mpunga Bahi

cha1509

JF-Expert Member
Jul 6, 2018
258
402
Jembe halimtupi mkulima. Huu msemo umetamalaki sana hapa kwetu Tz, lakini mara kadhaa huwa unakuwaga na ukweli ndani yake.

Msimu wa 2018/19 nilijaribu kulima mpunga Bahi hekari 5, japo nilikodi hekari 12 na kuzitifua zote kwa trekta, ila nikakumbana na ukame wakati napandikiza. Nilifanikiwa kupandikiza mashamba matano tu maji yakawa yameisha. Hivyo, nikawa sina jinsi.

Si haba katika heka hizo tano nimeweza kurudisha mbegu, nimepata magunia 54, yenye ujazo wa debe saba saba (7,7). Kiukweli nashukuru sana Mungu kwan mwaka huu ulikuwa na changamoto sana. Wengine hawakuweza kuvuna kabisa hata lita moja.

Nimezidi kujifunza mengi katika kilimo, ndugu zangu. Wakati mimi nimepata vigunia 54, kuna mtu kapata migunia 400, na mwingine migunia 600, hivyo ukiwa kupanda uhakika wa kupiga pesa kupitia kilimo INAWEZEKANA.

Nimeona si haba niwaletee mrejesho wananzengo kwani kuna baadhi ya wanaJF walitaka mrejesho mara baada ya kutoka shambani.

Picha hizi hapa

IMG_20190703_161625_6.jpeg
IMG_20190629_081522_7.jpeg
IMG_20190629_081945_2.jpeg
IMG_20190629_082732_4.jpeg
IMG_20190629_082722_2.jpeg
IMG_20190704_180909_2.jpeg
IMG_20190704_181016_0.jpeg
IMG_20190626_111858_6.jpeg
IMG_20190629_121431_6.jpeg
IMG_20190630_130850_9.jpeg
 
Hongera mkuu.
Kilimo cha mpunga kinachukua mda gani hadi kuvuna?
Na gharama zake je?
Asante, inategemeana na aina ya mbegu uliyopanda, Kuna mbegu zinaiva ndani ya siku 90 na 120 lkn pia Hali ya hewa inaweza kusababisha mpunga wako ukachelewa kukomaa, Kama ukilima mbegu moj wanaipenda sana hapa bahi, inaitwa NGANYARO, yenyewe huwa inarefuk tu maji yanapozidi kuwepo, inaweza fikia hata fut 5 kabisa, ila punde maji yanapokauka inabadilika rangi na kukomaa ndani ya siku chcahe tu.

Gharama: kiukweli kilimo Cha mpunga kina gharama lakni mavuno yake yanafidia Mara dufu gharama uliyotumia. Mfano mm nilikodi 150k@heka moj,
Kulima na trekta 60k@heka
Kupandikza mbegu 70@heka

KUVUNA:
Mtu wa kuamia ndge20@mwez (mahitaji yote juu yako)
KUVUNA na kupiga 4000@gania
Usafir toka mbugani mpka mashineni au stoo bahi 3500@gunia moj.

Nadhani hapo umepata picha
 
Hongera mkuu, bahi sehemu gani
Mm sio mwenyeji wa bahi, ila nilikodi mashamba mbugani tu chifu, achana na huku barabarani unaingia ndani zaidi mwendo wa masaa lisaa moj kwa pikipki Tena unatembea Kama lisaa moj na nusu ndiko unafika
 
Safi sana kwa kupambana unaweza sema ni sehemu ipi ni bahi hi ya barabarani
Hpn mkuu, km wewe n mwenyeji huko kun sehem wanapaitaga forozan wenyeji wa huko, ndiko ila mbele yake Sasa ndiko nilikokuwa nimejikita mkubwa
 
Mkuu una bahati Sana. Mimi nimelima ekari 3 nimepata gunia 4 tu.
Tena Bora yako Kuna wengine hawajapata kabisa, ndio maana nimesema hap awali, kun wengine hawajarudisha hata mbegu, ila amini nakuambia mpunga n moj ya zao lenye roho ngum sana.

Maji ya mwisho nilipandikizia mwez wa pili yakaisha baadh ya mashamba yangu nikashindwa kumalizia ,. Tena nilikata tamaa, mvua za mwez wa tano zikafufua matumaini yangu mkubwa.

Sehem km naguna, uhelela nadhani na chikuyu mapema sana walichoma Moto mashamba Yao. Hkn walichoambulia
 
Jembe halimtupi mkulima , huu msemo umetamalaki sana hapa kwetu tz, lakini Mara kadhaa huwa unakuwaga na ukweli ndani yake.

Msimu wa 2018/19 nilijaribu kulima mpunga bahi hekari 5, japo nilikodi hekari 12 na kuzitifua zote kwa trekta, ila nikakumbana na ukame wakat napandikiza. Nilifanikiwa kuoandikiza mashamba matano tu, maji yakawa yameisha, hivyo nikawa Sina jinsi.

Si haba katika heka hizo tano nimeweza kurudisha mbegu, nimepata magunia 54, yenye ujazo wa debe saba Saba 7,7. Kiukweli nashukuru San mungu Kwan mwaka huu ulikuwa na changamoto sana. Wngine hawakuweza KUVUNA kabisa hata Lita moja.

Nimezidi kunifunza mengi katika kilimo ndugu zangu, wakati mm nimepata vigunia 54, Kuna mtu kapata migunia 400, na mwingine migunia 600, hivyo ukiwa kupanda uhakika wa kupiga pesa kupitia kilimo INAWEZEKANA.

Nimeona si haba niwaletee mrejesho wananzengo kwani Kuna baadhi ya wanajf walitaka mrejesho Mara baada ya kutoka shambani.

Picha hizi hapa.
View attachment 1148431View attachment 1148432View attachment 1148433View attachment 1148434View attachment 1148435View attachment 1148436View attachment 1148437View attachment 1148438View attachment 1148440View attachment 1148444
Hongera, lakini huwa naona wafanyabiashara wa mazao ndo wanatajirika sijawahi kuona mkulima akitajirika.
 
Hongera, lakini huwa naona wafanyabiashara wa mazao ndo wanatajirika sijawahi kuona mkulima akitajirika.
Siwez kupingana na hoja yako mkuu, kwa kuwa sijafanya utafiti, lakin ukima kwa mazoea utaendelea kulalamika Kila kukicha, mfano gania saiv la mpunga lenye ujazo wa debe 6, linaizwa 55k-65k lkin ukikoboa mashineni gunia Hilo Hilo unauza kwa 84k na mashine ziko karibu hapo na napo panahitaji degree kuelewa? Halafu chief wote tukiwa matajiri vibarua tutatoa wapi? Maisha n kutegemean tu boss
 
32 Reactions
Reply
Back
Top Bottom