Mramba auza hoteli yake?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
Kuna habari za ndani sana zinazosema kuwa akitarajia muda si mrefu kuwekwa kizimbani aliyekuwa Waziri wa Viwanda Bw. Basil Mramba ameamua kuachilia umiliki wa hoteli yake ya Kibo Palace iliyoko Arusha karibu na cliniki ya AICC. Hili ni mojawapo ya maamuzu ambayo Bw. Mramba ameamua kufanya hasa baada ya uchunguzi wa chini chini ulionesha kuwa kutokana na nafasi yake aliweza kutumia madaraka yake vibaya kwa kujinufaisha.

Kuna dalili pia miradi yake mingine ambayo ameiandikisha kwa majina ya watu wengine ameanza taratibu kuiachilia ili kuharibu/kuficha ushahidi wa yeye au watu wake wa karibu kunufaika.

Vyanzo hivyo vilivyojikita katika kuta mbalimbali za jamhuri yetu vinaonesha pia kuwa Bw. Mramba ambaye ni mzazi mwenza wa mke wa Rais Mkapa ameshiriki kwa kiasi kikubwa katika kuhakikisha biashara za mama huyo zinafanikiwa na zinajikita katika maeneo mbalimbali. Bila ya Mramba inasemwa mama Mkapa asingeweza kujikita kwenye biashara zake.

Endapo Bw. Mramba atasimama kizimbani kama inavyotarajiwa atakuwa ni mtu mwingine aliyewahi kushika nafasi ya Uwaziri katika Muungano kusimamishwa Kizimbani. Kabla yake Waziri Nalaila Kiula alisimamishwa kizimbani kwa makosa ya ubadhirifu lakini baadaye aliweza kushinda rufaa yake na kuachiliwa huru.

Vyanzo hivyo vinaonesha pia kuwa siyo Mramba tu ambaye ameanza kusafisha sahani yake bali pia viongozi na mawaziri (na waliowahi kuwa mawaziri) ambao wameanza kuachilia miradi yao yenye "utata" hasa baada ya kugundulika kuwa Rais Kikwete hatozuia au kuingilia kati uchunguzi wowote dhidi yao au kujaribu kuwakingia kifua kama walivyotarajiwa.
 
Kuna uwezekano mkubwa kwamba JK amewaachia watuhumiwa wote wa ufisadi waendelee kuwa huru ili waharibu ushahidi dhidi yao na hata watakapofikishwa mahakamani, kama itatokea, basi hakuna ushahidi dhidi yao. Bongo yetu hiyo! lolote linawezekana kama una pochi la kifisadi.
 
Endapo Bw. Mramba atasimama kizimbani kama inavyotarajiwa atakuwa ni waziri wa pili wa serikali ya Mkapa kusimamishwa Kizimbani. Kabla yake Waziri Nalaila Kiula alisimamishwa kizimbani kwa makosa ya uhalifu lakini baadaye aliweza kushinda rufaa yake na kuachiliwa huru.

.

Sahihisho ndugu Mwanakijiji. Nalaila Lazaro Kiula hajawahi kuwa waziri katika serikali ya Mkapa. Hadi sasa hakuna waziri wa serikali ya Mkapa aliyesimamishwa kizimbani. Nalaila Kiula alikuwa waziri wa Ujenzi katika serikali ya Mzee Mwinyi.
 
Vyanzo hivyo vinaonesha pia kuwa siyo Mramba tu ambaye ameanza kusafisha sahani yake bali pia viongozi na mawaziri (na waliowahi kuwa mawaziri) ambao wameanza kuachilia miradi yao yenye "utata" hasa baada ya kugundulika kuwa Rais Kikwete hatozuia au kuingilia kati uchunguzi wowote dhidi yao au kujaribu kuwakingia kifua kama walivyotarajiwa.

Mkuu MMJ,

Heshima mbele, maneno yako yako very clear na ujumbe unaeleweka, inaelekea mafisadi wana wakati mgumu sana, maana sasa tunawamulika kila kona,

Mramba, anaelekea kwenye pingu najua kuwa ni very soon, halafu more zaidi nasikia wabunge wameamua kutuchangisha wananchi kwenye kikako kijacho cha bajeti ili tuwarudishie Mkapa na wenziwe zile shilingi millioni 70 walizolipa kule Kiwira, kumbuka kuwa Mramba naye yupo kule, iwapo serikali haitachukua hatua nzito dhidi yao,

Again, ahsante kwa hizi dataz nzito! Kwa sababu the big picture iko very clear!
 
Sahihisho ndugu Mwanakijiji. Nalaila Lazaro Kiula hajawahi kuwa waziri katika serikali ya Mkapa. Hadi sasa hakuna waziri wa serikali ya Mkapa aliyesimamishwa kizimbani. Nalaila Kiula alikuwa waziri wa Ujenzi katika serikali ya Mzee Mwinyi.

asante sana.. duh.. yaani muda umepita hivyo?
 
Things fall apart......... No longer at easy

Nitapata furaha isiyo na kifani siku nitakaposikia one of these or even all of them: Mramba, Yona, Karamagi, Lowassa, Rostam, Chenge na baba yao Mkapa are really prosecuted. I pray this dream to come true, sooner than later! Mungu Mkubwa!!
 
After more than two yrs in power, i have reached conclusive uamuzi kwa jk hana uwezo wa kufanya la maana kutuokoa na madhila haya. Kama aTaonekana kufanya kitu fulani, basi kitakuwa na malengo fulani binafsi yalijificha ambayo hatutayajua kwa wakati huo
 
hii vibweka vya wakubwa mod !!

au na mie nilete "facts" za mbowe kuajiri wasauzi kwenye hoteli yake (aliyoshindwa kumalizia mkopo)?.... where is this guy's patriotism ? mkopo kapewa tanzania, kashindwa kulipa, then anaajiri wasauzi ?
 
kada mpinzani kmaa unatakak uandika ya mbowe andika hujakatazwa na mtu!

mie namhesabia saa na dakika JK hadi kututimizia ahadi alizozitoa wakati wa kampeni.

hivi tuliambiwa mabilionea wangapi vile? au ndo hawa kina mramba tunawaona?
 
......Na serikali yetu ikiwa bado imeendelea kulala usingizi mzito wa njozi... inakoroma kabisa
 
Mwanakijiji Wengi Wanaofikiriwa Kwamba Wanaachia Mali Zao Sio Kweli , Wengi Wanabadili Majina Na Miliki Kisha Wanawapa Ndugu Na Jamaa Zao Kuziendeleza Wengine Wanatafuta Wageni Haswa Kutoka India Na Nchi Za Ulaya Ya Mashariki Kuja Kuziendeleza Kujifanya Ni Wawekezaji == Tatizo Wewe Hauko Tanzania Upate Experiance Hii Ya Makampuni Ya Wakubwa Yanayoongozwa Na Watu Kutoka Asia Kwa Majina Ya Wawekezaji Lakini Wamewekwa Pale Kama Mapambo Tu Wenyewe Ni Wale Wale Wameweka Miguuu Juu
 
Ile mkuu maisha bora kwa kila MT ilikuwa kwa ajili ya hao wenye POWER sio ss walalahoi...si unaona wao wanavyo neemeka mafisadi wanatanua kamakawa....kwa JK mm naona atachemka...
 
......Na serikali yetu ikiwa bado imeendelea kulala usingizi mzito wa njozi... inakoroma kabisa

Tatizo wanajua waTZ wote wamelala ndo maana utasikia wananchi inabidi waelimishwe hii mpaka lini??Ndo maana wao wanapata miaya ya kujineemesha kama kawa.
 
hii vibweka vya wakubwa mod !!

au na mie nilete "facts" za mbowe kuajiri wasauzi kwenye hoteli yake (aliyoshindwa kumalizia mkopo)?.... where is this guy's patriotism ? mkopo kapewa tanzania, kashindwa kulipa, then anaajiri wasauzi ?

I have always thought that Jf is here to critisize everyone driving this country to the mud. sijawahi kufikiri kwamba tuko hapa kufanya upambe au kushabikia au kusema mazuri juu ya mtu wakati amefanya mabaya. kama mtu amefanya madudu yasemwe hapa na sio kutishiana sisi kwa sisi tena.
 
Kwanza niseme kabisa kuwa niliimiss sana JF na nikadhani kuna mkono wa 'mtu'. But now najisikia vizuri sana kurudi katika dunia.

Mafisadi tunapowaongelea tunapaswa tujue kuwa mbali na kuwa wao ni kundi lakini pia wako mmmoja mmoja na hivyo kuchanganya mada haipendezi, tunapomwonglea Mramba jua kabisa hatumwongelei Chenge, hawa wote wana nafasi zao na tunawajadilimmoja mmoja ili kutoa kitu halisi kwa kila mtu, sweeping generalization haina nafasa hapa JF.

Mramba tunatarajia auze vyote na apelekwe mahakamani



Walinunua kwa siri, watauza usiku na mchana itawaonesha haki
 
hii vibweka vya wakubwa mod !!

au na mie nilete "facts" za mbowe kuajiri wasauzi kwenye hoteli yake (aliyoshindwa kumalizia mkopo)?.... where is this guy's patriotism ? mkopo kapewa tanzania, kashindwa kulipa, then anaajiri wasauzi ?

Ningekushauri usome thread kwanza ndipo uanze kusanuka. Hapa anaongelewa Mramba na miradi yake, wewe unaingiza hiyo yako ya Mbowe. Una zaidi ya post 3,500 kinakushinda nini kuanzisha thread yako nyingine inayomhusu huyo Mbowe. Ina maana hizo posts zote ulizoweka hapa JF ulikuwa unaomba ruhusa kabla ya kuzi-post?
 
Kada mbona unakurupuka?

Shy,sasa kumbe hayo yote unajua halafu bado una-side na mafisadi?

Btw,Safi sana kama mramba atashtakiwa,na jeuri yake atakoma
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom