Mradi wa Ununuzi wa Ndege ni "Critical Move" ya "Hapa Kazi Tu": Wacha Punda Afe Mzigo ufike

X-bar

JF-Expert Member
Mar 20, 2019
1,002
1,146
Nilichojifunza kutokana na maandamano ya vijana wa ccm kwenye ubalozi wa Sauz ni

1. Mradi wa "Ndege za Magufuli" ndio kielelezo nambari moja kinachotumiwa na wana ccm na serikali ya awamu ya tano katika kuonesha mafanikio ya uthubutu na uchapaji kazi wa Jiwe (hapa kazi tu).

2. Ndege hizi ndio "jeuri" ya Jiwe dhidi ya watangulizi wake na hutumika "kuwachambia" wakosoaji kwa kuwaonesha kuwa "nchi hii ni tajiri" na tuna uwezo wa kununua "equipment" hizi kwa fedha taslim.

3. Mradi huu umegeuka kama mpira katika mchezo wa kabumbu unaogombewa na timu mbili pinzani kwa maana ya serikali/ccm dhidi ya wakosoaji na kila upande unataka kuibuka mshindi.

4. Hivyo basi, serikali ya Jiwe iko tayari kutumia gharama yoyote kuhakikisha mradi huu unasonga mbele hata husipoleta faida ili tu kuthibitisha kwamba wanaokosoa mradi huu hawako sawa sawa.

5. Sasa basi, zinapotokea changamoto katika mradi huu kama vile kuharibika kwa ndege, kushindwa kuruka masafa ya kimataifa, uchache wa abiria au kushikiliwa na wadeni wetu kama ilivyotokea kule Canada na hii ya Sauz, inachukuliwa kama ni kufeli kwa serikali ya Jiwe na ushindi kwa wakosoaji.

6. Kwa kuwa mradi huu ni "critical move" kwa serikali ya awamu ya tano, changamoto zinapotokea serikali huwa "inapata tabu sana" dhidi ya wakosoaji, bali hutafutwa "mchawi" kuwa ndiye anayekwamisha. Kule Canada Tundu Lisu ndiye aliyechochea kukamatwa kwa ndege na hii ya Sauz tunaambiwa Mtanzania aliyefukuzwa kazi UD ndiye aliyeongoza jopo la mawakili wa ukoo wa Steyn katika madai yao dhidi ya serikali.

7. Kinyume chake, mafanikio yoyote yanayopatikana katika mradi huu yanakuwa ni ya Jiwe na huwa "highly promoted" dhidi ya wakosoaji.

Binafsi natambua mtazamo wa Rais Magufuli na nia njema aliyonayo juu ya kuifanya Tanzania yetu "Great Nation".

Rais Magufuli anaumia sana kuona nchi yetu pamoja na utajiri tulionao bado tunapitwa na nchi duni kama Ruanda, Ethiopia na Kenya ambazo zina mashirika makubwa ya ndege na hupeperusha bendera zake (ndege) kimataifa. Kwanini isiwe na Tanzania nayo? Ukweli ni kwamba sisi watanzania tulikuwa tukikosoa serikali zilizopita kuwa zilikosa maarifa ya kulinyanyua shirika letu la ndege. Tulikuwa tunasema tunashirika la ndege lisilo na ndege bali ni wafanyakazi tu. Swali la msingi hapa ni je Magufuli kama Rais wa awamu ya Sasa, hakupaswa kufanya chochote katika kuliendeleza shirika letu? Je, Kwanini kuna watu wanakosoa mradi wa ATCL? Je, wazalendo ni wale wanaosapoti au wanaokosoa? Je, kuna haja au tuachane na mradi huu?

Katika kujibu maswali haya napenda kuishauri serikali ya awamu ya tano kuwa kuna sehemu inakosea katika kutekeleza miradi ya maendeleo. Kwanza kabisa ieleweke hakuna Rais aliyeongoza nchi hii ambaye si mzalendo. Hakuna Rais ambaye hakuwa na nia njema au alipenda kuona ATCL inakufa. Wote walijitahidi kuiruzuku ATCL lakini changamoto za ATCL ni kubwa mno kiasi kwamba inatakiwa tuchague kuendeleza shirika au tupate hasara. Rais Kikwete alikuwa anasikitika sana kuhusu mwenendo wa shirika hili kuipa hasara serikali kwa kushindwa kujiendeleza licha ya jitihada za serikali kulisaidia shirika.

Ninaposema kuna sehemu sarikali ya awamu hii inakosea licha ya nia njema iliyonayo maana yangu ni moja tu, serikali hii inapenda sifa. Hulka ya sifa hupelekea serikali kushindwa kuona na kupima ugumu wa kutatua changamoto za kuiendeleza ATCL kwa maana ya madeni.

Gharama ya kuwa na ATCL ya "kimataifa" ni kubwa kuliko faida yake kiuchumi. Labda ndioma hesabu zake zinahifadhiwa ikulu na hazikaguliwi na CAG. Bali ni kujenga sifa tu kwamba Tanzania tuna shirika la ndege kama nchi zingine za jirani.

Lakini tunapoamua kutumia fedha taslim nyingi kununua midege hii wakati serikali na shirika lenyewe lina madeni na vikwazo kibao katika anga za kimataifa sijui tuite nini hii?

Kwa kumalizia, changamoto hizi za ndege za ATCL ni matokeo ya kukurupuka kuliendeleza shirika bila kutathmini changamoto zake ambazo viongozi wa awamu za nyuma waliziona. Lakini makada wa CCM wanapoandamana kwenye ubalozi wa Sauz kwa kisingizio cha kuonesha uzalendo kwa mali za nchi ni upuuzi. Wala wasijaribu kutuonesha kuwa Srikali ya Afrika Kusini ndiyo walioishikilia ndege. Na ikiwa serikali ya Sauz imeshindwa kumsaidia Jiwe kwa kuingilia maamuzi ya mahakama ya nchi hiyo, vijana wa ccm watambue kuwa mfumo wetu wa kiutawala na mambo ya sheria hauko sawa na ule wa Sauz. Serikali haipaswi kuingilia maamuzi ya mahakama kama ilivyo hapa Tanzania. Kenya walisaidia kurudisha dhahabu iliyoibiwa Tanzania. Je, wanataka kutuambia akina Steyn wapeiba ndege yetu serikali ya Sauz ifanye kama ile ya kenya kuturudishia ndege?
 
Uchambuzi sahihi, na ndiyo ukweli wenyewe. Lakini wapo wanaoamua kutotumia akili watakupinga.

Nchi haijengwi kwa kutafuta sifa za kijinga. Sifa za kijinga zinaligharimu Taifa.

1) Ni vyema kuwa na sheria na sera nzuri katika uwekezaji wa sekta ya madini, lakini kwa vile tulifanya kwa kutafuta sifa, tumeangukia pua

2) Viwanda ni muhimu sana kwenye uchumi wa Taifa, lakini kwa vile tunafanya kwa kutafuta sifa, tumeangukia pua

3) Japo usafiri wa anga ni muhimu lakini uimaridhaji wake kwa vile umeegemea zaidi kutafuta sifa, tutaangukia pua

Uchumi ni Sayansi, na ujenzi wake unahitaji utulivu wa akili, utafiti, mipango sawia, mbinu sahihi, umoja wenye ownership n.k. Hatuwezi kujenga uchumi wa nchi kwa kuwategemea watu ambao vichwa vyao wakati wote vimekaa kuwaza ni nani CCM, nani CHADEMA, ACT, n.k. Siasa za CCM zimefubaza utambuzi kwa viongozi wengi kiasi kufanya vitendo vya kulirudisha nyuma Taifa badala ya kulipeleka mbele.

Viongozi wa namna ya akina Bashite, ambao kwao kila kitu ni CCM na JPM (tena kwa kutoa sifa za kinafiki), badala ya Taifa, kamwe hawawezi kulisaidia Taifa.

Taifa linahitaji watu wenye akili kubwa, akili zisizo za kukaririri wala za kujipendekeza kama za akina Kibudu, kuweza kuja na nadharia sahihi za kulisaidia Taifa kwenda mbele kwa kasi. Na zaidi itategemea uwezo wa kuufanya umma uwe pamoja katika mipango mikubwa ya Taifa.

Huwezi kujenga nchi kwa juendekeza ubaguzi wa aina yoyote ile.
 
Hivi ukijipa muda ukasoma ukaelewa kilichoandikwa itakuwaje mkuu? Kwann mbele ya macho yenu huwa ni kupambana tu na yoyote anaetofautiana mawazo na nyie?

Sijui kingereza tu Ila ningekumbuka lile neno alilisema profesa kabidi kuhusu watu wasiotaka kujifunua vichwa vyao kuingiza kitu kipya, Ni kuwa mnaamini yoyote anaeongea kinyume na nyinyi sio mzelendo (kinyume na Jiwe in fact).

Sasa zaidi ya uchambuzi kama huu ulitaka nini zaidi kwa mfano. Msipobadilika na kukubali kuruhusu kupokea mawazo ya watu wengine katika kujifunza Hali itakuwa mbaya Sana upande wenu na upande wa wengine.
Wenzako wanapata mgao ktk kwa Muzungu ndo maana wanamtetea, weye wapata nini labda?
 
Wenzako wanapata mgao ktk kwa Muzungu ndo maana wanamtetea, weye wapata nini labda?
Mimi nasimamia haki kama msumeno unavyokata pande zote.so jiwe alitakadhulumu mkulima mkulima ni level nyingine jiwe anaendelea kua mshamba
 
Mimi nasimamia haki kama msumeno unavyokata pande zote.so jiwe alitakadhulumu mkulima mkulima ni level nyingine jiwe anaendelea kua mshamba


Unasimamia haki ya Muzungu? Kuna Watanzania wangapi wanadai haki huwasimamii? Kuna wati hawalipwa mafao yao hadi wanakufa mbona hamuwapiganii? Ee Mr Haki?
 
Profesa alisema "impevious brain"
Hivi ukijipa muda ukasoma ukaelewa kilichoandikwa itakuwaje mkuu? Kwann mbele ya macho yenu huwa ni kupambana tu na yoyote anaetofautiana mawazo na nyie?

Sijui kingereza tu Ila ningekumbuka lile neno alilisema profesa kabidi kuhusu watu wasiotaka kujifunua vichwa vyao kuingiza kitu kipya, Ni kuwa mnaamini yoyote anaeongea kinyume na nyinyi sio mzelendo (kinyume na Jiwe in fact).

Sasa zaidi ya uchambuzi kama huu ulitaka nini zaidi kwa mfano. Msipobadilika na kukubali kuruhusu kupokea mawazo ya watu wengine katika kujifunza Hali itakuwa mbaya Sana upande wenu na upande wa wengine.
 
Unasimamia haki ya Muzungu? Kuna Watanzania wangapi wanadai haki huwasimamii? Kuna wati hawalipwa mafao yao hadi wanakufa mbona hamuwapiganii? Ee Mr Haki?
Hao inawapaswa uwapiganie wewe hapo unaetambua mkuu huo ndo mgawanyo wa majukumu maana angewapigania hao uliowasema wewe unadhani ungesema kitu gani? Au wewe unapigani uchama tu enh?
 
Nilichojifunza kutokana na maandamano ya vijana wa ccm kwenye ubalozi wa Sauz ni

1. Mradi wa "Ndege za Magufuli" ndio kielelezo nambari moja kinachotumiwa na wana ccm na serikali ya awamu ya tano katika kuonesha mafanikio ya uthubutu na uchapaji kazi wa Jiwe (hapa kazi tu).

2. Ndege hizi ndio "jeuri" ya Jiwe dhidi ya watangulizi wake na hutumika "kuwachambia" wakosoaji kwa kuwaonesha kuwa "nchi hii ni tajiri" na tuna uwezo wa kununua "equipment" hizi kwa fedha taslim.

3. Mradi huu umegeuka kama mpira katika mchezo wa kabumbu unaogombewa na timu mbili pinzani kwa maana ya serikali/ccm dhidi ya wakosoaji na kila upande unataka kuibuka mshindi.

4. Hivyo basi, serikali ya Jiwe iko tayari kutumia gharama yoyote kuhakikisha mradi huu unasonga mbele hata husipoleta faida ili tu kuthibitisha kwamba wanaokosoa mradi huu hawako sawa sawa.

5. Sasa basi, zinapotokea changamoto katika mradi huu kama vile kuharibika kwa ndege, kushindwa kuruka masafa ya kimataifa, uchache wa abiria au kushikiliwa na wadeni wetu kama ilivyotokea kule Canada na hii ya Sauz, inachukuliwa kama ni kufeli kwa serikali ya Jiwe na ushindi kwa wakosoaji.

6. Kwa kuwa mradi huu ni "critical move" kwa serikali ya awamu ya tano, changamoto zinapotokea serikali huwa "inapata tabu sana" dhidi ya wakosoaji, bali hutafutwa "mchawi" kuwa ndiye anayekwamisha. Kule Canada Tundu Lisu ndiye aliyechochea kukamatwa kwa ndege na hii ya Sauz tunaambiwa Mtanzania aliyefukuzwa kazi UD ndiye aliyeongoza jopo la mawakili wa ukoo wa Steyn katika madai yao dhidi ya serikali.

7. Kinyume chake, mafanikio yoyote yanayopatikana katika mradi huu yanakuwa ni ya Jiwe na huwa "highly promoted" dhidi ya wakosoaji.

Binafsi natambua mtazamo wa Rais Magufuli na nia njema aliyonayo juu ya kuifanya Tanzania yetu "Great Nation".

Rais Magufuli anaumia sana kuona nchi yetu pamoja na utajiri tulionao bado tunapitwa na nchi duni kama Ruanda, Ethiopia na Kenya ambazo zina mashirika makubwa ya ndege na hupeperusha bendera zake (ndege) kimataifa. Kwanini isiwe na Tanzania nayo? Ukweli ni kwamba sisi watanzania tulikuwa tukikosoa serikali zilizopita kuwa zilikosa maarifa ya kulinyanyua shirika letu la ndege. Tulikuwa tunasema tunashirika la ndege lisilo na ndege bali ni wafanyakazi tu. Swali la msingi hapa ni je Magufuli kama Rais wa awamu ya Sasa, hakupaswa kufanya chochote katika kuliendeleza shirika letu? Je, Kwanini kuna watu wanakosoa mradi wa ATCL? Je, wazalendo ni wale wanaosapoti au wanaokosoa? Je, kuna haja au tuachane na mradi huu?

Katika kujibu maswali haya napenda kuishauri serikali ya awamu ya tano kuwa kuna sehemu inakosea katika kutekeleza miradi ya maendeleo. Kwanza kabisa ieleweke hakuna Rais aliyeongoza nchi hii ambaye si mzalendo. Hakuna Rais ambaye hakuwa na nia njema au alipenda kuona ATCL inakufa. Wote walijitahidi kuiruzuku ATCL lakini changamoto za ATCL ni kubwa mno kiasi kwamba inatakiwa tuchague kuendeleza shirika au tupate hasara. Rais Kikwete alikuwa anasikitika sana kuhusu mwenendo wa shirika hili kuipa hasara serikali kwa kushindwa kujiendeleza licha ya jitihada za serikali kulisaidia shirika.

Ninaposema kuna sehemu sarikali ya awamu hii inakosea licha ya nia njema iliyonayo maana yangu ni moja tu, serikali hii inapenda sifa. Hulka ya sifa hupelekea serikali kushindwa kuona na kupima ugumu wa kutatua changamoto za kuiendeleza ATCL kwa maana ya madeni.

Gharama ya kuwa na ATCL ya "kimataifa" ni kubwa kuliko faida yake kiuchumi. Labda ndioma hesabu zake zinahifadhiwa ikulu na hazikaguliwi na CAG. Bali ni kujenga sifa tu kwamba Tanzania tuna shirika la ndege kama nchi zingine za jirani.

Lakini tunapoamua kutumia fedha taslim nyingi kununua midege hii wakati serikali na shirika lenyewe lina madeni na vikwazo kibao katika anga za kimataifa sijui tuite nini hii?

Kwa kumalizia, changamoto hizi za ndege za ATCL ni matokeo ya kukurupuka kuliendeleza shirika bila kutathmini changamoto zake ambazo viongozi wa awamu za nyuma waliziona. Lakini makada wa CCM wanapoandamana kwenye ubalozi wa Sauz kwa kisingizio cha kuonesha uzalendo kwa mali za nchi ni upuuzi. Wala wasijaribu kutuonesha kuwa Srikali ya Afrika Kusini ndiyo walioishikilia ndege. Na ikiwa serikali ya Sauz imeshindwa kumsaidia Jiwe kwa kuingilia maamuzi ya mahakama ya nchi hiyo, vijana wa ccm watambue kuwa mfumo wetu wa kiutawala na mambo ya sheria hauko sawa na ule wa Sauz. Serikali haipaswi kuingilia maamuzi ya mahakama kama ilivyo hapa Tanzania. Kenya walisaidia kurudisha dhahabu iliyoibiwa Tanzania. Je, wanataka kutuambia akina Steyn wapeiba ndege yetu serikali ya Sauz ifanye kama ile ya kenya kuturudishia ndege?
6K
 
Wenzako wanapata mgao ktk kwa Muzungu ndo maana wanamtetea, weye wapata nini labda?
Je, unakumbuka Rais Maguli aliwahi kuelezea wasiwasi wake juu ya ndege anazonunua kuwa akiondoka madarakani watakaoongoza nchi wanaweza kuziuza ndege hizo? Unadhani ni kwanini aliwaza hivyo? Na kwanini hakuhofia kwamba watakuja kungo'a mataluma ya SGR?
 
Back
Top Bottom