Mradi wa Mwendokasi Mbagala umekuwa kero kwa wananchi

Kinumbo

JF-Expert Member
Dec 8, 2019
2,742
4,931
Moja kwa moja kwenye dhumuni la mada hii, huu mradi wa mwendo kasi kutoka Kariakoo mpaka Mbagala umekuwa kero sana. Si asubuhi, mchana ama usiku ni kero mtindo mmoja, kero yenyewe ni kujitokeza foleni. Yaani huu mradi umefanya iwepo kamba ya maana si mchezo. Hivi hiyo kampuni ama serikali haioni huo usumbufu ili kutafuta njia mbadala.?

Foleni kuanzia pale uhasibu inakwenda mpaka kwa Azizi Ally kisha itapoa mpaka Misheni. Baada ya hapo utaitafuta foleni nyingine kuanzia Kizuiani mpaka Mbagala Rangi tatu hii kamba ndio hatari sasa. Foleni kutoka Kizuiani mpaka Mbagala rangi tatu unaweza ukalala kwenye usafiri mpaka ukaota ndoto kabisa.

Kero hii imesababisha baadhi ya wasafiri kushuka na kutembea kwa miguu kutoka Kizuiani mpaka Mbagala. Pia kwa kero hii imepelekea kupoteza mda mwingi sana.

Kwann Serikali ama wanao endesha mradi huu wasitafute ufumbuzi mbadala? Tofauti na barabara hizo zilizo kwenye mradi pembezoni mwa mji kuna barabara za vumbi wameshindwa nn kupitisha greda ili kusawazisha mashimo kisha zitumike kwa wakati huu ili kuondoa hii kadhia.
 
Changamoto ya Mbagara sio Mradi wa Ujenzi wa Mwendokasi, changamoto kubwa inasababishwa na kutokuwepo kwa njia njia Mbadala zaidi ya Njia kuu.
Hali hiyo imepelekea usumbufu hata inapotokea ajali au gari kubwa kuharibika na kufunga njia lazima mlale tu..,
Ufumbuzi wa tatizo hilo ni kufungua njia ya Msikitini itakayotokea Mbagara Viwandani, hao wanaodai fidia walipwe na barabara ipanuliwe kidogo itapunguza Msongamano wa kutoka Mtongani hadi Mbagara!!!
 
Askari wa barabarani wanachangia katika hili..hawajipangi vilivyo zile sehemu korofi sijui kwanini..!

Yaani wao wanajikusanya sehemu moja kisha wanasimamisha magari hovyo hovyo kuliza hiki mara kile bila kujali kama wanasababisha foleni.
 
Changamoto ya Mbagara sio Mradi wa Ujenzi wa Mwendokasi, changamoto kubwa inasababishwa na kutokuwepo kwa njia njia Mbadala zaidi ya Njia kuu.
Hali hiyo imepelekea usumbufu hata inapotokea ajali au gari kubwa kuharibika na kufunga njia lazima mlale tu..,
Ufumbuzi wa tatizo hilo ni kufungua njia ya Msikitini itakayotokea Mbagara Viwandani, hao wanaodai fidia walipwe na barabara ipanuliwe kidogo itapunguza Msongamano wa kutoka Mtongani hadi Mbagara!!!
Hiyo changamoto ya kuwepo kwa njia mmoja tu, ni sawa , ila kwa sasa ilishazoeleka, balaa lililopo sasa la huo mradi wa mwendokasi ni balaaa!!!lisikiee tu, unaweza tumia masaa matatu toka mtongani hadi mbagala!!
 
Kama watu wanashuka na kutembea ili kupunguza vitambi hio imekaa poa, shida ni wenye magari binafsi ambao hawawezi kishuka na kukata wese
 
Changamoto ya Mbagara sio Mradi wa Ujenzi wa Mwendokasi, changamoto kubwa inasababishwa na kutokuwepo kwa njia njia Mbadala zaidi ya Njia kuu.
Hali hiyo imepelekea usumbufu hata inapotokea ajali au gari kubwa kuharibika na kufunga njia lazima mlale tu..,
Ufumbuzi wa tatizo hilo ni kufungua njia ya Msikitini itakayotokea Mbagara Viwandani, hao wanaodai fidia walipwe na barabara ipanuliwe kidogo itapunguza Msongamano wa kutoka Mtongani hadi Mbagara!!!
Mbagarrrrrrrrrrrrrrrrrrrraaaaaa
 
Kwani Morogoro road ilikuwaje? Kuwa mvumilivu ndugu, ujenzi ukiisha foleni itatoweka.
Inategemea na jiografia ya eneo, kwa huku mbagala tatizo ni huyu mkandalasi kuanza kazi kuchimbua kila sehemu kabla ya kuanza kutengeneza barabara za pembeni, kuanzia pale zakiem kuna barabara nyingi tu za kule nyuma viwandani wandeziba yale mashimo gari zingekuwa zinapita kule kwanza zinatokea kipati ingesaidia sana!!sasa zile hazipitiki ni mashimo tupu, kila sehemu amechimba, na kama mvua kubwa ikinyesha siku mbili mfululizo, mbagala hapaendeki tena kwa gari.
 
Inategemea na jiografia ya eneo, kwa huku mbagala tatizo ni huyu mkandalasi kuanza kazi kuchimbua kila sehemu kabla ya kuanza kutengeneza barabara za pembeni, kuanzia pale zakiem kuna barabara nyingi tu za kule nyuma viwandani wandeziba yale mashimo gari zingekuwa zinapita kule kwanza zinatokea kipati ingesaidia sana!!sasa zile hazipitiki ni mashimo tupu, kila sehemu amechimba, na kama mvua kubwa ikinyesha siku mbili mfululizo, mbagala hapaendeki tena kwa gari.

Jana na leo hali ni mbaya sana, naenda hapo Kijichi tu jana nilifika saa tano!! Leo sasa hivi nipo KwaAziziAli na magari yamezimwa kabisaa, hali ni mbaya mno. Foleni inaanzoa msikitini pale, wangefungua njia pale gari ziendelee kupita mbili!!
 
Jana na leo hali ni mbaya sana, naenda hapo Kijichi tu jana nilifika saa tano!! Leo sasa hivi nipo KwaAziziAli na magari yamezimwa kabisaa, hali ni mbaya mno. Foleni inaanzoa msikitini pale, wangefungua njia pale gari ziendelee kupita mbili!!
Kuishi maeneo ya mbagala kwa sasa ni mateso!!mtu anaekwenda vikindu kutokea tmk, siku hizi inabidi alipe buku, gari zikifika hapo 77, zinaingilia njia ya ng'ombe hapo, zinakwenda hadi mikwambe ndio zirudi kongowe na kwenda vikindu!!!
 
Mkitaka maendereooo lazima mkubari na mvumirie maumivuu

Ova
 
Back
Top Bottom