Mradi wa gesi wa LNG wa TPDC umeuzwa kwa mabeberu pia? Wanamaanisha nini wanaposema gesi si ya kwetu tena tayari imeuzwa?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,500
46,028
Wenye uelewa na hili jambo la gesi yetu huko kusini kuuzwa kwa mabeberu au wachina wanieleshwe.

1.Kuuzwa huko kwa hiyo gesi kunamaanisha kwamba hiyo gesi si mali yetu tena na sisi tumebaki kama wateja tu?

2.Vitalu vyote vya kuzalisha gesi vimeuzwa tayari na hivyo hatuwezi kuwa na vitalu vyetu tofauti?

3.Hiyo gesi iliuzwa kwa kiasi gani cha fedha?

4.Iliuzwa kwa mabeberu gani? Wa Marekani, Ulaya au China?

5.Mradi wa mkubwa wa dola za kimarekani bilioni 30 wa gesi wa LNG ambao ulikwama kipind JPM na ambao unaonekana kupigiwa chapuo na Rais Suluhu sio sehemu ya gesi hiyo iliyouzwa?

Maswali haya yanatokana na kauli za wale wanaotaka mradi mpya wa umeme wa maji wa bwawa la Nyerere huko Selous ujengwe iwe mvua iwe jua pamoja na uwepo wa gesi nyingi huko kusini ambayo inaweza kuwa nishati mbadala ya kuzalisha umeme huku ikizalisha faida lukuki kuliko huo umeme wa maji.

Jambo lingine ni kwamba kama taifa tulikopa pesa nyingi kutoka nje kwa ajili bomba la gesi ambalo inasemekana matumizi yake hayajawahi kuvuka robo ya uwezo wake!
Kwa nini tuachane na uwekezaji huo wa msingi kabisa?
 
uwepo wa gesi nyingi huko kusini ambayo inaweza kuwa nishati mbadala ya kuzalisha umeme huku ikizalisha faida lukuki kuliko huo umeme wa maji.
Tufundishe faida na hasara za kuzalisha umeme kwa njia ya maji na kwanjia ya gesi, kama umejipanga kisawasawa. Faida zijielekeze kuwanufaisha wananchi katika masuala ya fedha na uchumi.
 
Wenye uelewa na hili jambo la gesi yetu huko kusini kuuzwa kwa mabeberu au wachina wanieleshwe.

1.Kuuzwa huko kwa hiyo gesi kunamaanisha kwamba hiyo gesi si mali yetu tena na sisi tumebaki kama wateja tu?

2.Vitalu vyote vya kuzalisha gesi vimeuzwa tayari na hivyo hatuwezi kuwa na vitalu vyetu tofauti?

3.Hiyo gesi iliuzwa kwa kiasi gani cha fedha?

4.Iliuzwa kwa mabeberu gani? Wa Marekani, Ulaya au China?

5.Mradi wa mkubwa wa dola za kimarekani bilioni 30 wa gesi wa LNG ambao ulikwama kipind JPM na ambao unaonekana kupigiwa chapuo na Rais Suluhu sio sehemu ya gesi hiyo iliyouzwa?

Maswali haya yanatokana na kauli za wale wanaotaka mradi mpya wa umeme wa maji wa bwawa la Nyerere huko Selous ujengwe iwe mvua iwe jua pamoja na uwepo wa gesi nyingi huko kusini ambayo inaweza kuwa nishati mbadala ya kuzalisha umeme huku ikizalisha faida lukuki kuliko huo umeme wa maji.

Jambo lingine ni kwamba kama taifa tulikopa pesa nyingi kutoka nje kwa ajili bomba la gesi ambalo inasemekana matumizi yake hayajawahi kuvuka robo ya uwezo wake!
Kwa nini tuachane na uwekezaji huo wa msingi kabisa?
Huu ni upotoshaji wa kiwango cha lami.Kimsingi hata hujui ulichandika ,hivi unayo taarifa kuwa asilimia zaidi ya 60 ya umeme unazalishwa hapa nchini unatokana na Gesi?kama sio bomba la hesi lilijengwa enzi za JK hadi leo umeme hapa nchini bado ungekuwa ni wa mgao ?Kwa taarifa yako tu ,mgao wa umeme nchi hii umekuwa ni historia kutokana na matumizi gesi asilia.
Unapongelea mradi wa LNG ni kwamba hata hujui maana eti ni gesi ambayo ilishuzwa ?so kama ilishauzwa kwa nini tujenge tena LNG ?Mama simamia huu mradi ,alieshindwa kuusimamia ni shauri ya upuuzi wake ,Mama unayo nafasi ya kuweka historia kwa kukamilisha mradi wa LNG ambao ndio utakuwa mradi mkubwa kwenye uwekezaji kuliko mradi mwingine wowote hapa Africa.
 
Kwenye suala la gesi naona hata yule mzee wa makinikia, aliufyata mkia katika mazingira ambayo hayakutarajiwa na wengi!

Huenda Mabeberu wa kwenye huo mradi wa gesi, wana nguvu za kipekee!!
 
.................................................................................5.Mradi wa mkubwa wa dola za kimarekani bilioni 30 wa gesi wa LNG ambao ulikwama kipind JPM na ambao unaonekana kupigiwa chapuo na Rais Suluhu sio sehemu ya gesi hiyo iliyouzwa? ...............
Kipengere cha tano kimenigusa kuhusu kuchelewa kwa mradi.
Mradi huu mkubwa wa LNG haukuchelewa kuanzia kipindi cha JPM.
Hapana.
Ulichelewa kuanzia kipindi cha pili cha JK, Awamu ya 4, kwa miaka 5.
Kilichochelewesha hiyo miaka 5 kilikuwa Umiliki wa Eneo la Mradi lililokuwa na Hati ya Shamba la Mkonge la Mohamed Enterprises.
JPM alilitatua hilo mwanzoni mwa utawala wake, na TPDC wakakabidhiwa Hati ya Umiliki.
Kukwama kwa mara ya pili kulikuja kutokea kutokana na Serikali kutunga Sheria Mpya ya Umiliki wa Rasilimali za Taifa wenye lengo la kuleta manufaa kwa Taifa letu.
Wawekezaji walikuwa wameisha ingia Mikataba na Serikali, ambayo kwa mujibu ya Sheria yetu mpya ya Umiliki wa Rasilimali za Taifa, ilihitaji Mikataba hiyo kupitiwa upya.
Hapo kukaleta kizaazaa.
Ukweli ni kwamba Mikataba yote kabla ya Sheria hiyo mpya ya 2017, haikuwa na manufaa kwa Nchi yetu, zaidi ya kutuachia mashimo baada ya Gesi kumalizika, miaka 40 ijayo.
 
Huu ni upotoshaji wa kiwango cha lami.Kimsingi hata hujui ulichandika ,hivi unayo taarifa kuwa asilimia zaidi ya 60 ya umeme unazalishwa hapa nchini unatokana na Gesi?kama sio bomba la hesi lilijengwa enzi za JK hadi leo umeme hapa nchini bado ungekuwa ni wa mgao ?Kwa taarifa yako tu ,mgao wa umeme nchi hii umekuwa ni historia kutokana na matumizi gesi asilia.
Unapongelea mradi wa LNG ni kwamba hata hujui maana eti ni gesi ambayo ilishuzwa ?so kama ilishauzwa kwa nini tujenge tena LNG ?Mama simamia huu mradi ,alieshindwa kuusimamia ni shauri ya upuuzi wake ,Mama unayo nafasi ya kuweka historia kwa kukamilisha mradi wa LNG ambao ndio utakuwa mradi mkubwa kwenye uwekezaji kuliko mradi mwingine wowote hapa Africa.
Ata wewe uliyemjibu hujui ulichokiandika
 
Kipengere cha tano kimenigusa kuhusu kuchelewa kwa mradi.
Mradi huu mkubwa wa LNG haukuchelewa kuanzia kipindi cha JPM.
Hapana.
Ulichelewa kuanzia kipindi cha pili cha JK, Awamu ya 4, kwa miaka 5.
Kilichochelewesha hiyo miaka 5 kilikuwa Umiliki wa Eneo la Mradi lililokuwa na Hati ya Shamba la Mkonge la Mohamed Enterprises.
JPM alilitatua hilo mwanzoni mwa utawala wake, na TPDC wakakabidhiwa Hati ya Umiliki.
Kukwama kwa mara ya pili kulikuja kutokea kutokana na Serikali kutunga Sheria Mpya ya Umiliki wa Rasilimali za Taifa wenye lengo la kuleta manufaa kwa Taifa letu.
Wawekezaji walikuwa wameisha ingia Mikataba na Serikali, ambayo kwa mujibu ya Sheria yetu mpya ya Umiliki wa Rasilimali za Taifa, ilihitaji Mikataba hiyo kupitiwa upya.
Hapo kukaleta kizaazaa.
Ukweli ni kwamba Mikataba yote kabla ya Sheria hiyo mpya ya 2017, haikuwa na manufaa kwa Nchi yetu, zaidi ya kutuachia mashimo baada ya Gesi kumalizika, miaka 40 ijayo.
Huo ndo ukweli

Sent from my SM-A015F using JamiiForums mobile app
 
Kipengere cha tano kimenigusa kuhusu kuchelewa kwa mradi.
Mradi huu mkubwa wa LNG haukuchelewa kuanzia kipindi cha JPM.
Hapana.
Ulichelewa kuanzia kipindi cha pili cha JK, Awamu ya 4, kwa miaka 5.
Kilichochelewesha hiyo miaka 5 kilikuwa Umiliki wa Eneo la Mradi lililokuwa na Hati ya Shamba la Mkonge la Mohamed Enterprises.
JPM alilitatua hilo mwanzoni mwa utawala wake, na TPDC wakakabidhiwa Hati ya Umiliki.
Kukwama kwa mara ya pili kulikuja kutokea kutokana na Serikali kutunga Sheria Mpya ya Umiliki wa Rasilimali za Taifa wenye lengo la kuleta manufaa kwa Taifa letu.
Wawekezaji walikuwa wameisha ingia Mikataba na Serikali, ambayo kwa mujibu ya Sheria yetu mpya ya Umiliki wa Rasilimali za Taifa, ilihitaji Mikataba hiyo kupitiwa upya.
Hapo kukaleta kizaazaa.
Ukweli ni kwamba Mikataba yote kabla ya Sheria hiyo mpya ya 2017, haikuwa na manufaa kwa Nchi yetu, zaidi ya kutuachia mashimo baada ya Gesi kumalizika, miaka 40 ijayo.
Kwa hiyo suluhisho la haya yote ni nini ili na sisi tuifaidi gesi yetu?
 
Huwa nashindwa kuelewa mtu anazungumzia faida ya mradi wakati wa kujengwa ...mara utajiri watu 15000 kujenga..mama ntilie...watoa huduma nk..
.lakini hawazungumzi kama nchi wananchi watafaidi nini baada ya mradi kukamilika kujengwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenye uelewa na hili jambo la gesi yetu huko kusini kuuzwa kwa mabeberu au wachina wanieleshwe.

1.Kuuzwa huko kwa hiyo gesi kunamaanisha kwamba hiyo gesi si mali yetu tena na sisi tumebaki kama wateja tu?

2.Vitalu vyote vya kuzalisha gesi vimeuzwa tayari na hivyo hatuwezi kuwa na vitalu vyetu tofauti?

3.Hiyo gesi iliuzwa kwa kiasi gani cha fedha?

4.Iliuzwa kwa mabeberu gani? Wa Marekani, Ulaya au China?

5.Mradi wa mkubwa wa dola za kimarekani bilioni 30 wa gesi wa LNG ambao ulikwama kipind JPM na ambao unaonekana kupigiwa chapuo na Rais Suluhu sio sehemu ya gesi hiyo iliyouzwa?

Maswali haya yanatokana na kauli za wale wanaotaka mradi mpya wa umeme wa maji wa bwawa la Nyerere huko Selous ujengwe iwe mvua iwe jua pamoja na uwepo wa gesi nyingi huko kusini ambayo inaweza kuwa nishati mbadala ya kuzalisha umeme huku ikizalisha faida lukuki kuliko huo umeme wa maji.

Jambo lingine ni kwamba kama taifa tulikopa pesa nyingi kutoka nje kwa ajili bomba la gesi ambalo inasemekana matumizi yake hayajawahi kuvuka robo ya uwezo wake!
Kwa nini tuachane na uwekezaji huo wa msingi kabisa?
Pokea majibu from the horses mouth

P
 
Back
Top Bottom