Mr. II aibuka dhidi ya Zinduka!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Utata mkubwa umejitokeza ni nani aliekuwa na haki ya kutangaza tamasha la Zinduka ,..yaani kampeni ya kitaifa ya uzinduzi wa kukataa malaria.

Hali hiyo imejitokeza leo baada ya msanii Mr II kutangaza kwamba yeye ndie alieiomba kampuni husika ya Marekani kuja kuzindua no more malaria,...na badala yake ameshangaa kuona anaondolewa dk za mwisho,...hili swala ni la kisheria nimefungua lalamiko kule mMarekani na hapa natarajia kwenda mahakamani Jumatano kutoa malamiko yangu,...

Akishangaza waandishi wa habari Mr II aliigeukia kampuni ya sanaa iitwayo THT inayoongozwa na Bwana Ruge Mtahaba kwa kushiriki kenye tamasha hili.. Akijibu hoja hiyo Ruge alisema yeye hawezi kuongea chcochote, anamheshimu Mr II na amemwandikia aende mahakamani ili haki ikajulikane.

"Mimi ninafanya biashara na wasanii huwezi ukaniambia niache kutafuta wasanii wakati nahitaji hela, matatizo yake amalizane nao huko huko" Ruge alisema

Mr 2II inasemekana alikuwa anajiandaa kwenda kusimamisha tamasha hilo kabla hajasikia rais wa Tanzania ndie mhusika mkuu na kuamua kuwachia liendelee na lilipomalizika mambo ndio kama haya yameanza,...



VIDEO:

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=22f2_8d6F6M"]YouTube- Mr. II Sugu.(BONGO STAR LINK - www.djchoka.blogspot.com)[/ame]

Sugu akiongea na waandishi

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=W0lP3Sy2GSY"]YouTube- Ruge Mutahaba.mp4[/ame]

Ruge akijibu hoja

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=q2KlMlmLIPw"]YouTube- (GPLTZ.COM) Exclusive Interview with MR II[/ame]

Mr. II alipotembelea ofisi za Global Publishers


My take:

Wasanii nadhani hili swala la kuhamasisha watanzania kuhusu jambo fulani muhimu kwa kila mtanzania liwe huru kwa kila mtu na isifanyike kama mtaji wa watu kutokea kimaisha...

Nimehuzunishwa sana maana wakati na siku ya uzinduzi kuna watu walisema hawa hamna kitu hapo ndio imetoka watu washakula hela basi, hakuna malaria wala nini,...sasa naanza kuamini haya mambo ni hatari jamani,...

Mr II kaeni chini mmalizane badala ya kuanza kuita waandishi na kuanza kuaibishana mbele ya kadamnasi,...na mimi kama mdau nakutakia fidia njema ya dollar 260,000 ulizozidai huko Marekani kwenye kampuni ya No More Malaria, usinisahau kwenye ufalme wako
 
Srce
hayo yamesemwa na mr 2 wakati wa taarifa ya habari kipindi cha michezo tbc
 
Leo msanii Joseph Mbilinyi(Mr II) amefanya mkutano na wanahabari na kuanika tuhuma ya kuporwa mradi na maofisa ya ikulu ya Tanzania wakiongozwa na January Makamba na kupewa Ruge Mutahaba wa Clouds FM.

Mradi huo wa ZINDUKA wa malaria ulizinduliwa karibuni na Rais Jakaya Kikwete.

Ameonyesha vielelezo vya mawasiliano yake ya barua pepe ya miaka takribani miwili na wahusika na namna January Makamba alivyotumia nafasi yake ikulu kwenda tofauti na makubaliano ya awali kati yake na taasisi ya Malaria NO MORE.

Stay Tuned

PM
 
Aende mahakamani ili haki itendeke anavyofanya hivyo anakosea sana yeye kama msanii anajidhalilisha
 
Aende mahakamani ili haki itendeke anavyofanya hivyo anakosea sana yeye kama msanii anajidhalilisha
Shy,
Unaweza kutuambia ni lini na tupe mfano wa haki ilipotendeka mahakani Bongo?
 
Usicheze na Ruge , kiboko ya wasanii, peleka dili then una achwa kwenye mataa , hii nikawaida kwa Tanzania lakini , pole sana SUGU nend amahakamani!

Tutanzisha kampeni ya RUGe asipewe usimamizi wa hiyo Mastering Studio ndio tumeshaanza maandalizi tuna anza na maandamano, no voting mbaka RUge awe pembeni..JK hatutaki RUge
 
mpakaleo nashindwa kujua kama tamasha la 'zinduka' ni biashara au msaada wa kupambana na malaria?

hayo mengine ya madili au nini ni kawaida nchini kwetu sema hapa kidogo wamefika mbali kama lengo lilikuwa msaada wakahamua kufanya biashara.

hile siku kama ilikuwa ni harambee basi walalahoi walijichangia 3000 wasubiri net zao za mbu zinakuja ,kama ilikuwa ni introduction wa msaada wa vyandarua basi sh 3000 zao ni takrima na net za mbu wameenda kuzijaribu VIPs kama zinafaa kabla ya kuwapa walalahoi.
 
well.. sisi tumejifunza kwenye suala la kusaidia Red Cross!!!
yapi tena yaliwakuta mkuu? kama nzito sana hiweke kapuni tu manake hii ya "zinduka" naona mchezo mchafu uliofanyikwa mpaka ujumbe umeshindwa kuwafikia walengwa.

kama ni biashara basi hawajakosea manake biashara ushindani ,lakini kama ilikuwa msaada kaufisadi kamewafikia mpaka watoto sasa nao.
 
I hate some coincidences...

Tukapanga kusaidia Red Cross.. na tukazungumza na mashirika mbalimbali ya simu.. mojawapo ni Vodacom.. tukazungumza na mkuu wake wa Vodacom Foundation Dada... akaona ni wazo zuri na akawa tayari kutuunga mkono..

Tukaenda Clouds FM na nikazungumza kuhamasisha..

within few days..

Foundation ya dada.. wakaja na mpango wao kama huo huo wakitarajia kukusanya fedha zaidi kusaidia foundation yao (siyo Red Cross). kupitia.. you guessed it Clouds FM...
 
Inamaana kule kumvesha T shirt Mkulu ya Zinduka na kumwita usiku ule pale Leaders yote ilikuwa kumwingiza mjini watu wale mishiko? ama kweli sasa Mkulu umeruhusu watu wakufanye mtaji kama alivyosema Makamba kuwa wewe ni Mtaji.

Nakumbuka walivyo mwita kule Arusha afungue Hoteli kwa mbwembwe na kesho yake Tanroad wanaibomoa. Naona sasa nchi inaendeshwa kama kikundi cha Mdumange, maana kama Mkulu anafanywa mtaji naye anatabasamu tuu, ANATUDHALILISHA WOTE
 
Mwanakijiji,

how comes you kept quiet for such long time without telling me this kinda foolish behavior?

am mad too

Kitu kingine cha kipuuzi ni kitendo cha rais kupelekwa kwenye tamasha amablo limekaa kitapeli..No more Malaria ila mpaka sasa nini kimefanyika?aua lengo ao lilikuwa ni nini?wtf?

Usalama wa taifa uko wapi?
mpaka kumpeleka Rais kwenye kampeni ambayo ilikuwa imejaa usanii?am mad but am glad anyways coz ya watu wanopenda sifa na kujihusisha na mambo yasiyo na msingi
 
enheeeeee bora hili sakata asingekuwemo Ruge au clouds FM and associates . si ndo hao hao kupiga nyimbo za Mr II kwao mwiko. Kwa style hii wanamtonesha kidonda.
 
Mkuu wa kaya kaahidi kuwalinda wasaniii....! Hebu aanzie kwenye hili. Sasa sikiliza siasa zitakavyoingia hapo!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom