Mr Bernard Membe Addressing the 67th session of the United Nations General Assembly in New York

teh teh..hiyo ndiyo CCM chama cha Hovyo kabisa africa. Mwenyekiti wa CCM wilaya huwa pia anachanganya majukumu yake na ya mkuu wa wilaya.
 
Ninajiuliza inapotokea Makamo wa kwanza wa SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA anapotembelea Tanzania Bara na kupokelewa kwa heshima zote ikiwemo na kupigiwa saluti je Katiba yetu inakitambua cheo hicho? Wajuzi wa Katiba /Sheria naomba ufafanuzi.

Hakuna sehemu inayoitwa Tanzania bara.
Muungano wa mambo 11 wa 1964 uliundwa na nchi zipi?
Kama unajua majina hayo basi pia ndio majina ya pande hizo za Muungano.
Ukizungumza muungano unazungumzia Tanzania.
Unapozungumzia pande mbili za muungano basi kwa usahihi ni Tanganyika na Zanzibar.

Tanzania bara imetoka wapi? Jaji Warioba atakusaidia ukimtupia swali hili.

Mimi si mwanasheria lakini kwa uelewa wangu wa usanii/mazingaombwe ya Muungano wa Tanzania
ni kuwa, uwepo wa serikali ya Zanzibar hautegemei baraka/ matakwa ,upendo au hasira za serikali ya Muungano.
Katiba ya Muungano kuweka vipengele vinavyoihusu/ vinavyohusiana na serikali ya Zanzibar ni katika hayo mazingaombwe.

Je serikali ya Zanzibar ni katika yale mambo 11(22) ya muungano?

Kimsingi serikali ya Zanzibar ni mamlaka inayojitegemea. muundo wa serikali ya Zanzibar au aina ya viongozi watakaoendesha serikali hiyo yanatokana na sheria za baraza a wawakilishi. It has nothing to do with the union constitution.

Kama hili ni gumu kulifahamu. Jiulize. Kati ya serikali ya muungano na serikali ya Zanzibar ipi ilikuwepo mwanzo?
Serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika zilikubaliana kuunganisha mambo 11 ambayo yaliitwa mambo ya muungano. Na kutokana na makubaliano hayo ndio iliundwa serikali ya Muungano (ilipewa mamlaka ya kusimamia mambo 11 yaliyoitwa mambo ya muungano)

Mwalimu Nyerere kwa utaalamu wake, alikasimisha pia mamlaka ya serikali ya Tanganyika juu ya yale mambo ambayo si ya muungano (mambo ya Tanganyika) kwa serikali ya Muungano ambayo yeye aliiongoza kwa miaka 24(26?). Wabunge wetu wa Tanganyika kupitia sheria ya muungano ya 1964 waliridhia huu utaratibu wa kukasimisha mamlaka ya Tanganyika kwa serikali ya Muungano. Kwa maneno mengine waliridhia serikali ya Tanganyika iwe serikali kivuli(ghost/ invisible).

Mazingaombwe yalianza hapo au kama ni usanii/ukiini macho ulianza hapo. Hivi mamlaka ya kuifuta serikali ya nchi ilitoka wapi/inapatikana wapi?

Rais wa Tanganyika na wabunge wa Tanganyika walitoa/walipata wapi mamlaka ya kuifuta nchi,katiba ya nchi na serikali ya nchi? Au jina la nchi!!??

Rais wa Tanganyika na wabunge wetu wa Tanganyika walipata wapi mamlaka ya kuifuta serikali yetu?
Wao wanayo mamlaka ya kuingia mikataba ya kimataifa kwa niaba ya nchi/ wananchi. Hilo halina ubishi. Lakini hawana mamlaka ya kuifuta katiba na serikali ambayo iliwaweka wao madarakani.

Mkuu. Usitoneshe kidonda. Haya mazingaombwe ya muungano yanahitaji kuondoshwa lakini naona kama hatuna ujasiri vile. Badala ya kuonesha mzizi wa tatizo. tunaulizia mambo ya watu. Serikali ya Zanzibar ni ya wazanzibari. Haituhusu.

Serikali inayotuhusu sisi(wabara/watanganyika) ni serikali ya muungano na serikali zetu za mitaa.

Utata wa haya ya makamu wa rais/ rais wa Zanzibar tulizidi kuyaparaganya tulipoondosha utaratibu wa Rais wa Zanzibar kuwa makamu wa Rais wa serikali ya muungano.

Itakuwa ni suala la kiitifaki zaidi lakini makamu wa rais wa Zanzibar hana nafasi yoyote ya kiutendaji katika serikali ya muungano.
Hapa natofautiana na watu wengi wanaosema kuwa Katiba ya serikali ya Muungano inamtambua waziri kiongozi.
Kwa maoni yangu, Katiba ya muungano haipaswi kabisa kuwa na vifungu vinavyoihusu serikali ya Zanzibar.
Zanzibar wana haki na uhuru kuamua muundo na aina ya viongozi wanaotaka wawe nao katika serikali yao.

Mazingaombwe tuliyokuwa nayo, tuliyafanya kuwa kiroja zaidi kwa kumtupa (mkakatiwa kisiasa) mwakilishi mkuu wa wazanzibari/serikali ya Zanzibar(rais wa Zanzibar) nje ya muundo wa serikali ya Muungano.

Makosa haya mawili 1. kuifuta katiba ya Tanganyika na serikali yake. na 2. kumwondoa Rais wa Zanzibar katika nafasi ya umakamu wa rais wa serikali ya muungano yametuweka katika usanii wa hali ya juu(ukiini macho) na tunapata tabu/tunashindwa kuuelezea au kuufafanua na kuweza kufahamika muungano wa mambo 11 (au 22) baina ya Tanganyika na Zanzibar aka muungano wa Tanzania.

Hivi Bilali anamwakilisha nani? Kama sio yeye mwenyewe na familia yake?

Tanzania bana...Jenerali Ulimwengu ametutahadharisha kuhusu "upuuzi" lakini wadanganyika tumekuwa kama mbuzi.Mziki(gita) linapigwa lakini hatuchezi. Basi hata hatufikiri? Hatujui chanzo cha mauza uza haya ya muungano?
Natumai nimechokoza fikra za wadanganyika wenzangu hapa.

Hapo juu usahihishe hakuna sehemu inayoitwa Tanzania bara bali ni Tanganyika.
 
Huna taarifa kwamba mbolea inaliwa na mafisadi?Ndo hayo ambayo hakuyasema kuhusiana na MDG.Ufisadi ni kikubwa kinachokwamisha everything.Si kwenye kilimo si kwenye uwekezaji.Alizungumzia hilo?

Itafikia wakati mtashindwa kuwapa mimba wake zenu kwa kisingizio cha mafisasi; hivi umeshasoma kilichomo kwenye kilimo kwanza kabla kujikita kwenye mjadala?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Zanzibar haijawahi kuwa nchi, Karume aliajiriwa tu na Nyerere, wewe unajua kwanini Mwalimu alimtumia huyu Mmalawi Karume badala ya John aliepindua au kina Hanga waliouliwa na Karume au kina Babu waliofukuzwa na Karume au angemweka Mnyamwezi yeyote katika wale walioletwa kupindua? Mimi ni Mkiristu wa Zanzibar na ni kati Wazanzibari asilia, lakini nadiriki pia kusema Mzanzibari halisi hakuna. Zanzibar leo kwa tamaaa na kujisikia tunajiundia historia tunavyopenda sisi tu.
 
Zanzibar haijawahi kuwa nchi, Karume aliajiriwa tu na Nyerere, wewe unajua kwanini Mwalimu alimtumia huyu Mmalawi Karume badala ya John aliepindua au kina Hanga waliouliwa na Karume au kina Babu waliofukuzwa na Karume au angemweka Mnyamwezi yeyote katika wale walioletwa kupindua? Mimi ni Mkiristu wa Zanzibar na ni kati Wazanzibari asilia, lakini nadiriki pia kusema Mzanzibari halisi hakuna. Zanzibar leo kwa tamaaa na kujisikia tunajiundia historia tunavyopenda sisi tu.

Mkuu Democracy999,
Hayo niliyoyaweka katika rangi nyekundu ni maneno yako ambayo sikuyaelewa au ningependa ukipata muda kwa faida ya wanajf pia uyatolee ufafanuzi au uyajibu. Yaliyo katika weusi ni maswali yangu, tafadhali tusaidie tukuelewe unakusudia kusema nini. Hatujakuelewa bado.

1.Zanzibar haijawahi kuwa nchi,
Huyu John alipindua nini? Kama jibu ni serikali, ni serikali ya nchi ipi ambayo John alipindua?

Pia unamaanisha Zanzibar haikubaliana na Tanganyika kuunganisha mambo 11 na hivyo kuunda Muungano?

2. Karume aliajiriwa tu na Nyerere,

Mkuu, ulishuhudia utiaji saini wa makataba wa ajira baina ya Nyerere na Karume? Au umepata wapi habari hii ya Nyerere kumtumia Karume(mmalawi)

3. wewe unajua kwanini Mwalimu alimtumia huyu Mmalawi Karume badala ya John aliepindua

Hapa nakiri kuwa sijui, tafadhali nipatie shule/darasa juu ya hili.

4.au kina Hanga waliouliwa na Karume au kina Babu waliofukuzwa na Karume au angemweka Mnyamwezi yeyote katika wale walioletwa kupindua?

Kwa nini Nyerere hakuwatumia hao uliowataja hapa?

5.Mimi ni Mkiristu wa Zanzibar na ni kati Wazanzibari asilia, lakini nadiriki pia kusema Mzanzibari halisi hakuna.
Wewe ni mkiristo, ok. Ungekuwa mwislamu kungekuwa kuna tofauti yoyote? Ipi?
Unasema wewe ni mzanzibari asilia halafu unasema hakuna Mzanzibari asilia. Hapa umekusudia kusema nini?


6.Zanzibar leo kwa tamaaa na kujisikia tunajiundia historia tunavyopenda sisi tu

Historia ipi hiyo mnayojiundia mkuu? Tuelimishe hapa!

Pia tueleweshe, tamaa ipi hiyo mliyonayo? Na mnajisikia vipi? Ni historia ipi hiyo mnayoipenda?
 
Itafikia wakati mtashindwa kuwapa mimba wake zenu kwa kisingizio cha mafisasi; hivi umeshasoma kilichomo kwenye kilimo kwanza kabla kujikita kwenye mjadala?

Chama
Gongo la mboto DSM
Wewe unataka nimpe mimba mke wako?
 
Nonda;4732913]Hakuna sehemu inayoitwa Tanzania bara.Muungano wa mambo 11 wa 1964 uliundwa na nchi zipi?.......Je serikali ya Zanzibar ni katika yale mambo 11(22) ya muungano...........Serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika zilikubaliana kuunganisha mambo 11 ambayo yaliitwa mambo ya muungano. Na kutokana na makubaliano hayo ndio iliundwa serikali ya Muungano (ilipewa mamlaka ya kusimamia mambo 11 yaliyoitwa mambo ya muungano)?
Nonda, usitahayari Ahli wangu, hayo unayoyaita mambo 11 ndio Mkataba. Kwahiyo sema hivi: katika mambo 11 ya mkataba wa mwaka 1964. Hakuna kitu kinaitwa mambo, mambo ni neno. Kilichotokea mwaka 1964 ni mkataba wa muungano(Article of union).Unakwepa kusema mkataba kwasababu ZNZ inadai uwepo mkataba, wenye akili zao wanasema huu ni mkataba kabla ya mkataba uvunjwe kwanza huu uliopo wa 1964. Ushanifahamu !
uwepo wa serikali ya Zanzibar hautegemei baraka/ matakwa ,upendo au hasira za serikali ya Muungano...Katiba ya Muungano kuweka vipengele vinavyoihusu/ vinavyohusiana na serikali ya Zanzibar ni katika hayo mazingaombwe........Kimsingi serikali ya Zanzibar ni mamlaka inayojitegemea. muundo wa serikali ya Zanzibar au aina ya viongozi watakaoendesha serikali hiyo yanatokana na sheria za baraza a wawakilishi.........It has nothing to do with the union constitution....... Serikali ya Zanzibar ni ya wazanzibari. Haituhusu
Nashukuru sana kuwa unajibu hoja za siku nyingi WZNZ wanaogopa kuzikabili. Kwa maelezo yako Naomba nimualike Baru baru. Yeye anasema muungano utavunjwa na bunge la JMT. Kwa maelezo yako mwanana 'that has nothing to do with Zanzibar'. Umeelewa kuwa hatima ya ZNZ ipo mikononi mwa BLW na SMZ. Kwahiyo ZNZ ingetaka kuvunja muungano hakuna pingamizi, kinachotokea ni hofu ya wapi watajibanza? Ndiyo maana tunaona EU, Senegambia, Uswiss n.k.
Hapa natofautiana na watu wengi wanaosema kuwa Katiba ya serikali ya Muungano inamtambua waziri kiongozi.Kwa maoni yangu, Katiba ya muungano haipaswi kabisa kuwa na vifungu vinavyoihusu serikali ya Zanzibar.Zanzibar wana haki na uhuru kuamua muundo na aina ya viongozi wanaotaka wawe nao katika serikali yao
Hapa napo unajichanganya tena sana. Unapokuwa na mambo 1, 2, 11 au 32 huwezi kuepeuka mahusiano ya serikali. Mathalani, utazungumziaje mambo ya ulinzi na usalama bila kushirikisha serikali zote mbili?
Hayo mambo 11 unawezaje kuyatekeleza kama hutahusisha serikali husika? Ni jambo gani katika hayo 11 ambalo unadhani linaweza kufanyika bila kushirikisha SMZ.
Mazingaombwe tuliyokuwa nayo, tuliyafanya kuwa kiroja zaidi kwa kumtupa (mkakatiwa kisiasa) mwakilishi mkuu wa wazanzibari/serikali ya Zanzibar(rais wa Zanzibar) nje ya muundo wa serikali ya Muungano.....Hivi Bilali anamwakilisha nani? Kama sio yeye mwenyewe na familia yake?
Hili nalo linahitaji ufahamu. Gharibu Bilal alipata nafasi hiyo kwasababu ya Uzanzibar wake. Juzi alipewa bilioni 32 apeleke ZNZ kupitia ofisi ya makamu wa Rais. Kama hilo si kweli WZNZ wangeanza na kumkana kwanza makamu wa Rais wakane pesa ili tujue msimamo wao.

Unajua ubinafsi, uchoyo, fitna na majungu vinawatesa sana WZNZ. Inafikia mahali ukisikia matamshi fulani unahisi wanamdhihaki muumba. Huwezi kuwa muumini ukiwa na roho ya chuki, umeshiba fitna, na kuvimbiwa uchoyo.

Mfano, SMZ imepeleka mswada wa kuondoa mafuta katika mambo ya muungano. Hakuna hata siku moja wamewahi kujadili kwanini wanatumia umeme bure. Hapa mafuata ni SMZ, umeme ni Tanzania.
 
Duh!Yani kuanzia ndani hadi nje anapongezwa tu.Na wakati picha nyingine ni kama tu photo opp.Kama hizo picha nyingine za nje bado tu anapongezwa lol!Anyways inaonekana walikuwa so excited na hiyo wanayoiita statement,ngoja niitafute niisome.

BTW naona hizi kama mbio za urais.Ndo chaguo la JK huyu?Halafu msafara mkuubwa,wabongo bana,na umasikini wa wananchi lakini wapi!
jmushi1; Hiyo siyo delegation ya Mh. Membe ni Staff wa balozi zetu Washington na New York, bali kunawasaidizi wake wawili tu. Hiyo Hotuba yake imeweka Tanzania juu ya map ya UN maana one of the best message in the World preventive deplomacy. He spoke about from Cuba, Western Sahara, Great Lakes, Palestine to Syria. Big Up Hons. Membe!
 
Last edited by a moderator:
Baada ya hotuba Mh. Membe katika Umoja wa Mataifa, Tanzania imekuwa juu kwa umahiri wake pamoja na ujumbe uliokamilika na ulioenda shule ya nguvu. Mh. membe tunakupongeza kwa hilo!
 
Hawa wagombea uraisi wa 2015 - CCM inabidi watafute watu makini wa kuwapigia kampeni kwenye mitandao. Nadhani huyu mleta uzi anaaminika kwenye kampeni za majukwaani sio mitandaoni. Ila poa kula zutu yako kaka.
 
Harudi tena ulomuuliza maswali hayo :-D nafikiri yeye ndio anajiundia historia yake mwenyewe maana hajui kitu, na siamini kama eti yeye ni mzanzibari halisi kisha eti anauliza tangu lini zanzibar ilikua nchi!

Ni ushahidi tosha kama hajui alisemalo bali anahadithiwa hadithi za paukwa pakawa! Hajui kama zanzibar ilikua na kitu Umoja wa Mataifa, hajui kama zanzibar ilikua na bendera yake, katiba yake, kiongozi wake, mamlaka yake.

Halafu sijamfahamu amekusudia nini aliposema yeye mkiristo, au ndo anataka kuonesha kama wakiristo wapo zanzibar? Hilo linajulikana ndugu ilikua haina maana ya yeye kusema eti mkiristo, labda atamwambie amemaanisha nini?
 
Nonda, usitahayari Ahli wangu, hayo unayoyaita mambo 11 ndio Mkataba. Kwahiyo sema hivi: katika mambo 11 ya mkataba wa mwaka 1964. Hakuna kitu kinaitwa mambo, mambo ni neno. Kilichotokea mwaka 1964 ni mkataba wa muungano(Article of union).Unakwepa kusema mkataba kwasababu ZNZ inadai uwepo mkataba, wenye akili zao wanasema huu ni mkataba kabla ya mkataba uvunjwe kwanza huu uliopo wa 1964. Ushanifahamu ! Nashukuru sana kuwa unajibu hoja za siku nyingi WZNZ wanaogopa kuzikabili. Kwa maelezo yako Naomba nimualike Baru baru. Yeye anasema muungano utavunjwa na bunge la JMT. Kwa maelezo yako mwanana 'that has nothing to do with Zanzibar'. Umeelewa kuwa hatima ya ZNZ ipo mikononi mwa BLW na SMZ. Kwahiyo ZNZ ingetaka kuvunja muungano hakuna pingamizi, kinachotokea ni hofu ya wapi watajibanza? Ndiyo maana tunaona EU, Senegambia, Uswiss n.k. Hapa napo unajichanganya tena sana. Unapokuwa na mambo 1, 2, 11 au 32 huwezi kuepeuka mahusiano ya serikali. Mathalani, utazungumziaje mambo ya ulinzi na usalama bila kushirikisha serikali zote mbili?
Hayo mambo 11 unawezaje kuyatekeleza kama hutahusisha serikali husika? Ni jambo gani katika hayo 11 ambalo unadhani linaweza kufanyika bila kushirikisha SMZ. Hili nalo linahitaji ufahamu. Gharibu Bilal alipata nafasi hiyo kwasababu ya Uzanzibar wake. Juzi alipewa bilioni 32 apeleke ZNZ kupitia ofisi ya makamu wa Rais. Kama hilo si kweli WZNZ wangeanza na kumkana kwanza makamu wa Rais wakane pesa ili tujue msimamo wao.

Unajua ubinafsi, uchoyo, fitna na majungu vinawatesa sana WZNZ. Inafikia mahali ukisikia matamshi fulani unahisi wanamdhihaki muumba. Huwezi kuwa muumini ukiwa na roho ya chuki, umeshiba fitna, na kuvimbiwa uchoyo.

Mfano, SMZ imepeleka mswada wa kuondoa mafuta katika mambo ya muungano. Hakuna hata siku moja wamewahi kujadili kwanini wanatumia umeme bure. Hapa mafuata ni SMZ, umeme ni Tanzania.

Mkuu Nguruvi3
Pole sana kwa maumivu.
Natumai msomaji yeyote atakayesoma mchango wangu na halafu akasoma mchango wako atachanganyikiwa.

Sio tatizo lako lakini ni tatizo la mods kuchanganya threads.

Mchango wangu ulikuwa unajibu au unaweka mwanga juu ya mada ya we gule :Re: Makamo wa kwanza wa rais -suk kupokelewa kitaifa. utaiona post#40 baada ya kulundikwa humu,ilikuwa post #1 alipoianzisha.

Wewe sijui unachangia kuhusu nini. Hata hivyo umepotosha mambo mengi ( out of context) ya kile nilichosema.
Kwa leo nauwacha mchango wako ili ujitanafasi katika furaha kidogo.

Katika niliyoandika katika mchango wangu huo unaouchakachua ni lipi ambalo hukubaliani nalo au si sahihi?
Soma post#40 kwanza halafu mwaga mistari,mkuu.
 
Kobello; Nimekuwa nikifuatilia uwakilishi wa Mh. Membe katika jukwaa la kimataifa, mambo yafuatayo Tanzania imekuwa ipo juu kwenye Ramani ya Dunia! 1. Tanzania inafuata sera za Preventive Diplomacy ili kudumisha amani Duniani hii imetuletea heshima kubwa duniani. 2. AGRF 2012 in Arusha 3. Africa Food Security Program Tanzania ni miongoni mwa nchi tatu kama model ya program. na mengine mengi ambapo Tanzania imekuwa destination ya mikutanon mingi ya dunia.
 
Back
Top Bottom