Mpya: Tume ya Rais ya EPA yalonga

Kamanda

Senior Member
Dec 5, 2007
150
176
Hivi sasa ndiyo kwanza nimemaliza kusikiliza tarifa muhimu kwamba ile Tume ya Rais ya EPA ya kuchunguza ubadhirifu wa fedha za malipo ya akaunti ya madeni ya nje pale BoT imeeleza kuwa imefikia mahali pazuri kutoa taarifa yake.

Tume hiyo katika taarifa yake imesema imeweza kusaidia kurejeshwa kwa kiasi kikubwa cha fedha zilizolipwa kitapeli kwa kampuni za kisanii.

Imesema kuwa mali zisizohamishika zimekamatwa maeneo mengi ya Dar na miji mingine, kuhusu mali zilizo ne ya Tanzania, tume hiyo imesema kuwa nazo zitapatikana karibuni kabla ya kukabidhi ripoti kamili kwa Rais Jakaya Kikwete..

Mwenyekiti amesema wananchi wote wanaombwa kutoa taarifa kwa tume hiyo kwa kutumia namba za simu zifuatazo

+255 784 994881

+255 784 231928

+255 784 785742


Haya jamani mambo yetu yale, kama mnafahamu mali za mafisadi wale wa BoT semeni ili turejeshe serikalini na ziuzwe kama hazihamishiki ili pesa zinazopatikana zikajenge barabara, kununua dawa, kuboresha elimu na dawa hospitalini.

Nawatakieni kila jema.
 
Hivi sasa ndiyo kwanza nimemaliza kusikiliza tarifa muhimu kwamba ile Tume ya Rais ya EPA ya kuchunguza ubadhirifu wa fedha za malipo ya akaunti ya madeni ya nje pale BoT imeeleza kuwa imefikia mahali pazuri kutoa taarifa yake.

Tume hiyo katika taarifa yake imesema imeweza kusaidia kurejeshwa kwa kiasi kikubwa cha fedha zilizolipwa kitapeli kwa kampuni za kisanii.

Imesema kuwa mali zisizohamishika zimekamatwa maeneo mengi ya Dar na miji mingine, kuhusu mali zilizo ne ya Tanzania, tume hiyo imesema kuwa nazo zitapatikana karibuni kabla ya kukabidhi ripoti kamili kwa Rais Jakaya Kikwete..

Mwenyekiti amesema wananchi wote wanaombwa kutoa taarifa kwa tume hiyo kwa kutumia namba za simu zifuatazo

+255 784 994881

+255 784 231928

+255 784 785742


Haya jamani mambo yetu yale, kama mnafahamu mali za mafisadi wale wa BoT semeni ili turejeshe serikalini na ziuzwe kama hazihamishiki ili pesa zinazopatikana zikajenge barabara, kununua dawa, kuboresha elimu na dawa hospitalini.

Nawatakieni kila jema.

Usanii mwingine hata unavuka maelezo ya kawaida. Yaani ni lini sheria za nchi zilibadilishwa na kuruhusu watuhumiwa wa wizi kurudisha mali na sio kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.

Ina maana leo wale watuhumiwa wa wizi wa kuku na simu walioko Keko wanaruhusiwa kuachiwa huru as longer as wanarudisha kile walichoiba?
 
Kama ni kweli, hapa hata sisi die hard Kikwete critics tutampa hongera.Maana hata kama anafanya kwa kutaka approval ratings zipande afanye tu bora mihela ya taifa irudi.

Lakini tatizo ni kuwa bado anakuwa reactionary president, anasubiri mpaka watu waibue mabomu.Ningempa credit zaidi kama yeye mwenyewe na serikali yake wangekuwa wanagundua huu uhuni na kufanya kweli.
 
Kama ni kweli, hapa hata sisi die hard Kikwete critics tutampa hongera.Maana hata kama anafanya kwa kutaka approval ratings zipande afanye tu bora mihela ya taifa irudi.

Lakini tatizo ni kuwa bado anakuwa reactionary president, anasubiri mpaka watu waibue mabomu.Ningempa credit zaidi kama yeye mwenyewe na serikali yake wangekuwa wanagundua huu uhuni na kufanya kweli.

Pundit,

Hii yote bado ni habari tu na hadithi kama za mtaani. Mali zimerudishwa - lakini hawasemi ni za nani, ziko wapi, ni lini zilirudhiswa, zilirudishwa vipi, wahusika ni nani, na wako wapi.

Nimeanza kukumbuka yale aliyosema Kikwete kuwa hakuna upotevu wowote kwenye hazina kabla hajabadilisha story na kusema kuwa pesa zilizopotea ni za ndani na sio za wafadhili.

Mhhh, yangu macho hapa na masikio!
 
Kama ni kweli, hapa hata sisi die hard Kikwete critics tutampa hongera.Maana hata kama anafanya kwa kutaka approval ratings zipande afanye tu bora mihela ya taifa irudi.

Lakini tatizo ni kuwa bado anakuwa reactionary president, anasubiri mpaka watu waibue mabomu.Ningempa credit zaidi kama yeye mwenyewe na serikali yake wangekuwa wanagundua huu uhuni na kufanya kweli.


Mimi nina akili timamu siwezi kuwaamini hawa .Wanataka kumpa chat jamaa .Hii ni kashfa walio chukua pesa kwa wizi wanajulikana .Wanarudisha baada ya sisi kuwa wakali wajulikane .Kila mmoja asemewe aliiba kiasi gani na karudisha ngapi na baada ya hapo ushahidi umekamilika na kesi inaanza kuunguruma Mahakamani.Haya ya kuambiwa zimerudi uhakika wa kwamba zimerudi ni upi ?Wacha mie ninywe gahawa na kashata mnanizingua sasa.
 
Mhh, usanii tuu, warudishe pesa kimya kimya, na watuhumiwa watachukuliwa hatua gani?,something fishy is happening here, really, may be they are among of them, the dont want to be in public spot
 
Ahsante JK kwa uongozi wako, wenye macho tunauona na wenye masikio tunausikia. uzi huo huo, tunakuombea Mwenyeezi Mungu akuepushe na mahasidi wasioona unachokifanya kwa roho zao mbaya na akuepusha na fitna na majungu na visasi vya hao unao-washughulikia.

Haya wale wanaolonga longer humu waanze kuonyesha uzalendo wao, namba hizo.

Ahsante JK kazi tunaiona. Wengine waanze kukaa mkao wakula zamu yao inakuja.
 
Ahsante JK uongozi wako wenye macho tunauona na wenye masikio tunausikia. uzi huo huo, tunakuomba Mwenyeezi Mungu akuepushe na mahasidi wasioona unachokifanya kwa roho zao mbaya na akuepusha na fitna na majungu na visasi vya hao unao-washughulikia.

Haya wale wanaolonga longer humu waanze kuonyesha uzalendo wao, namba hizo.

Ahsante JK kazi tunaiona. Wengine waanze kukaa mkao wakula zamu yao inakuja.

Mhh JF imevamiwa!

Kama vile alivyoomba kupewa list ya wauza madawa ya kulevya, naona tena hapa watanzania wanaombwa kutaja majina ya walioiba pesa za BoT????!!!!

Haya wale wenye fitna na majungu na visasi ambao mulikuwepo wakati hizo pesa zikiibwa pelekeni ushahidi kwani namba hizo hapa mmepewa!
 
Wandugu: Ni wapi wamesema baada ya kurudisha mali hawatachukuliwa hatua za kisheria in regards to their actions?
 
hapo ni usanii tu kwanza tunataka wajumbe wawili wa hiyo kamati yaani Hosea na Mwanyika wawajibike na swala la Richmond maana uma hatuna imani nao hata kiduchu kutokana na ushilika wao katika hilo swala... Pili tungependa kujua ni kina nani hasa wamerejesha hizo fedha zetu na kina nani wanasuasua!?!?
 
yaani wamerudisha mali ili yaishe kimya kimya. Basi si waambiwe tu warudishe mali yaishe. Maana kutakuwa na umuhimu gani wa kuwafikisha mahakamani wakati wamesharudisha mali?
 
Raha jipe mwenyewe,kwani maisha ni mafupi hebu kongoli hapa,[media]http://www.youtube.com/watch?v=LVC_tHEaIyw&feature=related[/media]
tukiangaika sana na hawa mafisadi tunaweza kufa mapema,maana sasa hata pa kukanyaga hakuna kwa jinsi walivyotapakaa lika kona.
 
Wandugu: Ni wapi wamesema baada ya kurudisha mali hawatachukuliwa hatua za kisheria in regards to their actions?

Hakuna waliposema kuwa watawachukulia hatua either ukichukulia na ukweli kuwa kulingana na propaganda hiyo hapo juu, hakuna jina wala mali (au location ya mali) zilizotajwa.
 
Tuwe 'Optimistic'. Kama sikosei, JK aliipa tume/kamati kazi ya kuchunguza hili na kuhakikisha 1. Fedha zilizoibwa zinarudi, na 2. kuwachkulia hatua wote walihusika na wizi huo wa fedha za umma. Fedha kuanza kurudi kwa 'wenyewe' ni hatua nzuri, na bila shaka hatua hii itafuatiwa na kufikishwa katika sheria wahusika. Huenda kuanza kuwachukulia hatua mapema kutaharibu ushahidi au kuzorotesha upatikanaji wa fedha zetu.
 
Naomba kuuliza hivi ....Hii taarifa kwa umma ina maana gani? Ndivyo walivyo ambiwa na aliyewatuma kuwa baada ya muda fulani watoe progress ya kazi hiyo? kwani akina Mwakyembe walifanya hivyo? Basi kama ni progress wangempelekea Rais aliye watuma? Sisi tunataka report kamili yenye mapendekezo yaliyo tulia kama ile ya kina Mwakyembe!
 
Tuwe 'Optimistic'. Kama sikosei, JK aliipa tume/kamati kazi ya kuchunguza hili na kuhakikisha 1. Fedha zilizoibwa zinarudi, na 2. kuwachkulia hatua wote walihusika na wizi huo wa fedha za umma. Fedha kuanza kurudi kwa 'wenyewe' ni hatua nzuri, na bila shaka hatua hii itafuatiwa na kufikishwa katika sheria wahusika. Huenda kuanza kuwachukulia hatua mapema kutaharibu ushahidi au kuzorotesha upatikanaji wa fedha zetu.

Ni fedha kiasi gani zimerudi? Out of what? Ni kina nani waliorudisha? Ni wangapi hawajarudisha na kwa nini? Taarifa kuwa wengine wamekimbia nchi au wanakimbia nchi wakati huu uchunguzi unaendelea zinajaliwa katika haya? Kama haya maswali kwako si ya msingi basi sina haya ya kuwa optimistic!
 
yaani wamerudisha mali ili yaishe kimya kimya. Basi si waambiwe tu warudishe mali yaishe. Maana kutakuwa na umuhimu gani wa kuwafikisha mahakamani wakati wamesharudisha mali?

hili ni swali kubwa Mwanakijiji, yaani kama watuhumiwa wote wa wizi Tanzania wangekuwa wanapewa nafasi ya kurudishwa walichokwibwa nadhani jela na selo nyingi zingekuwa tupu bila wafungwa!
 
Hii story inatia mashaka. Kamati imepata wapi hiyo nguvu ya kurudisha mali???? Anyaway, ngoja tusubili hiyo ripoti kama kweli itatoka!!!
 
Usanii mwingine hata unavuka maelezo ya kawaida. Yaani ni lini sheria za nchi zilibadilishwa na kuruhusu watuhumiwa wa wizi kurudisha mali na sio kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.

Ina maana leo wale watuhumiwa wa wizi wa kuku na simu walioko Keko wanaruhusiwa kuachiwa huru as longer as wanarudisha kile walichoiba?

Mwafrika wa Kike,

Pole mama yangu, sheria mpya ya PCCB inaruhusu hivyo ova.
 
Back
Top Bottom