Mpwa wa Rais Magufuli autaka uenyekiti UVCCM taifa

Baada ya kusoma hii post nimeamini ninayoyasikia ni ukweli mputu. Huyu anayepigiwa debe Kheri James, alikuwa DAS, aliondolewa kwa miongoni mwa wale fyeki, 12,000, kwa kufyoji vyeti. Pia kwa tuhuma za USHOGA, wanaomkaza/bwana zake ni Antony Mtaka, mkuu wa mkoa wa Simiyu na John Kayombo, mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo. Wote wanazunguka huko mikoani kutoa rushwa ili Huyu sshoga achaguliwe, pia anapigiwa chapuo na shoga mwenzake Shaka.
Chama chetu hawa wenye makandokando ndo hupitishwa na kuondoa wenye misimamo mikali, huyu Khery James ni shoga hii kila mtu anajua sio siri hata kwenye interview Dodoma huyu mme wake Kayombo alikuwepo akitoa rushwa
 
Kuna ubaya gani!? Mbona mkwe wa muasisi wa Chadema ndio Mwenyekiti wa kudumu Chadema (Taifa)!
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Duuuh hadi uchaguzi wa ndani figisu figisu, sasa chaguzi nyingine zitaachaje kuwa na figisi
 
Chama Cha Mapinduzi kimekamilisha mchakato wa uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho na jumuiya zake. Masikio na macho ya wengi ni kwenye jumuiya ya vijana ndani ya chama hicho. Mpaka sasa walioteuliwa ni Musa Mtoro kutoka kusini mwa Tanzania, huku Kheri James, Mathias Saimon Kipara na Thobias Richard Mwesiga wote wanatoka kanda ya ziwa; Mganwa Nzota na Kamana Juma Simba hawa ni kutoka Dar es Salaam; Mwingine ni Juma Boaz Mwaipaja kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini mwa Tanzania.

Duru za siasa zinasema uteuzi wa majina haya umewaacha wengi midomo wazi hususani kupitishwa kwa Ndg Mathias Saimon Kipara ambaye analalamikiwa kudanganya umri kwani wengi wanaomfahamu wanasema amezaliwa mwaka 1984 hivyo kuwa na miaka 33 wakati kwa mujibu wa kanuni ya UVCCM mgombea awe na umri usiozidi miaka 30.

Chanzo changu cha uhakika kutoka ndani ya kamati kuu ya CCM na moja ya maafisa usalama Ikulu ni kuwa Ndg. Kipala hakupendekezwa na vikao vyoye vya awali pamoja na taarifa ya vyombo vya usalama kutokana na kutokuwa na sifa lakini Rais Magufuli aliingia na jina hilo kwenye kamati kuu kwa kulazimisha kuwa naye ajumuishwe kwenye orodha jambo ambalo wajumbe walilipokea kwa shingo upande. Rais Magufuli alionekana kukerwa na mhusika kutokuwepo katika mapendekezo wahusika wanadai ni kwa sababu Ndugu Kipala ni mpwa wake na mtumishi wa idara ya usalama wa Taifa maarufu kama “SWEEPER.”

Habari za uhakika ni kuwa tayari maelekezo yamekwishatoka kuhakikisha Ndugu Kipala anashinda. Jukumu hili linaongozwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul Makonda ambaye hata hivyo ushahidi wa sauti iliyorekodiwa wakati wa mkutano wake na marais wa serikali za wanafunzi wa vyuo vikuu mkoa wa Dar es salaam alithibitisha hilo kuwa yeye anamuunga mkono Ndugu Kipala. Mkakati ni kuwa baada ya kura kupigwa siku ya mkutano mkuu wa UVCCM TAIFA Dodoma wajumbe watapewa mapumziko huku kura zikihesabiwa na meza yaani wasimamizi wa uchaguzi huku wagombea wakitakiwa kuamini meza kurahisisha mchakato wa kumsaidia Ndugu Kipala. Watoa habari wameonya wajumbe wasikubali kura zikaondoka ukumbini bila wao, zikahesabiwa na wasimamizi pia wajumbe wasikubali kwenda mapumziko ndio warudi kumchagua makamu mwenyekiti wa UVCCM TAIFA.

Waliosoma na kumfahamu Ndugu Kipala wanadokeza kuwa Ndugu Kipala ni mpwa wa Rais Magufuli kama anavyojinasibu wakati akiwa amepata kilevi lakini pia ni mzinzi na mlevi aliepindukia kama alivyo Mwenyekiti wa UVCCM anaemaliza muda wake.

Hivyo basi kwa mtazamo wangu namuona kijana Kheri James kutoka Mwanza ambaye ni katibu wa mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe Angelina Mabula ambaye ni naibu waziri wa ardhi kuwa mtu sahihi kwa sasa kuiongoza jumuiya hii. Nimefarijika sana kuona watu makini kama kaka yangu Antony Mtaka mkuu wa mkoa wa Simiyu akiungana na kijana huyu anayesubiri kukabidhiwa ofisi. Mwenyezi Mungu amuongoze vyema.

Mjukuu wa Dr. Shika.
Igoma Mwanza.
Wivu wa kike
 
Mpeni kipara uenyekiti wa UVCCM labda atajaribu kuifufua Ambiance Club pale mwenge( Nafikiri mshaelewa).. DC aliifunga kwa kuwa alidhulumiwa penzi pale
 
Aisee kama ni kweli basi ngozi nyeusi ina laana yaani mijitu inawaza kupeana favours za uongozi tu hivi hatujifunzi kwa Mugabe ,huyu mzee angeweza hata kufia madarakani but the only worst mistake that the poor old man did was an attempt of power transfer to his wife .
 
Mijitu imevimbisha mitumbo na mashavu tu kwenye gari na ofisi za serikali ,yaani kuna mambo yanakera na kwa kweli kama watanzania hatutapambana tukapata katiba mpya tutaendelea kushuhudia upuuzi wa Karne katika nchi yetu .Mchawi hapa ni katiba tu

Hivi li jitu kama hili unatarajia nini kizuri kitatokea likishapata madaraka hayo ambayo linapigiwa promo sasa hivi?
 
Ana haki. Mtanzania na umri unatosha. Hakuna shida ni safi sana. Na kama DNA ni sawa ndio mzuri sana
 
Eti SWEEPER hahahaha wabongo punguzeni kula carbohydrates. Wananchi tunataka uchumi mifukoni na sio James Bond movies.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom