Zulqarnayn
Senior Member
- Oct 17, 2011
- 107
- 50
Kesho asubuhi kuanzia saa moja kamili asubuhi wabunge wawili wa kamati ya kudumu ya bunge ya huduma za jamii, mh Dkt Hamis Kigwangalla (CCM) na Mh Dkt Hussein Ali Mwinyi ambaye ni mb na waziri wa afya kwenye serikali ya jamhuri ya muungano wa tanzania watakuwa kwenye kipindi cha tuongee asubuhi kinachorushwa na kituo cha Star TV kutokea bungeni dodoma wakijadili sakata la mgomo wa madaktari. kila jumanne, star TV hurusha topic inayohusiana na mambo ya afya ya jamii. kipindi hiki huwa ni laivu na hivyo watazamaji mnaweza kuuliza maswali na kutoa michango yenu moja kwa moja