Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
MBUNGE wa Kasulu Magharibi, Kilontsi Mporogomyi (CCM), leo anatarajiwa kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya Dodoma kwa tuhuma za kusababisha kifo baada ya kumgonga mtembea kwa miguu na gari lake hadi kufa.
Mbunge huyo, ambaye alikuwa akiendesha mwenyewe, anadaiwa kumgonga mtu mwenye jinsia ya kiume ambaye jina lake halikupatikana mara moja anakadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 28 na 30.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Steven, aliiambia Tanzania Daima ofisini kwake mjini hapa jana, kuwa ajali hiyo ilitokea usiku wa kuamkia jana, majira ya saa 5:30 usiku katika eneo la Wajenzi mjini hapa.
Alisema, mbunge huyo alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili, T 288 ASJ, ambapo alimgonga mtu na kumsababishia mauti papo hapo kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata sehemu mbalimbali za mwili.
Mbunge huyo, ambaye alikuwa akiendesha mwenyewe, anadaiwa kumgonga mtu mwenye jinsia ya kiume ambaye jina lake halikupatikana mara moja anakadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 28 na 30.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Steven, aliiambia Tanzania Daima ofisini kwake mjini hapa jana, kuwa ajali hiyo ilitokea usiku wa kuamkia jana, majira ya saa 5:30 usiku katika eneo la Wajenzi mjini hapa.
Alisema, mbunge huyo alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili, T 288 ASJ, ambapo alimgonga mtu na kumsababishia mauti papo hapo kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata sehemu mbalimbali za mwili.