Nkerejiwa
Senior Member
- Feb 25, 2014
- 146
- 214
MPINA AMEAMUA KUWA MZABIBU MWITU AU AMEFIKA BEI KWA MAFISADI?
Niko kwenye mfungo wa mwezi mkukufu wa Ramadhani, wakati alasiri inayoyoma kuelekea magharibi nimeketi kwenye uwa wangu nikisikiliza vikao vya Bunge letu tukufu, nimesikia mambo ambayo sikupendezwa nayo kabisa kutoka kwa baadhi ya wachangiaji, hapa namzungumzia Luaga mpina.
Kabla ya kutoa hoja yangu, kwanza nimuulize Luaga Mpina, una chuki binafsi na Mh Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba? Kwanza nikuulize, Je, alishawahi kukuchukulia mkeo au demu wako? Kama lau si hivyo, Luaga Mpina umepatwa na muwasho gani kumsakama kiasi kile Mwigulu Nchemba kwa makosa ambayo dhahiri si yake? na sio mara yako ya kwanza, kwa hoja zilezile, hii haiwezi kuwa bahati mbaya! There's something behind.
Sitaki kuamini Mpina amekosa akili kiasi hiki, sitaki kuamini Mpina alikuwa amelewa au Mpina au bado ana Stress na kuchapiwa Mkewe na vijana wa mjini, ingawa hii leo si mada tutazungumza siku nyingine. Ila, ukiwa kama Mbunge na mtu ambaye ulishawahi kuwa Waziri lakini umezungumza upuuzi bila kufanya tafakuri.
Nianzie wapi?
Mpina analalamika juu ya ubadhirifu uliofanywa na Wizara za kisekta zikiwemo Wizara ya Nishati na Uchukuzi juu ya utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya SGR na JNHPP. CAG ameonesha uchafu na ufisadi mkuwa wa wizara hizo, lakini Mpina akajivika upofu na kutupa lawama kwa Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba. Au ndio huko kuwashwa ninakozungumzia? Kama sio kuwashwa tuite nini sasa.
Mwigulu Nchemba kama Waziri wa Fedha anahusika kwenye masuala ya mikataba ya kukusanya na kutoa fedha, Waziri wa fedha hausiki hata senti moja kipande na mikataba ya wizara ya uchukuzi wala nishati, hausiki na zabuni zao, na ununuzi wa jambo lolote. Kama wizara hizo ambazo zina mawaziri wake, walikaa chini wakaona gharama za bidhaa fulani ziko sawa, wakaidhinisha malipo kwa kuzingatia maslahi ya nchi, kazi ya hazina ni kulipa tu, wala haihusiki na kitu kingine, sasa mlitaka Mwigulu azuie hayo manunuzi, ili mseme anakwamisha maendeleo? sijapenda.
Huwezi kusema eti “Waziri wa Fedha amekwenda kukopa bila idhini ya Bunge”, yani umelenga Waziri moja kwa moja na ukasahau kabisa kwamba Waziri yeye ni mwakilishi wa Rais na Serikali yake. Mwigulu katu hawezi kutoka huko kwao Makunda akaenda hadi Brussels, NewYork au London kwenda kukopa, hawezi. Ila Mwigulu kwa niaba ya serikali, kupitia yeye kama Waziri mwenye dhamani husaini mkopo au msaada wa nchi kwa niaba yetu, utasemaje eti “Waziri wa Fedha amekwenda kukopa”.
Sheria ya Mikopo na Amana za Serikali (CHAPTER 134
THE GOVERNMENT LOANS, GUARANTEES AND GRANTS ACT) haitoi ulazima wa bunge kuambiwa kuhusu kila mkopo ambao serikali inaingia/inatafuta.
Waziri wa Fedha anawajibika kwa kamati ya kitaifa ya madeni ambayo ndiko anatakiwa kutoa taarifa ya wapi anakopa na ifanyike tathmini ya masharti ya mkopo husika.
2. Hakuna mahala CAG ameonesha kuna ukiukwaji wa sheria hii ambayo ndo basis ya Mikopo ya nchi so ni headless argument vilevile.
Okay tuendelee, hivi kwani anakopa kwa ajili ya familia yake? Hapa Mpina hukuteleza, ulifanya kusudi kwa lengo la kumchafua Mwigulu kwa mtaji wa kisiasa wa waliokutuma na tunawajua, hadi hotel uliyopokea fungu tunaifahamu, hilo liko wazi. Kwa uzoefu ulio nao ni aibu kwa mtu kama wewe kuongea kiwango hiki cha samadi. Ita Press omba radhi, maneno uliyotamka kama hutoomba radhi yatakuja kukutafuta, malipo ni hapa hapa duniani.
Mwisho lakini sio kwa umuhimu, umeona hadi Bunge limefuta kauli zako kwenye hansadi ya Bunge hadi pale ripoti ya kamati ya PAC itakapotoka baada ya serikali kujieleza kutokana na siku walizopewa na Bunge. Umezungumza maneno ya uwongo, yenye ubazazi, umaimai na uzandiki wa hali ya juu. Mpina ndugu yangu kumbuka njia unaipanda miiba leo na kutupa mabale ya chupa, iko siku utaitumia kurudi, ukiwa peku na huyu unayembagaza kwa mabaya leo, ndio atakuwa mtu pekee wa kukusaidia.
By: Saidi Mgeta
Mkali wa Hizi Kazi
Makorora, Tanga.
Niko kwenye mfungo wa mwezi mkukufu wa Ramadhani, wakati alasiri inayoyoma kuelekea magharibi nimeketi kwenye uwa wangu nikisikiliza vikao vya Bunge letu tukufu, nimesikia mambo ambayo sikupendezwa nayo kabisa kutoka kwa baadhi ya wachangiaji, hapa namzungumzia Luaga mpina.
Kabla ya kutoa hoja yangu, kwanza nimuulize Luaga Mpina, una chuki binafsi na Mh Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba? Kwanza nikuulize, Je, alishawahi kukuchukulia mkeo au demu wako? Kama lau si hivyo, Luaga Mpina umepatwa na muwasho gani kumsakama kiasi kile Mwigulu Nchemba kwa makosa ambayo dhahiri si yake? na sio mara yako ya kwanza, kwa hoja zilezile, hii haiwezi kuwa bahati mbaya! There's something behind.
Sitaki kuamini Mpina amekosa akili kiasi hiki, sitaki kuamini Mpina alikuwa amelewa au Mpina au bado ana Stress na kuchapiwa Mkewe na vijana wa mjini, ingawa hii leo si mada tutazungumza siku nyingine. Ila, ukiwa kama Mbunge na mtu ambaye ulishawahi kuwa Waziri lakini umezungumza upuuzi bila kufanya tafakuri.
Nianzie wapi?
Mpina analalamika juu ya ubadhirifu uliofanywa na Wizara za kisekta zikiwemo Wizara ya Nishati na Uchukuzi juu ya utoaji wa zabuni ya ujenzi wa reli ya SGR na JNHPP. CAG ameonesha uchafu na ufisadi mkuwa wa wizara hizo, lakini Mpina akajivika upofu na kutupa lawama kwa Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba. Au ndio huko kuwashwa ninakozungumzia? Kama sio kuwashwa tuite nini sasa.
Mwigulu Nchemba kama Waziri wa Fedha anahusika kwenye masuala ya mikataba ya kukusanya na kutoa fedha, Waziri wa fedha hausiki hata senti moja kipande na mikataba ya wizara ya uchukuzi wala nishati, hausiki na zabuni zao, na ununuzi wa jambo lolote. Kama wizara hizo ambazo zina mawaziri wake, walikaa chini wakaona gharama za bidhaa fulani ziko sawa, wakaidhinisha malipo kwa kuzingatia maslahi ya nchi, kazi ya hazina ni kulipa tu, wala haihusiki na kitu kingine, sasa mlitaka Mwigulu azuie hayo manunuzi, ili mseme anakwamisha maendeleo? sijapenda.
Huwezi kusema eti “Waziri wa Fedha amekwenda kukopa bila idhini ya Bunge”, yani umelenga Waziri moja kwa moja na ukasahau kabisa kwamba Waziri yeye ni mwakilishi wa Rais na Serikali yake. Mwigulu katu hawezi kutoka huko kwao Makunda akaenda hadi Brussels, NewYork au London kwenda kukopa, hawezi. Ila Mwigulu kwa niaba ya serikali, kupitia yeye kama Waziri mwenye dhamani husaini mkopo au msaada wa nchi kwa niaba yetu, utasemaje eti “Waziri wa Fedha amekwenda kukopa”.
Sheria ya Mikopo na Amana za Serikali (CHAPTER 134
THE GOVERNMENT LOANS, GUARANTEES AND GRANTS ACT) haitoi ulazima wa bunge kuambiwa kuhusu kila mkopo ambao serikali inaingia/inatafuta.
Waziri wa Fedha anawajibika kwa kamati ya kitaifa ya madeni ambayo ndiko anatakiwa kutoa taarifa ya wapi anakopa na ifanyike tathmini ya masharti ya mkopo husika.
2. Hakuna mahala CAG ameonesha kuna ukiukwaji wa sheria hii ambayo ndo basis ya Mikopo ya nchi so ni headless argument vilevile.
Okay tuendelee, hivi kwani anakopa kwa ajili ya familia yake? Hapa Mpina hukuteleza, ulifanya kusudi kwa lengo la kumchafua Mwigulu kwa mtaji wa kisiasa wa waliokutuma na tunawajua, hadi hotel uliyopokea fungu tunaifahamu, hilo liko wazi. Kwa uzoefu ulio nao ni aibu kwa mtu kama wewe kuongea kiwango hiki cha samadi. Ita Press omba radhi, maneno uliyotamka kama hutoomba radhi yatakuja kukutafuta, malipo ni hapa hapa duniani.
Mwisho lakini sio kwa umuhimu, umeona hadi Bunge limefuta kauli zako kwenye hansadi ya Bunge hadi pale ripoti ya kamati ya PAC itakapotoka baada ya serikali kujieleza kutokana na siku walizopewa na Bunge. Umezungumza maneno ya uwongo, yenye ubazazi, umaimai na uzandiki wa hali ya juu. Mpina ndugu yangu kumbuka njia unaipanda miiba leo na kutupa mabale ya chupa, iko siku utaitumia kurudi, ukiwa peku na huyu unayembagaza kwa mabaya leo, ndio atakuwa mtu pekee wa kukusaidia.
By: Saidi Mgeta
Mkali wa Hizi Kazi
Makorora, Tanga.