Mpiga chapa mkuu kwanini bado yuko ofisini?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
Kama , mkurugenzi wa ilala. Aliposema jana kosa ni la ofisi ya mpigachapa Mkuu

Basi nilitarajia by saa sita mchana angekuwa amejiuzulu

Najiuliza

Gharama za makaratasi yaliokosewa nchi nzima nani awajibike huu ni upuuzi na uzembe mgombea wa CHADEMA uandike nafasi ya CCM huu ni wehu.
 
uwajibikaji ni msamiati mgumu sana kwa viongozi wa tanzania.
 
Kumbe tuko wengi tunaoshangazwa na hali hiyo yani afadhali ingekuwa makosa hayo ni kwa vijiji/mitaa michache lakini hii hali imetokea sehemu nyingi tu...kali kuliko yote pale mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala aliposema walirekebisha hayo makosa ila ilipopelekwa tena kwa mpiga chapa akachapa softcopy ileile yenye makosa.............mimi nikaenda mbali zaidi na kujiuliza pasipo kuwa na jibu hivi vifaa vinapoisha ilhali idadi ya wapiga kura inafahamika ina maana Serikali huwa haijiandai?
 
Back
Top Bottom