- Thread starter
- #21
FactsDah kanikeraaaaaa watu wengine ni wachoyo by nature, wanapenda kutumia vya wengine, vya kwao visiguswe.
Mm roho yangu ya huruma ndio inaniponzaga Siku zote, MF. Mpz / rafiki tu aniombe hela siwezi mwambia hata kama sina naanza kujaribu kukopa kwa mashoga zangu labda hata huko nukose ndo ntaweza kumwambia sina,
Ingawa huwa Nina mkosi wa pesa yaani ikitokea nikakosa pesa nikamkopea MTU hata kwenye chama hili arudishe, huwa hawanirudishiagi na ikitokea bahati mbaya akarudisha basi ntakuwa nishabebeleza mwaka mzima, ntarejesha hiyo hela mwanzo mwisho loh!
Mleta Mada huyo Dada ndani ya hiyo miaka 4 kama hajawahi kukusaidia wakati wa shida, nakuhakikishia hawezi kubadilika, tena ukimuoa ndio kabisaaaa.
Labda nijue kitu kimoja, huwa anakununuliaga hata zawadi? Kama yeye kwake hakunaga -, kwake + tu achana nae, bora MTU akunyime kitu ujue hana ila unajua na anayo kakunyima? Loh.
Nb. Ukiona hupewi wewe jua kuna mwenzio anapewa hii ni kwa jinsia zote.