Mpenzi wangu hataki kunielewa na yupo tayari kuachana na Mimi kisa mtumishi mwenzie

Mpatuka

JF-Expert Member
Nov 15, 2015
1,711
2,494
Mimi ni kijana, mwenye kila sababu ya kuwa na mke kwa umri wangu, lakini kutokana na changamoto za kimaisha nimejikuta nachelewa mpaka muda huu nipo kwenye mahusiano tu. Nimepitia mahusino kadha wa kadha lakini kwa huyu binti niliyenaye sasa nahisi tunaweza kufikia lengo hasa lakuwa mwili mmoja, kilichonifanya kuanzisha uzi huu na kuhitaji maoni toka kwa wadau kwenye jukwaa hili ni mazingira ya mimi na huyu bibie.

Huyu binti yupo wizarani mkoa x kama data clerk na mm nipo mkoa x kama researcher. Anadai ananipenda sana nami niwe muwazi nampenda pia tena sana, changamoto ni yeye anadai kutokana na ugumu wa maisha hasa kwenye nyumba za kupanga amepata kijana mmoja anadai wachukue nyumba nzima waishi pamoja.

Huyo kijana kipindi cha nyuma alishawahi kumtaka kimapenzi na mimi nilishirikishwa na mpenzi wangu na sms nikaoneshwa. Baada ya kupokea taarifa hizo nikakataa kabisa kuwa mpango huo siyo salama kwa mapenzi yetu, lakini jambo la kushangaza huyu mpenzi wangu amesisitiza kuwa anajielewa na wala hakuna shida yoyote ile.

Nilipoonesha msimamo wangu kuwa sitaki hilo litokee ameninunia na amani hakuna mpaka muda huu. Hivyo basi naombeni ushauri wenu wadau nifanye uamuzi gani katika hili.
 
Maisha ya ndoa na kumpata mke mzuri hayana formula. Huko ulipo tongoza tongoza unaweza pata mke maana mapenzi ni betting. Hapo hauna mke.
Muda siyo mrefu, huyo mchumba wako anayedai anakupenda sana anakuja kukutegeshea mimba.
Huyo jamaa anamla demu wako 100% halafu hakuna urafiki wa jinsia ya KE na ME ambao siyo ndugu waishi nyumba moja. Hao wanakulana.
Ikifika kipindi mwanaume unabidi utumie akili. Jiandae kulea watoto siyo wako
 
nimejitoa sana kwa huyu binti hata anapoishi sasa mimi ndiye niliyempangia na kodi nimelipa mimi. Sasa nachofikiria nikutoa uhai wa mtu muda si mrefu maana kuna mambo hayavumiliki
Yani ukajipe kesi ya mauaji kisa kiumbe ambacho mmekutana ukubwani tu? Acha ujinga, mpotezee uanze maisha mapya. Kwani bila ya yeye huendi haja kubwa au hupumui?
 
Huyo jamaa ameshamla huyo manzi hapo huna chako , kama kweli mtu ana kupenda Hawezi kung'ang'ania kukuweka ktk mazingira yanayo kupa wasi+ hofu na mashaka kwaajili yake Mtu anaye kupenda Hawezi kukubali kuwa sehemu ya kuku kosesha furaha ilhali anajua kuwa kufanya hivyo ni makosa na ana kuumiza

Ingekuwa Mimi ndiye wewe hiyo ndio ingekuwa ndio ticket ya kuachana nae , huyo Kesha liwa na jamaa na mapenzi yame mlevya , pindi linapo kujaga swala la nyege hakunaga mtu anaye jielewa,

so asikuhadae kuwa ana jielewa na hatoweza kumpa papa huyo jamaa, huo ni utetezi wa kipumbavu,

Pole sana
 
Unataka kufia jela kwa sababu ya mwanamke uliyekutana ukubwani? Huenda wewe ni wa 7 hata wa 10 kwa watu waliolala na huyo mwanamke.

Angalia maisha yako, hauna mtoto halafu unataka kuzua mabalaa mengine. Wanawake ndiyo walivyo cha msingi acha kuwekeza kwa mwanamke. Huyo mwanamke angekuwa anajilipia chumba mwenyewe.

Acha tabia ya kuwa na mwanamke mmoja ndiyo matokeo yake haya. Mapenzi ni betting unatakiwa u-bet hata mikeka 5 lazima kuna mmoja utatitiki tu kwahiyo ukibet mmoja ukichanika ndiyo matokeo yake haya

nimejitoa sana kwa huyu binti hata anapoishi sasa mimi ndiye niliyempangia na kodi nimelipa mimi. Sasa nachofikiria nikutoa uhai wa mtu muda si mrefu maana kuna mambo hayavumiliki
 
nimejitoa sana kwa huyu binti hata anapoishi sasa mimi ndiye niliyempangia na kodi nimelipa mimi. Sasa nachofikiria nikutoa uhai wa mtu muda si mrefu maana kuna mambo hayavumiliki
Shukuru Mungu amekuonyesha aina ya mwanamke uliyetaka kumuoa.
Amekosa kujiheshimu na kukuheshimu mapema mno. Ukweli ni kwamba asingethubutu hata kukuambia juu ya huo mpango kwa sababu huyo jamaa alishamtongoza na ilipaswa aweke umbali nae. Kukaa/kupanga nae nyumba moja inaonyesha aidha wameanza mahusiano au amevutiwa kihisia na huyo mtumishi.


Kimbia bro'
 
Mimi ni kijana, mwenye kila sababu ya kuwa na mke kwa umri wangu, lakini kutokana na changamoto za kimaisha nimejikuta nachelewa mpaka muda huu nipo kwenye mahusiano tu. Nimepitia mahusino kadha wa kadha lakini kwa huyu binti niliyenaye sasa nahisi tunaweza kufikia lengo hasa lakuwa mwili mmoja, kilichonifanya kuanzisha uzi huu na kuhitaji maoni toka kwa wadau kwenye jukwaa hili ni mazingira ya mimi na huyu bibie.

Huyu binti yupo wizarani mkoa x kama data clerk na mm nipo mkoa x kama researcher. Anadai ananipenda sana nami niwe muwazi nampenda pia tena sana, changamoto ni yeye anadai kutokana na ugumu wa maisha hasa kwenye nyumba za kupanga amepata kijana mmoja anadai wachukue nyumba nzima waashi pamoja.

Huyo kijana kipind cha nyuma alishawahi kumtaka kimapenzi na mimi nilishirikishwa na mpenzi wangu na sms nikaoneshwa. Baada ya kupokea taarifa hizo nikakataa kabisa kuwa mpango huo siyo salama kwa mapenzi yetu, lakini jambo la kushangaza huyu mpenzi wangu amesisitiza kuwa anajielewa na wala hakuna shida yoyote ile.

Nilipoonesha msimamo wangu kuwa sitaki hilo litokee ameninunia na amani hakuna mpaka muda huu. Hivyo basi naombeni ushauri wenu wadau nifanye uamuzi gani katika hili.
Wewe ni wale wanaume wenye mawazo "nitaoa mwanamke wa kusaidia maisha" ndio maana umemkimbilia anaefanya kazi "wizarani" ?! ok swadaktaaaa mambo naweza kukushauri kupanga ni kuchagua.

1. Kubali kua mwanaume itikia itikia, hauna kauli wala maoni yako weka kando, kiongozi wa familia weka kando, Kichwa na maalaka ya familia weka kando, utachapiwa huyo mke na mawivu weka kando.
2. Kubali na kua tayari kuishi kwa fedhea na dhihaka.

Mwanamke mwenye kiajira hawezi kamwe kukuheshimu, ataigiza igiza tu kwa vipindi fulani ila ukweli KAMWE hatakuheshimu. Mtaishi kwa mivutano sana na mara zote you will be the looser.

Ona hata hapo umemkataza kuishi nyumba moja na mwanaume mwingine ambayo kweli kimaadili sio sawa lakini kakudindia na hakuna kitu unaweza kufanya na huyo jamaa anamtafuna haswa mpaka kanogewa and nigga you can't do a thing a bout it.
 
Back
Top Bottom