Mpenzi wangu ananishauri nitoe mimba, hana uwezo wa kulea

Anaonekana anaogopa kulea bila baba ndio maana anataka wale wanaochukia single moms wampe ushauri.
Anataka kuzaa ila hajielewi
aya nimaisha yake hapaswi kuwaza watu watasema nini juu yake akiwasikiliza watu atakosa vyote watu hao hao wataanza mbana haolewi angekuwa na mtoto tu wakati umli umeshakata
Bai ze wei usingle mother uko mitandaoni nimeudhuria harusi nyingi tu jamaa wameoa mabinti wsliokwisha zaa
 
Sasa miaka 29 na unakazi nzuri tu unawasiwasi gani dada yetu. Lea mtoto huwezi jua una mayai mangapi uliyoandikiwa na mungu. Huyo mtu asije kukupa kidonda cha majuto baadae. Wenzenu tunatafuta watoto hatuwapati huku ohoo!!
 
Ujue hata kutoa ushauri inategemea na mshauriwa yukoje ufikiri wake.
1) Ni dereva bajaj (Probably younger than you) , na keshasema kabisa uwezo wa kulea hana na hataki kuwa na mtoto na wewe. What the hell were you doing with him in the first place??? Hivi watoto mnawachukuliaje? Like unaeza beba na kutoa tu mimba? Kwa starehe ya week mbili?

2) Wiki mbili uko na mtu ambaye anapitisha tu mda, na mimba ukabeba?

Kama maneno ya bwana wako dereva bajaj hukuyasikiliza, utakuja kutusikiliza sisi?
 
nadhani jamaa hana maamuzi ya kukwambia utoe au usitoe kwa sababu tangu mwanzo alishasema hajiwezi. wewe ilibidi ujue tangu siku hio kwamba ukibeba mimba hilo ni juu yako.

Maswali ya kujiuliza wewe mwenyewe

1. Je, unahitaji mtoto kwa sasa?
2. una uwezo wa kumlea bila usaidizi kutoka kwa baba yake?

hapo ndio utajua kama uitoe au usiitoe.
Kumbuka, uamuzi wa kuitoa au kutoitoa ni wa kwako kwasababu jamaa alishasema asihusishwe pindi utakapopata mimba.
Usimlaumu kabisa utamtendea dhambi, alishakupa tahadhali.
 
Unataka kuwa muuaji? Kama jibu ndio basi toa hiyo mimba. Kama hapana basi leo mimba.

Huwezi jua huyo mtoto anaweza kuja kuwa profesa akatusaidia kupunguza ujinga wa watanganyika.
 
Mimi nina Mika 29 ninafanya kazi nzuri tu. Ila sasa nikawa sinamtu mda mrefu nikajikuta natuliza miwasho kwa Dereva mmoja wa bajaji.

Sasa swala linakuja kuwa tumedumu kwa muda wa mwezi na Sasa nimegundua ni mjamzito wa week mbili. Kwanzia mwanzo kabisa siku ya Kwanza aliniambia usije beba mimba yangu kua hawezi kulea Saiv.

Nimemwambia juu ya ujauzito anasema nitoe yeye hataki kulea kwani anamtoto mmoja na anashindwa kuhudumia....

Je mnanishaurije?

Miaka 29 unashauriwa kutoa mimba halafu inakuingia akilini!!? Wapo wanawake wenye umri kama wako wanashinda makanisani, kwa mashekhe na kwa waganga kutafuta mtoto
Huyo dereva bajaji atakua na mtu wake au hana mpango na wewe....tumia hiyo kazi yako nzuri lea mimba......
 
Kama hana uwezo wa kulea, pambana huwezi jua umembeba nani. Na usikute ndio ujauzito wa kwanza na ukitoa usije kubeba tena. Acha yoga wa maisha. Komaza akili.
 
Mimi nina Mika 29 ninafanya kazi nzuri tu. Ila sasa nikawa sinamtu mda mrefu nikajikuta natuliza miwasho kwa Dereva mmoja wa bajaji.

Sasa swala linakuja kuwa tumedumu kwa muda wa mwezi na Sasa nimegundua ni mjamzito wa week mbili. Kwanzia mwanzo kabisa siku ya Kwanza aliniambia usije beba mimba yangu kua hawezi kulea Saiv.

Nimemwambia juu ya ujauzito anasema nitoe yeye hataki kulea kwani anamtoto mmoja na anashindwa kuhudumia....

Je mnanishaurije?
Kwahiyo atakuwa maskini hadi kufa? Huyo ni mpita njia... Jiongeze... Mimba ingetakiwa kuwa chanzo cha muunganiko mpya....
 
Mimi nina Mika 29 ninafanya kazi nzuri tu. Ila sasa nikawa sinamtu mda mrefu nikajikuta natuliza miwasho kwa Dereva mmoja wa bajaji.

Sasa swala linakuja kuwa tumedumu kwa muda wa mwezi na Sasa nimegundua ni mjamzito wa week mbili. Kwanzia mwanzo kabisa siku ya Kwanza aliniambia usije beba mimba yangu kua hawezi kulea Saiv.

Nimemwambia juu ya ujauzito anasema nitoe yeye hataki kulea kwani anamtoto mmoja na anashindwa kuhudumia....

Je mnanishaurije?
Pole sana.

Kosa la awali ni kukutana kimwili kabla ya kukamilisha taratibu.Ni kosa ambalo dini zote na mila haliruhusu.Inahitaji taratibu ya msamaha wa Mungu wako.

Pili,jaribu kuwaza huyo unayetaka kumtoa (kukatisha uhai wake) ni binadamu kama wewe (na si ajabu atakayekuja kuwa bora zaidi yako ama yetu sote) ambaye, si ajabu ndie kiumbe pekee utakayejaliwa.

Kutoa mimba ni ukatili usiomithilika.Infact,neno sahihi ni 'KUUA MWANANGU MWENYEWE NILIYEJAALIWA' kwa utashi,pesa na hiyari yangu tena kwa ubinafsi wangu na kutojali kwangu.
Umeshasema mwenyewe kuwa 'una kazi nzuri tu',je,hiyo haitoshi? Kukubaliwa na huyo mwanaume kuhusu malezi au wewe kuamua kumlea lipi ni jema na bora zaidi?

Kosa likishafanyika,lisifanyike kosa jingine(tena baya na kubwa zaidi) ili kulifuta au kusawazisha kosa la wali.
Huyo mtoto si ajabu ndio baraka yako ya pekee-hatuombei hilo.Nakuombea upate wengi utakavyo.Ila,nani ajuae mipango ya Mungu?Na hata ukiitoa ukaja kupata wengine,siku akili na moyo wako vikikaa sawa,utamkumbuka na huyo uliyemtoa na kujiuliza/kujilaumu kwa mengi.Ujana mara nyingine huwa una ujinga mwingi sana uliofichika,hadi utakapopevuka zaidi.

Tuwe na huruma.Haifai hata kufikiri hili la uuaji,hasa kiumbe ambeye ni too innocent,vulnerable na wanaotaraji upendo na ulinzi toka HASA kwa wanaowaleta humu duniani,yaani wazazi au mzazi,si vinginevyo.

Kuua kiumbe ambaye alishapitishwa na Muumba kuwa awepo duniani hai,nadhani pia ni kumpinga Mungu.Kuua kiumbe ambaye si ajabu angekuja kuyafurahia mno maisha yake na kuyapenda,ni sawa na kujiua mwenyewe.Kiumbe ambaye si ajabu ataleta maana,thamani,suluhisho na faraja kwa maisha ya wengi,pamoja na kwa wazazi wake.Kiumbe ambaye si ajabu maisha yake yatakuja kuwa ya maana na thamani zaidi hata kuzidi waliomzaa.

Please,usiitoe hiyo mimba!!!
 

Similar Discussions

8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom