Konakali
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 1,533
- 263
Mpenzi wangu, hali yangu ya kiafya sio nzuri, na hivyo muda wowote huenda nikatangulia na kuwaachia dunia hii; lakini mpenzi wangu kabla mapenzi ya Mwenyezi Mungu hayajatimia, ningeomba uniambie:
- Ni kitu gani kizuri nilichowahi kukufanyia katika uhai wangu, ambacho hautakaa usahau.....!
- Ni kitu gani kibaya nilichotokea kukufanyia kipindi cha mahusiano yetu, ambacho usingeweza kuisahau, na ningepaswa kupiga magoti unisamehe.....!
- Ni neno gani ungependa kuniambia kama neno la kuagana....!
- Ni nini unachokijua mwenyewe, ambacho ulinifanyia na sio kizuri, na hivyo ungependa nikusamehe kabla kifo hakijatutenganisha....!