Mpenzi wa zamani kaleta vurumai kumkuta mpenzi mpya

Hainaga ushemeji

JF-Expert Member
Aug 22, 2016
451
777
Wakuu natumai weekend zenu zipo poa, mi hapa nimechoka..hii weekend nilihisi itakua moja ya weekend nzuri sana lakini nimekuja kua weekend mbovu kabisa

Majuzi hii nlileta mkasa wa kumuacha huyu mtoto wa kitanga, hii ni baada ya kuanza mahusiano na binti mwingine, kutoa clarification tu maana Uzi ulijaa sana mapovu ule, ni kwamba wakati naanza mahusiano na huyu mtoto wa kitanga nilimueka wazi kua sipo tiari ku settle na mtu kwa sasa, yeye akadai we give it a try, so alikua anajua what she was walking into

Baada ya kasheshe za hapa na pale na kupelekana polisi hatimaye huyu binti wa kitanga akaja chukuliwa na Dada yake, nimejaribu kuwasiliana nae nione kama I can make her understand kwanini nlifanya maamuzi kama Yale lakini mawasiliano yakawa magumu ikiwa na pamoja na kunipa vitisho... SMS ya mwisho aliniandikia "kama unahisi unaweza kuniacha kirahisi rahisi, jipange tena" .. Mi nakaamua kumpotezea

Mapenzi na huyu binti mpya S yakawa motomoto,lakini nikawa sitaki kumleta kwangu maana nilikua naogopa huyu mtoto wa kitanga anaweza kuja kuleta maneno hapa, jana nimetoka na S baada ya matembezi tumeenda kulala hotelini, jambo ambalo hakulipenda hata kidogo,Leo akalazimisha ikabidi nimlete tu hapa kwangu, japo nae nlimueleza nilikua na mtu ila tumeamua kuachana!!!

Leo mchana nimepigiwa simu ya dharura ikabidi nitoke nimuache S hapa nyumbani, BIG MISTAKE!!! inavyoonyesha kuna huyu mdada apartment inayofuata anawasiliana na huyu mtoto wa kitanga, kaja hapa kaleta vurumai la hela yote yani...

S akawa ananipigia nikakata simu nikamwambia ntampigia nkipata nafasi, kuja kumcheki yani ata simuelewi, hatusikilizani yaani analia tu kwenye simu, nikapanic, nikamwambia atulie then anitumie sms, akani text "nipo njiani narudi kwangu, ex wako kaja, she is angry, crazy and VERY PREGNANT"

baada ya hapo akazima simu sijampata tena, huyo nkaenda mpaka nyumbani, nikamkuta huyu mtoto wa kitanga, chupa Lile la Drosthoff anakaribia kulimaliza na wakati navyojua mimi alikua hanywi... Tofauti na siku kama mbili tu ivi nlimshawishi anywe glasi moja..

Sikutaka ku panic,nikamsalimia then kumuuliza kulikoni... Dah yani huyu mtoto kama vile nilikua simjui yani, kacharuka sio kidogo na wakati anakuaga mpole sana... Anadai ana mimba yangu ya zaidi ya mwezi,na kaja na begi lake anadai haondoki hapa labda niondoke mimi.. Nikamuuliza mbona hajaniambia haya ya mimba tulivyokua wote akakaa kimya tu

Nikaona nisi panic hapa, nikaingia chumbani nikachukua documents zangu muhimu na nguo mbili tatu nikaweka kwenye gari nikaondoka zangu maana tumeshindwa kuongea kwa amani, nikapita kwa Mshkaj wangu nikaacha vitu nikaenda mpaka kwa S, nikamkuta na rafiki yake japo nimeshindwa kuongea nae, rafiki yake anadai nije kesho nimpe muda kwanza maana hayuko poa

Nikaona poa tu, nimepita polisi nikatoa ripoti kama tahadhari maana huyu mtoto wa kitanga nimemuacha simuelewi elewi its better nichukue tahadhari isije tokea majanga nikashindwa pa kuanzia...

Leo nlivyotoka home nilienda hoteli flani nikafanya reservation kwa ajili ya dinner na S, lakini ndo ivo mambo yamekuja kua hivi, nilishatoa advance na wamesema hawa refund mtu kwa cancellation, so npo hapa na Mshkaj wangu, midume miwili in a romantic place tunapiga dinner, what else can go wrong this weekend

Ngoja niagize bia hapa akili ikae sawa...
 
Wakuu natumai weekend zenu zipo poa, mi hapa nimechoka..hii weekend nilihisi itakua moja ya weekend nzuri sana lakini nimekuja kua weekend mbovu kabisa

Majuzi hii nlileta mkasa wa kumuacha huyu mtoto wa kitanga, hii ni baada ya kuanza mahusiano na binti mwingine, kutoa clarification tu maana Uzi ulijaa sana mapovu ule, ni kwamba wakati naanza mahusiano na huyu mtoto wa kitanga nilimueka wazi kua sipo tiari ku settle na mtu kwa sasa, yeye akadai we give it a try, so alikua anajua what she was walking into

Baada ya kasheshe za hapa na pale na kupelekana polisi hatimaye huyu binti wa kitanga akaja chukuliwa na Dada yake, nimejaribu kuwasiliana nae nione kama I can make her understand kwanini nlifanya maamuzi kama Yale lakini mawasiliano yakawa magumu ikiwa na pamoja na kunipa vitisho... SMS ya mwisho aliniandikia "kama unahisi unaweza kuniacha kirahisi rahisi, jipange tena" .. Mi nakaamua kumpotezea

Mapenzi na huyu binti mpya S yakawa motomoto,lakini nikawa sitaki kumleta kwangu maana nilikua naogopa huyu mtoto wa kitanga anaweza kuja kuleta maneno hapa, jana nimetoka na S baada ya matembezi tumeenda kulala hotelini, jambo ambalo hakulipenda hata kidogo,Leo akalazimisha ikabidi nimlete tu hapa kwangu, japo nae nlimueleza nilikua na mtu ila tumeamua kuachana!!!

Leo mchana nimepigiwa simu ya dharura ikabidi nitoke nimuache S hapa nyumbani, BIG MISTAKE!!! inavyoonyesha kuna huyu mdada apartment inayofuata anawasiliana na huyu mtoto wa kitanga, kaja hapa kaleta vurumai la hela yote yani...

S akawa ananipigia nikakata simu nikamwambia ntampigia nkipata nafasi, kuja kumcheki yani ata simuelewi, hatusikilizani yaani analia tu kwenye simu, nikapanic, nikamwambia atulie then anitumie sms, akani text "nipo njiani narudi kwangu, ex wako kaja, she is angry, crazy and VERY PREGNANT"

baada ya hapo akazima simu sijampata tena, huyo nkaenda mpaka nyumbani, nikamkuta huyu mtoto wa kitanga, chupa Lile la Drosthoff anakaribia kulimaliza na wakati navyojua mimi alikua hanywi... Tofauti na siku kama mbili tu ivi nlimshawishi anywe glasi moja..

Sikutaka ku panic,nikamsalimia then kumuuliza kulikoni... Dah yani huyu mtoto kama vile nilikua simjui yani, kacharuka sio kidogo na wakati anakuaga mpole sana... Anadai ana mimba yangu ya zaidi ya mwezi,na kaja na begi lake anadai haondoki hapa labda niondoke mimi.. Nikamuuliza mbona hajaniambia haya ya mimba tulivyokua wote akakaa kimya tu

Nikaona nisi panic hapa, nikaingia chumbani nikachukua documents zangu muhimu na nguo mbili tatu nikaweka kwenye gari nikaondoka zangu maana tumeshindwa kuongea kwa amani, nikapita kwa Mshkaj wangu nikaacha vitu nikaenda mpaka kwa S, nikamkuta na rafiki yake japo nimeshindwa kuongea nae, rafiki yake anadai nije kesho nimpe muda kwanza maana hayuko poa

Nikaona poa tu, nimepita polisi nikatoa ripoti kama tahadhari maana huyu mtoto wa kitanga nimemuacha simuelewi elewi its better nichukue tahadhari isije tokea majanga nikashindwa pa kuanzia...

Leo nlivyotoka home nilienda hoteli flani nikafanya reservation kwa ajili ya dinner na S, lakini ndo ivo mambo yamekuja kua hivi, nilishatoa advance na wamesema hawa refund mtu kwa cancellation, so npo hapa na Mshkaj wangu, midume miwili in a romantic place tunapiga dinner, what else can go wrong this weekend

Ngoja niagize bia hapa akili ikae sawa...
Pouleeee
 
Gangamara na S inaelekea unampenda sana, mueleze ukweli na labda atakuelewa ila uwe tayari kujibu swali la mimba. Je ulimuacha kwa sababu ya kukimbia mimba? Una mpango gani na mtoto akizaliwa? Akili mkichwa kama kweli unampenda S kihivyo usikurupuke kuyajibu hayo maswali mawili. Vinginevyo majibu yako yanaweza kumfanya naye kuamua kuingia mitini au kuamua kutulia nawe. Mrejesho muhimu.
 
Gangamara na S inaelekea unampenda sana, mueleze ukweli na labda atakuelewa ila uwe tayari kujibu swali la mimba. Je ulimuacha kwa sababu ya kukimbia mimba? Una mpango gani na mtoto akizaliwa? Akili mkichwa kama kweli unampenda S kihivyo usikurupuke kuyajibu hayo maswali mawili. Vinginevyo majibu yako yanaweza kumfanya naye kuamua kuingia mitini au kuamua kutulia nawe. Mrejesho muhimu.
Mkuuu BAK

Swala la mimba nahisi kama nachezewa akili, hakuwahi kuniambia hapa awali, na kuhusu S nilishamueka bayana kua nilikua na mtu ila tumeachana
 
Back
Top Bottom