BabaMorgan
JF-Expert Member
- Dec 18, 2017
- 4,040
- 10,459
Ni moja kati ya washkaji wangu wa karibu nilimchukulia kama brother na mshauri sababu alinizidi umri. Kutembea na mpenzi wake haikuwa kwa bahati mbaya, nilimjua huyu Dada kupitia yeye kazi aliyoifanya ni kama middleman aliyewakutanisha buyer na seller. Alikuwa kama Dada shemeji maana hata yeye alinizidi umri tulianza kuwa na ukaribu uliopitiliza japo alikuwa ni shemeji nikajikuta naanza kumpenda na yeye akawa ananipenda huku mshikaji alikuwa hajui kinachoendelea nakumbuka masaa machache kabla ya kutunukiwa kuna maneno shemeji aliongea yaliyonifanya niamini kuwa yeye ndio soul mate wangu. Nilimuuliza kwa nini unamcheat mpenzi wako na Mimi na sio mtu mwingine aliniambia ni kwa sababu nakupenda wewe napenda unavyoongea, napenda unavyonitreat, na akaniambia anatamani azae mtoto anayefanana na Mimi. Mwisho wa siku jamaa alikuja kujua baada ya miezi mitatu kupita toka walipoachana so haikuwa ishu kubwa.