Mpendazoe kuweka wazi masuala ya kesi yake dhidi ya Mahanga Jumamosi

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Mpendazoe kuweka wazi masuala ya kesi yake dhidi ya Mahanga Jumamosi

Ndugu zangu wote katika JF, mmekuwa mnakumbuka kuwa nimekuwa nawafahamisha kuhusu kesi aliyofungua Mpendazoe dhidi ya Mahanga kwa niaba ya wapiga kura wa jimbo la Segerea. Kwa wale wote mliopo Dar es Salaam na vitongoji vyake, na hasa wananchi wa jimbo la segerea mnataarifiwa kuwa ndugu yetu, Mpendazoe aliyekuwa mshindi katika uchaguzi huo anatarajia kuongea na wananchi kuwafahamisha yafuatayo:-
  1. Mwenendo wa kesi
  2. Uchangiaji wa fedha umefikia wapi?
  3. Hatua inayofuata katika kesi hiyo.

Mkutano utafanyika viwanja vya Tabata Liwiti siku ya Jumamosi 11/12/2010 kuanzia saa tisa alasiri (bara bara ya kwenda Segerea). Kufika, panda basi linalokwenda Segerea, shuka Liwiti au endesha gari kama unaenda Segerea, kiwanja cha Liwiti kiko barabarani karibu na kanisa katoliki.

Wote mnaombwa kufika. Fika na wenzako angalau watano.

Kumbuka huu siyo mkutano wa wanachama wa CHADEMA bali wa watanzania wote hasa wapenda haki. Karibu sana.

:frown:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom