RRONDO
JF-Expert Member
- Jan 3, 2010
- 51,719
- 107,834
.
1.Wajumbe
2.Rachel Mashishanga
3.Freddy Mpendazoe.
Aliyekuwa Mbunge wa Kishapu CCM na baadae kukihama chama hicho na kuhamia Chama mfu CCJ na kuhama tena CCJ kwenda CHADEMA, Freddy Mpendazoe leo hii amebwagwa vibaya katika kura za maoni kuomba ridhaa ya wajumbe ya kugombea ubunge jimbo la Segerea.Katika uchaguzi uliofanyika ukumbi wa baa ya Seper Karatu Ukonga na kukamilika jioni hii Mpendazoe ameangushwa vibaya na Mwanamama Rachel Mashishanga kwa zaidi ya kura 20, Rachel Mashishanga amepata kura 48, ikiwa Fred Mpendazoe akiambulia kura 28 tu. Kwa matokeo hayo Rachel Mashishanga ndiye Mgombea ubunge jimbo la Segerea jijini Dar es Salaam kwa Tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
kwa hisani ya:MJENGWA BLOG.