Mpatie Ushauri Samuel!

Red Scorpion

JF-Expert Member
Feb 1, 2012
5,737
4,252
Samweli alipata safari ya kikazi kwenda Mwanza ambako kampuni yao inajenga jengo fulani, kufika akaamua kumtafuta mpenzi wake wa zamani Dorice ili apate pa kujificha kesho yake Dorice akamuomba Samweli amuazime laki tatu 3, Samweli akampa kadi yake ya ATM pamoja na nambali ya siri na kumwambia atumie vyovyote atakavyo Dorice akashangilia kwelikweli.

Samweli alifanya hivyo akijua akaunti yake ina elfu 10 tu Kabla Dorice hajaenda bank Samweli akakwea gari ili arudi Dar, njiani simu ikakata charge, kufika home akaweka kwenye Charge akalala, kuamka leo asubuhi anakuta sms kutoka kwa boss wake ikisema; Samweli nimeweka million 10 kwenye akaunti namba yako, usirudi kwanza Dar mpaka uwalipe mafundi"

... Mshauri Samweli afanyeje kwa suala hili?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom