Mpasuko mkubwa CHADEMA Mbeya mjini, Msigwa avunja uongozi huku walioondolewa wakimpinga. Ni mparaganyiko mkuu

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Mpasuko mkubwa umeukumba uongozi wa Chadema Mbeya mjini na hii ni dalili kuwa hawako kwenye good terms. Sijui lini watafika mbali

===========

Mchungaji Msigwa: Tumeuvunja uongozi wa jimbo la Mbeya mjini na tunawapa mkoa siku tatu kwa mujibu wa katiba kama nilivyosema kuunda timu(Task force) ambayo itasimamia shughuli za chama na tunaipa siku 60 iunganishe wanachama, iandae uchaguzi wa jimbo la Myeya mjini tupate viongozi walio halali

Wale wote tuliowatoa kwa mamlaka ya kanda(Kanda ya Nyasa) tuliyonayo, kuanzia sasa hawatakiwi kufanya shughuli za chama, wakiendelea kufanya shughuli za chama ni utovu wa nidhamu, hii ni mamlaka ambayo ipo kwenye kanda ila wanayo haki ya ukata rufaa, mlango uko wazi.

Mwenyekiti aliyeondolewa: Msigwa hana mamlaka na wenzake hawa watatu kuniondolea nafasi yangu mimi ya uenyekiti wa Mbeya mjini. Kwa mnaonisikiliza Mbeya mjini, viongozi wangu ninaowaongoza, relax. Kwasababu kamati ya kanda ina wajumbe kumi, wao wanaofanya maamuzi ya kihuni wako wanne.

Nimwambie tu Msigwa, haya ni maisha.. aache stress, sio kila kasa analiwa. Kwangu mimi ninajitambua, labda akasimamishe pembeni kwa wenyeviti ambao hawajitambui, hawasomi katiba.

Mimi nina miaka sasa 15 nachaguliwa kila msimu Mbeya kwahiyo constitution ya chama naijua, hata ukiniamsha usingizini naijua kuisoma katiba ya CHADEMA.

Mimi sio mwenyekiti wa... wanaowababaisha babaisha, mimi ni mwenyekiti wa mjini kwenye jiji, asiniletee mambo ya Iringa ambayo anawafukuza fukuza wenzake

 
Kutofautiana mawazo ndio dalili ya wanadamu wanaojitambua, hawawezi kufanana kila siku kwa kila kitu, hiyo issue kama imetokea haiwezi kuwa tatizo la kudumu, ni suala la muda tu litapatiwa ufumbuzi maisha yataendelea, chama chenye miaka zaidi ya thelathini hakikosi challenges za aina hiyo.
 
Mpasuko mkubwa umelikumba uongozi wa Chadema mbeya mjini na hii ni dalili kuwa hawako kwenye good terms. Sijui lini watafika mbaliView attachment 2102008
Erythrocyte kubali kataa, hii ni effect ya baba mwenye nyumba kuwa mahabusu kwa muda Mrefu. Nyumba inakosa uongozi na kila mtoto anakuwa ni decision taker. Hapa kuna tatizo maana baba msaidizi naye anag’ang’ania ubeleji! Asingekuwa mbinafsi asharudi nchini kujaza vacuum iliyoachwa na baba. Nyie mnafurahia kwenda Mahakamani na kula mandazi! Ona sasa
 
Nilisema huko nyuma CDM Mbeya hakuna kitu.
Gari kubwa la CCM liko barabarani.
Kama CCM ilivyojikaanga yenyewe 2007, sasa zamu ya CDM.
Vijana wahamie kwa Tulia.
Aiseee kweli jamaa hawa wanawatesa sanaaa mpk maji mnaita MMA.
Me nilijua hiki Chama kilishajifia tangu enzi za mtu yule kumbe kimefufuka hongera kwao kwa kufufuka.
 
Aiseee kweli jamaa hawa wanawatesa sanaaa mpk maji mnaita MMA.
Me nilijua hiki Chama kilishajifia tangu enzi za mtu yule kumbe kimefufuka hongera kwao kwa kufufuka.
CHADEMA inajitesa yenyewe, kwenye clio umesikia CCM?
 
Nilisema huko nyuma CDM Mbeya hakuna kitu.
Gari kubwa la CCM liko barabarani.
Kama CCM ilivyojikaanga yenyewe 2007, sasa zamu ya CDM.
Vijana wahamie kwa Tulia.
Huyo mwambigija kabebwa Sana lakini habebeki mwaka 2015 alituuza Rungwe bado akabebwa pamoja na kuuza chama
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom