Mpasuko Mkubwa CCM: Muungano wa TANU na ASP uliozaa CCM nao Hatarini Kuvunjika?

saggy

Senior Member
Nov 12, 2008
153
70
Kuna mjadala mkali wa Muundo wa Muungano wa Tanzania ambapo kuna maoni kinzani wengine wakitaja Serikali Mbili na Wengine wakitaka Tatu.

Napenda kuwakumbusha wana Sisiemu kwamba Chama chao ni Muungano wa Vyama Viwili yaani,TANU-Tanganyika na ASP –Zanzibar na Muungano huo uliofanyika mwaka 1977 ulikuwa na lengo kuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliofanyika mwaka 1964 na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964. Najiuliza maswali haya:-

1.Yapi yalikuwa Malengo ya Muungano wa TANU na ASP mwaka 1977?

2.Ziko wapi hati au Mkataba wa Muungano wa Vyama hivi Viwili vilivyokuwa na Sera tofauti kutoka katika nchi mbili Tofauti?

Napenda kutoa Wito kwa wana Sisiemmu wanaounga Mkono muundo wa Serikali Tatu wajue kwamba, nje ya Muungano wa Serikali mbili hakuna "CCM" bali kuna "TANU – Tanganyika na ASP- Zanzibar" .

Hivyo muundo wa Serikali Tatu utakisambaratisha Chama Chama hiki chenye nguvu kubwa na kilicho muhimili wa Umoja na Mshikamano wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa zaidi ya miaongo maika 50 hivi.

"Tanganyika, sio Sera ya Chama Cha Maaaapinduzi, kwakuwa CCM ni Muungano wa TANU na ASP" Ikiwa Muungano wa Serikali Tatu utakubalika basi Chama hiki itabidi kivunjike Vipande Viwili TANU- Tanganyika na ASP –Zanzibar hivyo kukisambaratisha kabisa Chama hiki Kikongwe na kilichosimamia Uchumi ,Umoja na Mshikamano wa Watanzania.

Hatuwezi kuzungumizia Muundo wa Muungano bila kuzungumzia Muundo wa muungano wa Chama hiki imara kabisa na Chenye nguvu nyingi.

Natoa wito kwa Wahafidhina wote kwamba sasa ni Wakati wa Kudai Kipande cha TANU- Tanganyika kutoka kwenye CCM,na wale wa Zanzibar wabaki na ASP yao.

Nawasilisha maoni yangu kwenye Jukwaa.
 
Kama sikosei katika mapendekezo ya tume ni kwamba Usajili wa vyama vya siasa ni mojawapo ya majukumu ya serikali ya muungano na si serikali za washiriki...kwa mantiki hiyo bado ccm itaendelea kuwepo km ilivyo..
 
Haitakaa itokee muungano kuvunjika hata siku moja. ccm ilikuwa imara,iko imara na itazidivkuwa imara. ccm ndio tumaini la kweli la mtanzania.
 
Kama sikosei katika mapendekezo ya tume ni kwamba Usajili wa vyama vya siasa ni mojawapo ya majukumu ya serikali ya muungano na si serikali za washiriki...kwa mantiki hiyo bado ccm itaendelea kuwepo km ilivyo..
hapo tu ndo waryoba alicheza pele.
 
Kama sikosei katika mapendekezo ya tume ni kwamba Usajili wa vyama vya siasa ni mojawapo ya majukumu ya serikali ya muungano na si serikali za washiriki...kwa mantiki hiyo bado ccm itaendelea kuwepo km ilivyo..

Mkuu kama sikosei, katika muundo wa serekali tatu, kutakuwa na pande mbili zinazounda serekali ya Muuungano, Hivyo basi katika mfumo huo itabidi kila chama kijitegemee katika kila upande (Tanganyina na Zanzibar) nina maana kuwa kama zimwi ccm halitakufa basi itabidi libasuke vipande viwili ili zaziba kuwe na kipande kimoja na mwenyekiti wao vilevile Tanganyika napo kipande cha pili na mwenyekiti wake.

Ikumbukwe kuwa jambo la usajili wa vyama sio jambo la muungano.
 
Hii mada ni ya kijinga sana

Nazungumzia Muundo wa Chama hicho kwamba ni Muungano wa Vyama viwili,Si zungumzii swala la Kisheria hapo,najua hakuna Sheria itakayokigawa Chama,ila nasema ASILI ya chama hiki ni Muungano wa Vyama vya TANU na ASP sasa kama mtu ana akili timamu anaweza kufikiri vizuri anaweza kusema kwamba je Kama Tanganyika itakuwa Pekee yake na Zanzibar Peke yake basi CCCCM ya nini?maana Tanganyika ilikuwa TANU na Zanzibar ni ASP.Hapo upo?

ASP na TANU vilikuwa vayna viwili tofauti na kila kimoja kilikuwa na Sera zake Tofauti kabisa ila ili kuuujenga Muungano imara vikaungana na kuzaa CCCCM.So Tanganyika ni TANU na Zanzibar ni ASP au Sera zao zilikuwa zinafanana?
 
Leo ndo nimefahamu kwa nini chama changu CCM bara kinaing'ang'ania Zanzibar! Du kama ni hivi naunga mkono serikali mbili hata kwa mbinde/mabomu.
 
Ni lazima wana CCCCM wanaoshabikia Serikali Tatu wawe waangalifu sana,wajue Nje ya Muungano huu wa Serikali mbili hakuna CCCCM kuna "TANU-Tanganyika na ASP-Zanzibar" na wale ambao sio wana CCCCM wajue mpasuko wa Chama hiki Kikongwe na Chenye nguvu nyingi,kilichoshikiria Umoja ,Uchumi na Mshikamano wa Watanzania kwa Miaka mingi unaweza kulisambaratisha Taifa letu la Tanzania.Shime Jamani Tuache dhambi hiyo ya ubaguzi.
 
Nazungumzia Muundo wa Chama hicho kwamba ni Muungano wa Vyama viwili,Si zungumzii swala la Kisheria hapo,najua hakuna Sheria itakayokigawa Chama,ila nasema ASILI ya chama hiki ni Muungano wa Vyama vya TANU na ASP sasa kama mtu ana akili timamu anaweza kufikiri vizuri anaweza kusema kwamba je Kama Tanganyika itakuwa Pekee yake na Zanzibar Peke yake basi CCCCM ya nini?maana Tanganyika ilikuwa TANU na Zanzibar ni ASP.Hapo upo?

ASP na TANU vilikuwa vayna viwili tofauti na kila kimoja kilikuwa na Sera zake Tofauti kabisa ila ili kuuujenga Muungano imara vikaungana na kuzaa CCCCM.So Tanganyika ni TANU na Zanzibar ni ASP au Sera zao zilikuwa zinafanana?
Hapa umefafanua vizuri lakini mbona kwenye mada umejichanganya sana? Mbona mada haiendani na kichwa cha habari? Mbona umeandika jina la ccm kijahili namna hii? Kwa sababu hakuna chama cha siasa chenye hilo jina.
 
CCM hatuwezi kushindana na wakati, ni muhimu tukarekebisha mapungufu yaliyopo sasa kuliko kukariri serikali mbili ama tatu eti ndiyo dawa ya kuimarisha muungano. Kwasasa chini ya serikali mbili bado muungano ni legelege ama haupo kwasasa kwani Zanzibar ilikwishajitoa. Ningewakubalia serikali mbili iwapo mngejadili hija ya Zanzibar wakubali kufuta Katiba yao ya 2010. Sasa wana bendera yao, wimbo wao wa taifa, watakuja kutengeneza na Sarafu yao nk huku sisi tuking'ang'amia kuwa tumeungana chini ya mwamvuli wa serikali mbili.
 
Ni lazima wana CCCCM wanaoshabikia Serikali Tatu wawe waangalifu sana,wajue Nje ya Muungano huu wa Serikali mbili hakuna CCCCM kuna "TANU-Tanganyika na ASP-Zanzibar" na wale ambao sio wana CCCCM wajue mpasuko wa Chama hiki Kikongwe na Chenye nguvu nyingi,kilichoshikiria Umoja ,Uchumi na Mshikamano wa Watanzania kwa Miaka mingi unaweza kulisambaratisha Taifa letu la Tanzania.Shime Jamani Tuache dhambi hiyo ya ubaguzi.

mkuu chama kitabaki kilivo na wala muundo wa serikali sio ishu ya kivyama, tuone mataifa kama ya marekani, je kuna vyama 52 kwamba kila jimbo/nchi ina chama chake? Take an easy example kwa kuwa umesema sio ishu ya kisheria then lets speak as laymen, tanzania tuna majimbo ya uchaguzi zaidi ya miambili ila tuna vyama visivozidi40, je ccm pamoja na vyam vyote si vinaweza kuendelea kuwa na uwakilishi kila upande wa Muungano? Sasa ukisema kila upande uwe na chama chake na je tukija kuchagua rais wa Muungano unataka kusema kuwa Zanzibar wawe na mgombea wa ccm wanayemtaka na bara iwe na mgombea wa ccm wanayemtaka? apo sasa si vyama viwili? nadhani muundo wa nchi regardless TANU na ASP unabakik ukiwa na mfumo ule ule wa vyama, tofauti itakuaja kuwa katika kuchagua serikali za washirika ccm yaweza kushinda bara ikashindwa zanzibar, na ili jambo sio geni ndo maana tuna serikali ya mseto zanzibar, ivo sio tatzo kabisa.
Tanu na Asp vilishafutwa baada ya kuunda ccm kwa ivo hakuna sheria inayosema chama chaweza kufufka baada ya kufutwa/kufa. Na asset za Asp na Tanu hazipo kabisa. Na ikumbikwe hawana cha kupoteza kwa kuwa mali za ccm ni zile zilizokuwa za Tanu na asp na ndo izo izo zilizokuwa za Tanganyika na Zanzibar,
Nitakuelea haraka ukisema CCM itabidi ife kwa kuwa WATANGANYIKA TUTADAI BARABARANI NA MAHAKAMANI MALI ZA TANGANYIKA KWA KUWA SASA NDO ZINATUMIWA NA CCM. HAPO LAZIMA IFILISIWE ILI CHA ZENJI NA TANGANYIKA KIRUDI.
 
Mkuu kama sikosei, katika muundo wa serekali tatu, kutakuwa na pande mbili zinazounda serekali ya Muuungano, Hivyo basi katika mfumo huo itabidi kila chama kijitegemee katika kila upande (Tanganyina na Zanzibar) nina maana kuwa kama zimwi ccm halitakufa basi itabidi libasuke vipande viwili ili zaziba kuwe na kipande kimoja na mwenyekiti wao vilevile Tanganyika napo kipande cha pili na mwenyekiti wake.

Ikumbukwe kuwa jambo la usajili wa vyama sio jambo la muungano.
https://www.jamiiforums.com/newreply.php?do=newreply&p=9054378



[NYONGEZA]
[Imetajwa katika Ibara ya 63]
Mambo ya Muungano:

1. Katiba na Mamlaka ya jamhuri ya muungano wa Tanzania
2. Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
3. Uraia na Uhamiaji
4. Sarafu na Benki Kuu
5. Mambo ya nje
6. Usajili wa vyama vya siasa
7. Ushuru wa Bidhaa na Mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya
muungano

##hiyo ni kwa mujibu wa rasimu ya pili ya katiba kutoka tume.....
 
Uongozi wa CCM naomba wamwombe Askofu Mtetemela awafundishe kuhusu Mfalme Belishaza wa kule Babeli, alipoona maandishi yameandikwa ukutani, alishindwa kuyasoma akalia kwa sauti, ''NENDENI MKAMUITE DANIEL"
Mengine atawafafanulia, Lakini kwa mwanajamvi kasome, Kitabu cha Nabii Daniel 5:1-31

CCM wamepigwa upofu na kiburi cha madaraka, hawawezi tena kuona kilichoko mbele yao, hawawezi kuona kilichoko nyuma yao, hawawezi kuona kilichoko kati mwao. Asomaye na afahamu.....
 
mkuu chama kitabaki kilivo na wala muundo wa serikali sio ishu ya kivyama, tuone mataifa kama ya marekani, je kuna vyama 52 kwamba kila jimbo/nchi ina chama chake? Take an easy example kwa kuwa umesema sio ishu ya kisheria then lets speak as laymen, tanzania tuna majimbo ya uchaguzi zaidi ya miambili ila tuna vyama visivozidi40, je ccm pamoja na vyam vyote si vinaweza kuendelea kuwa na uwakilishi kila upande wa Muungano? Sasa ukisema kila upande uwe na chama chake na je tukija kuchagua rais wa Muungano unataka kusema kuwa Zanzibar wawe na mgombea wa ccm wanayemtaka na bara iwe na mgombea wa ccm wanayemtaka? apo sasa si vyama viwili? nadhani muundo wa nchi regardless TANU na ASP unabakik ukiwa na mfumo ule ule wa vyama, tofauti itakuaja kuwa katika kuchagua serikali za washirika ccm yaweza kushinda bara ikashindwa zanzibar, na ili jambo sio geni ndo maana tuna serikali ya mseto zanzibar, ivo sio tatzo kabisa.
Tanu na Asp vilishafutwa baada ya kuunda ccm kwa ivo hakuna sheria inayosema chama chaweza kufufka baada ya kufutwa/kufa. Na asset za Asp na Tanu hazipo kabisa. Na ikumbikwe hawana cha kupoteza kwa kuwa mali za ccm ni zile zilizokuwa za Tanu na asp na ndo izo izo zilizokuwa za Tanganyika na Zanzibar,
Nitakuelea haraka ukisema CCM itabidi ife kwa kuwa WATANGANYIKA TUTADAI BARABARANI NA MAHAKAMANI MALI ZA TANGANYIKA KWA KUWA SASA NDO ZINATUMIWA NA CCM. HAPO LAZIMA IFILISIWE ILI CHA ZENJI NA TANGANYIKA KIRUDI.


Maelezo mazuri sana Gsana. Vilevile ni vizuri muundo wa Muungano usitegemee TANU na ASP. Je kama chama cha upinzani kitaongoza bara ama visiwani, inamaana hakutakuwa na hiyo misingi ya muungano. Ni vyema sasa tukaunda muungano halisia kwa kutengeneza katiba yenye muundo bora na kushughulikia kero halisi za muungano.
 
Last edited by a moderator:
Uongozi wa CCM naomba wamwombe Askofu Mtetemela awafundishe kuhusu Mfalme Belishaza wa kule Babeli, alipoona maandishi yameandikwa ukutani, alishindwa kuyasoma akalia kwa sauti, ''NENDENI MKAMUITE DANIEL"
Mengine atawafafanulia, Lakini kwa mwanajamvi kasome, Kitabu cha Nabii Daniel 5:1-31

CCM wamepigwa upofu na kiburi cha madaraka, hawawezi tena kuona kilichoko mbele yao, hawawezi kuona kilichoko nyuma yao, hawawezi kuona kilichoko kati mwao. Asomaye na afahamu.....

Umesema sahihi sana wala hawahitaji kufundishwa na Askofu maandiko yametafsiriwa vizuri kwa lugha wanayoielewa vizuri ya Kiswahili wachukue Biblia zao kama wanazo na wasome wenyewe hayo maandiko!
 
"Tanganyika, sio Sera ya Chama Cha Maaaapinduzi, kwakuwa CCM ni Muungano wa TANU na ASP" Ikiwa Muungano wa Serikali Tatu utakubalika basi Chama hiki itabidi kivunjike Vipande Viwili TANU- Tanganyika na ASP –Zanzibar hivyo kukisambaratisha kabisa Chama hiki Kikongwe na kilichosimamia Uchumi ,Umoja na Mshikamano wa Watanzania.

Poa tu! Tutakuwa tumeua ndege 'wawili' kwa jiwe moja...
 
Ikumbukwe kwamba Maandiko hayachakachui Historia, Kwa faida ya wasiosoma Biblia niwakumbushe machache kuhusiana na kinachoendelea kwenye Bunge la Katiba na Utawala wa Tanzania kwa Sasa,
Alikuwepo Mzee Samweli aliyewaongoza wana wa Israel kwa upendo bila upendelea, wakajengewa Umoja na Amani, Baadaye wana wa Israel wakaanza kulalamika kwamba mzee Samwel anawacheleweshea maendeleo, mara watoto wake hawakwenda katika njia sawasawa na za aba yao, walianza kupokea rushwa, dhuluma na dharau kwa wananchi, Ndipo waisarael wakadai wapate kiongozi mwingine ambaye angewaongoza kulingana na wakati na mazingira,changamoto za wakati huo.

Ndipo walipompata Sauli ambaye hakuwa na sifa ispokuwa maumbile yake, sura yake, Aliwaongoza na wakajikuta kwenye matatizo makubwa, na wakati wote huo Israel ilikuwa moja, Mungu akawahurumia ndipo akawaletea Mfalme Daudi aliye warejeshea heshima na usalama wao. Baada ya Mfalme Daudi ndipo mfalme Suleiman akarithi mikoba ya Baba yake, Baada ya Suleiman kukazuka sintofahamu ni nani atakayemrithi Mfalme Suleiman, kwa kifupi baada ya utawala wa Mfalme Suleiman na Israel ikagawanyika Kaskazini na Kusini.

Kilichokosekana ni hekima, Uzalendo, Utaifa kwanza, na mwisho wa yote hayo ni nchi kusambaratika, Mwenye Kusoma na afahamu, Kwa wenye macho ya kiroho wanaweza kuona na kulinganisha watawala wetu na Reputations zao kufuatia mchakato wa Kuandika Katiba Mpya na kinachoendelea nchini,
Samwel aliongoza wana wa Israel kwa kuzingatia mapemzi ya Mungu Wafalme wafuatao walipatikana kwa mapenzi na matakwa na sifa za kibinadamu zaidi,

1. Sauli
2. Daudi
3. Suleiman
4. Jeroboam
5. Rehoboam


Niwatahadharishe wawakilishi wetu hao, kwamba kwa vile mliapa kwa misahafu Mitakatifu, na kinachofanyika sirini ni itikadi zenu za kisiasa, hakutakuwa na njia nyepesi bali mnatuandalia mapigo kutoka kwa Mungu
 
Maelezo mazuri sana Gsana. Vilevile ni vizuri muundo wa Muungano usitegemee TANU na ASP. Je kama chama cha upinzani kitaongoza bara ama visiwani, inamaana hakutakuwa na hiyo misingi ya muungano. Ni vyema sasa tukaunda muungano halisia kwa kutengeneza katiba yenye muundo bora na kushughulikia kero halisi za muungano.

Ahsante Mkuu,Maelezo yako ni mazuri sana but mimi nazungumzia swala la tofauti ya SERA za Vyama hivi, hapa ni kwamba Muungano wa TANU na ASP uliounda CCM mwaka 1977 uliunganisha vyama viwili vyenye SERA au Mlengo Tofauti kutoka katika Nchi mbili tofauti,Tanganyika na Zanzibar kwa Lengo la kuimarisha Muungano.Sasa Huwezi kuzungumzia Kuitenga Zanzibar na Tanganyika bila kuzungumzia Muungano wa Vyama hivi Viwili vya TANU na ASP ambavyo Muungano wao Umejengwa Katika Msingi Imara wa Muungano wa Nchi hizo mbili.

My concern ni Ule msingi wa Muundo wa Chama umejengwa kwenye Muundo wa Muungano,Mwl.JK Nyerere was very clever kwakweli,alijua ameunda CCM kwenye msingi Imara wa Muungano wa Tanganyika -TANU na ASP-Zanzibar.So Ninawaonya wale wanaotaka Serikali Tatu ni lazima wajue kwamba madai yao ni kukisambaratisha Chama hiki.Kuna utata mkubwa kwenye Swala hili.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom